Elections 2010 Kuchagua CCM itakuwa ni 'GRAVE MISTAKE' Kwa watanzania

Elections 2010 Kuchagua CCM itakuwa ni 'GRAVE MISTAKE' Kwa watanzania

Masauni

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2010
Posts
386
Reaction score
58
Watanzania wenzangu inabidi tuache Ushabiki na tuangalie mustakabali wa nchi yetu. Pengine tunashabikia bila kufahamu mambo haya. Kuipa kura CCM itakuwa ni 'grave mistake' kwa watanzania. Nasema hivyo kwa sababu zifuatazo

  • CCM ikiingia madarakani itakuwa ni kama imepewa go ahead na ufisadi, watafanya ufisadi kama kawaida na hata wapinzani wakipinga bado watakuwa na strong point kwamba kama CCM ni mafisadi mbona wananchi walitupa ridhaa ya kuongoza nchi? hakuna mtanzania hatakaye weza kujibu swali hilo.(swala la kuiba kura halitakuwepo hapo)

  • Ishu za kagoda, meremeta, kiwira ndo zitakuwa zimezikwa rasmi HUTAZISIKIA TENA, na hata wapinzani wakitaka kuibua kashfa itakuwa ni ngumu kwa maana watawambia si mliwaeleza wananchi kuhusu ufisadi huo,kama ni kweli si wangewapa ridhaa ya kuongoza nchi, watasema siku zote wapinzani ni waongo

  • Lowasa na wenzake watakuwa na nguvu kubwa sana ya kurudi serikalini na hata kugombea Uraisi. kwa kigezo cha kwamba kama kashfa zake zilikuwa za kweli mbona wananchi walimchagua tena kwa kishindo(Mtanzania uliye makini kumbuka maneno ya kikwete alipokuwa akimnadi lowasa,mramba)
  • CCM watahakikisha wanaweka sheria ngumu mno kwa wapinzani kuhakikisha kwamba they will never ever try to challenge the ruling party CCM.
Na ndo maana nasema ni pigo kubwa kwa watanzania kwa sababu tatizo kubwa ni ufisadi ambao unaathiri uchumi si wataifa tu hata wa mtu mmoja mmoja
 
Ni kweli Mkuu,
sasa kazi yetu kubwa ni kufanya kila namna kwa nafasi zetu kwa jamii kuwashawishi, ndugu jamaa marafiki kuhusu umuhimu wa kulielew hilo
 
mzee hapa nakubaliana na wewe kitakuwa ni kipindi cha lala salama kwa jk hatajali mtu, si watu watakuwa wamempigia kwa kiherehere chao
 
Masauni

kweli kabisa hii chance tukiichezea mafisadi wata jizatiti zaidi.

ole wetu
 
Wanasubiri kupata ridhaa ya kushika serekali ili waweze kufanya biashara ya Kigamboni kwa usalama zaidi.
hata hivyo pesa inayopatikana hapo mlimani city itafichuliwa kuwa ni nani anayeichukua.
wako tayari kwa lolote kuhakikisha wanaingia madarakani hata kwa kumwaga damu ya watu wachache.
 
Burke [Edmund] was horrified at the thought that individuals would use abstract reason to sweep away arrangements that had stood the test of time. He believed in continual reform, but reform is not novelty. You don’t try to change the fundamental substance of an institution. You try to modify from within, keeping the good parts and adjusting the parts that aren’t working.

If you try to re-engineer society on the basis of abstract plans, Burke argued, you’ll end up causing all sorts of fresh difficulties, because the social organism is more complicated than you can possibly know. We could never get things right from scratch

I believe we can all use a little Burkenism in this coming election--
 
Back
Top Bottom