Kubwa usilolijua kuhusu Papa Wemba (RIP)

BEHOLD

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2013
Posts
5,056
Reaction score
10,721
Papa Wemba ana "watoto wengi sana, idadi yao haifahamiki".

Watoto hawa wamezagaa ndani ya DR Congo na Nje.

Kwa sasa wanaendelea kuwasajili kabla ya maziko yake Jumanne ijayo!!!!

REST IN PEACE PAPAA.
 
Aliwasaidia wakongomani wengi kwenda ufaransa mpaka idara ya uhamiaji ilimsumbua nchini ufaransa.
 
Alivaa jeans mpaka Mobutu Sesseko akaamuru asiwe anatoka nje ya nchi maana wao ilikuwa ni vitambaa tu. Hatimaye vazi hilo kutoka America likawa maarufu sana.
 
Aliwasaidia wakongomani wengi kwenda ufaransa mpaka idara ya uhamiaji ilimsumbua nchini ufaransa.
Alifungwa nadhani mwaka mmoja kwa hiyo issue ya uhamiaji, alikuwa kila mara anakuja Congo na kuondoka na kundi la watu akisema ni wanamuziki wake na wakifika Ubelgiji ama Ufaransa anasema wamemtoroka, alifanya sana michezo hiyo, mara ya mwisho walikamatwa aliowaleta na ndio wakasema wao sio wanamuziki ila walimlipa jamaa awalete ulaya, ndio akafungwa mwaka mmoja
 
Papa Wemba ana "watoto wengi sana, idadi yao haifahamiki".

Watoto hawa wamezagaa ndani ya DR CONGO na Nje.

Kwasasa wanaendelea kuwasajili kabla ya maziko yake jumanne ijayo!!!!

REST IN PEACE PAPAA.

Ndio alikuwa mwanamziki mtanashati kuliko mwanamuziki yoyote wa DRC, hakuna Mwanamuziki wa Congo aliyekuwa anavaa kama yeye, walikuwa wakimwita Le Grand Sapeur Congolaise
 
Wabongo wangegundua hiyo wangemfuata
 
Wangemfata vipi wakati wabongo wanajifanya hawapendi kubeba mabox na wanawatukana wabeba box kila siku mtandaoni?
Mkuu wanaowasema wabeba box ni watu waliojaa na wivu tu, ni haters ambao hutafuta tu njia za kujiliwaza but kiuhalisia hata wao wanatamani kupata hiyo fursa ya "kubeba box" ila wameshindwa kuipata.
 
Papa Wemba ana "watoto wengi sana, idadi yao haifahamiki".

Watoto hawa wamezagaa ndani ya DR Congo na Nje.

Kwa sasa wanaendelea kuwasajili kabla ya maziko yake Jumanne ijayo!!!!

REST IN PEACE PAPAA.
ana watoto 9 tu
 
RIP papaa wemba. Umeacha alama duniani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…