Kubeti: Huu Ndio mrejesho yangu niingie kwenye mchezo huu miezi 4 ilopita!!

CCNP Engineer

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2017
Posts
463
Reaction score
1,286
Nimeanza kubeti mwezi March wakat Rafik yangu alipokuja kunitembelea Ghetto na kunionesha sample ya mikeka anayokula. Nikatamani sana!!

Mwanzo nilikua muoga sana, nikawa naweka stake ya sh. 500 tu. Nikila saana nakula 900 labda. Na ikitokea nimeliwa kajero kangu hakaniumi sana. Si jero tu!!

Siku moja nipo kituo cha kubetia (Premier) nikashuhudia jamaa mmoja anaweka stake ya 450,000 kwenye Bet of the day.
Kwamba Juve, Atletico na Santos wote washinde. Odds zilikua 11.

Na kweli kesho kuchek matokeo timu zote zimeshinda.
Kwahiyo nikapiga Hesabu jamaa atakua alilamba zaidi ya Millions 4+.

Daaah... Nikashawishika.
Bet of the Day ilofatia namie nikajitutumua. Kwa Mara ya kwanza nikaweka ka 10,000 kangu nikatulia. Odds zilikua 10.
Khaaaa... Kweli nikashinda.
Kesho mapeema nikaenda pale Premier (Mwananyamala A kuelekea Komakoma) nikavuta 100,000 yangu safiii...

Basi nikazidi kupata confidence.
Kumbe kuna hela za burebure namna hii.
Basi ikawa stake zangu natupia kuanzia 10, 000 kwenda juu..
Siku nimepinda sana, naweka 5000. Mara nakula, Mara naliwa.

Nakumbuka Mara ya mwisho kula hela nyingi ni Final ya UEFA.
Bet of the day ilikua Madrid ashinde ndani ya dakika 90 na pia timu zote zifungane magoli.
Odds zilikua 7. Nikaweka stake ya 15,000.

Kweli bana, wakatoka 4-1.
Kesho nikavuta 90,000 yangu safiiii....

Nikaendelea kama kawaida.
Nakula, naliwa...

Sasa Leo :
Nikakaa chini na kufanya Auditing ya biashara hii.
Nimeliwa shingapi.
Nimekula shingapi.
Net profit shingapi.

Bahati nzuri huwa nabeti online.
Hivo records zote ninazo.
Nimepitia accounts zangu zote Mbet, Premier Bet, Sportpesa, Mkekabet na Princess Bet.

Total Profit made is 177,000.
Total Loss incurred is 397,500.
Net Profit is -220,500.

Hapo sijagusia mikeka ya bukubuku nayowekaga kila siku kwenye Jackpot ya Perfect 12 ya Mbet. Kila siku naliwa tu.

Yani kifupi ni kuwa mwisho Wa siku mimi ni Loser.

Kubeti ni mchezo Wa kuhamisha pesa toka kwa masikini kuwajazia Matajiri.
Nimeachana na habari za kubeti Rasmi Leo hii 30 July 2017.

Mdogo wenu CCNP
 
Sijawahi kula hasara kwenye kubet, kuna wakati nilikua nimeliwa zaidi ya 700k nikataka kuacha kubet, nikajipa matumaini nikatia 200k nikacheza mikeka ya 50k kwa timu 4, nikalala kuamka asubuhi mzigo unasoma 2mil, toka siku hiyo mimi na kubet ni kama mapacha, nakula nakupoteza at the end namake profit
 
Upo sahihi huu ni ulevi mbaya sana na unashusha hata thamani ya shilingi ,na inaongeza watu wenye msongo wa mawazo ningekuwa serikali nafutilia mbali kadhia hii ili watu wafanye kazi na wasiishi kwa kucheza kamari. Ona spoti pesa hizo fedha zote ni za wajinga anazoa, na naona makampuni yanaendelea kumiminika bongo hii ni hatari, unaweza kula mara moja lakini mpaka ule tena unaweza kukausha akiba yako yote
 


Kubeti ni ulevi. Acha kudanganya umma.
Mchezo Wa kubeti uko hivi, ukipatia Mara 3 unaliwa Mara 10.
Yani 30% ni Winnin stakes.
Then 70% and above ni Loosing stakes.
 
Kubet always mchezaji ndio loser in the long run, nashangaa kuna watu hapa jamiiforums wanasema ku bet ni ajirana wanadai wamejenga nyumba na wanasomesha watoto

Wapo wanao bet na wanapata faida kweli, ila hawa wapo highly disciplined na wanafanyia utafiti wa kutosha michezo kabla ya kucheza..ILA HAWASHINDI KILA MCHEZO, ila in the long run wanakuwa na net gain, Na watu hawa Tanzania hawapo, maana siamini mswahili anaweza kuwa na nidhamu kwenye jambo kama hili

Vijana fanyeni kazi hakuna pesa rahisi msidanganywe, hao wanao bet na kupata faida effort na nidhamu wanazoweka hapo ni kama mfanyakazi aliyeajiriwa anavyoweka effort na nidhamu kwenye ajira la sivyo kibarua kinaota nyasi.
 
Na bado unaendelea???
Nilipumzika kidogo kwa kuwa nilikuwa na mambo mengi. Nitarejea tena Jumanne. Unajua kubet sio mpira. Betting is mathematics! Ingekuwa its all about footbal kina Kitenge na kina Dauda wangekuwa mabilionea. Nimeunda mathematical formula kibao zinazoweza kumla mbetishaji kwa many possibilities ila tatizo nikiziweka zile kwa asilimia mia napata loss. So lazima niziweke with some probability of winning perhaps 60%. Tatizo linakujaga kutokea nikiliwa huwa nakasirika ila pia nikila nakula kidogo kwa kuwa ninakuwa nime hedge kwa kutumia stakes nyingi...
 
Analysis yako imekosewa.Hiyo loss ya 397 si wala umeliwa yote at once.Kwa kifupi haikua na hiyo hela ulikua na 10000 na 5000 tu.Ila ukiweka 10,000 ukashinda unakula 60,000 directly.Yaani wewe unampa kidogo kidogo ila wewe unachukua hela nyingi.

Sent from my iPhone 8 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…