Kuchanganya udongo wa Zanzibar na Tanganyika haiwezi kuwa ni kifungo kwetu cha daima?

Kuchanganya udongo wa Zanzibar na Tanganyika haiwezi kuwa ni kifungo kwetu cha daima?

Pendaelli

JF-Expert Member
Joined
Feb 13, 2014
Posts
11,050
Reaction score
31,412
Salamu kwa wote na heri za maadhimisho ya kumbukumbu ya muungano wetu.

Tuna kila sababu ya kuwapongeza waasisi wetu kwa kuwa na fikra chanya za kutaka kuungana na hatimaye ikawa hivyo.

Umoja, undugu, mshikamano kwa kiasi kikubwa imekuwa sababu ya kupelekea maendeleo ya moja kwa moja kwa wale wanaoungana iwe ni taifa au kikundi au mtu mmoja mmoja.

Lakini kama ilivyo ada ya mwanadamu asivyo mkamilifu na asiyejua kwa ukamilifu lililo mbele yake, kunaweza kukawa na error zinazoweza kujitokeza na kupelekea kuona ile sababu ya kuungana haipo tena, na suluhu pekee ni kuvunja au kusimamisha kwa muda huo muungano.

Hapa kwetu wakati ule mataifa haya yalipoungana lilifanyika tunaweza kusema tendo la Kiibada la kuchanganya udongo wa mataifa haya.

Kitendo kile tunaweza kusema au kuona ni cha kawaida lakini kimantiki kina maana kubwa sana na kiasi inaweza kuleta gharama kubwa iwapo itafanyika kinyume chake.

Siku ikitokea inatakiwa muungano usitishwe, itawezekana je kuutenganisha ule udogo uliochanganywa?

Wajuzi wa mambo ya kiroho labda wanaweza kutujuza labda kuna ibada inayoweza kutenganisha automatically.
View attachment 2599824
 
Hapa kwetu wakati ule mataifa haya yalipoungana lilifanyika tunaweza kusema tendo la Kiibada la kuchanganya udongo wa mataifa haya.

Kitendo kile tunaweza kusema au kuona ni cha kawaida lakini kimantiki kina maana kubwa sana na kiasi inaweza kuleta gharama kubwa iwapo itafanyika kinyume chake.

Siku ikitokea inatakiwa muungano usitishwe, itawezekana je kuutenganisha ule udogo uliochanganywa?

Wajuzi wa mambo ya kiroho labda wanaweza kutujuza labda kuna ibada inayoweza kutenganisha automatically.
View attachment 2599824
Udongo ndio element kuu ya dunia hii. Mungu alimuumba binadamu kwa udongo na mwisho wa maisha mafupi ya dunia hii, binadamu hurejea mavumbini!.

Kitendo cha kuchanganya udongo ndio muungano wenyewe for life, hakuna kutengana kwasababu huwezi kuutenganisha ule udongo, ni maagano na ndio maana sisi Wazalendo tunasema Muungano wetu huu adhimu, tutaulinda kwa gharama yoyote!.
P
 
Kwa teknolojia ya sasa inawezekana kabisa kuutenganisha udongo ule. Kifupi hata wakati ule ule iliwezekana kuutenganisha. chembe za udongo wa maeneo tofauti zina density, size, shape, ...tofautitofauti.
 
Udongo ndio element kuu ya dunia hii. Mungu alimuumba binadamu kwa udongo na mwisho wa maisha mafupi ya dunia hii, binadamu hurejea mavumbini!.

Kitendo cha kuchanganya udongo ndio muungano wenyewe for life, hakuna kutengana kwasababu huwezi kuutenganisha ule udongo, ni maagano na ndio maana sisi Wazalendo tunasema Muungano wetu huu adhimu, tutaulinda kwa gharama yoyote!.
P
Basi ni moja kwa moja wale viongozi walioafiki na kutekeleza hilo hawakuwaza upande wa pili wa athari zinaweza kutokea kwa kitendo hicho
 
Sasa tunachanganya damu.
Mzee Julius anatoka ukoo wa machifu kule Butiama. Ukoo huu kwa kawaida uliendeshwa na kusimamiwa na miungu (mapepo?). Mzee kwa namna moja au nyingine alikiwa mshirikina sema suti zinawasetiri wasomi wetu sana.
Kuna vitu viwili vinafanyika Nchi hii vilivyoasisiwa na Mzee huyu; Muungano, na, Mwenge. Kama ulivyogusia kwa mbali inatakiwa kuwa na uangalifu mkubwa na wa ziada tunaposhughulika na mambo haya mawili kwani yanahusisha nguvu za ulimwengu wa roho (mizimu?). Moja ya siri wanazoapishwa viongozi wakubwa wa Nchi hii ni kitogusa maeneo haya mawili na kwamba yanatakiwa kulindwa kwa gharama yoyote. Hili tumeliona kwa viongozi wetu waliopokezana vijiji.
Aidha, Mzee aliwahi tahadharisha kipindi kile Mzee ruksa analotupilia mbali Azimio la Arusha, ... Futeni kila kitu nilichoanzisha, lakini msidhubutu Kuvunja muungano, na, Mbio za Mwenge, mkifanya hivyo kitakachokuja kuipata Nchi, asilaumiwe. Aliomba iwapo watatekeleza, basi, wafanye hivyo akiwa hayupo duniani (bila shaka kama hivi) lakini kitakachoisibu nchi anajua Mungu. Ngahwe, habari ndiyo hiyo!
 
Back
Top Bottom