Kuchelewesha mafao ya wastaafu inauma, inasisimua nafsi, inawaondolewa walipaji baraka na kuwapaka laana

Kuchelewesha mafao ya wastaafu inauma, inasisimua nafsi, inawaondolewa walipaji baraka na kuwapaka laana

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
Nchi ina vipaombele lakini suala la mafao linapaswa kuwa kipaombele Cha Kwanza. Nipo na watu waliostaafu utumishi wa Umma wengi wakiwa walimu na wahudumu wa afya, Wana maisha magumu.

Tafakari walikua na mshahara mdogo kwa maisha yao yote ya utumishi, wakafanya kazi kwa kujibana wasomeshe watoto. Leo wamestaafu hawana
-Hawana mshahara
  • Pensheni kwa maana mafao ya mkupuo
  • Hawana malipo ya mwezi

Hawa watu wamehama wamerejea kijijini, wengine wamebaki mjini na watoto wao bado awajapata ajira..inaumiza sana.

Kibaya zaidi wanajitahidi kutumia kidogo walichonacho kufuatilia, kila siku wanapigwa Tarehe na wanaowapiga Tarehe kwa kuwadanganya wengi wao ni watoto wao yaani vijana waliojiriwa hivi karibuni. Unakutana na mzee amebaki kuwalaani wafanyakazi wa mifuko ya jamii hadi unajiuliza tatizo ni mifuko au tatizo ni kipaumbele Cha serikali. Hivi kweli viongozi waandamizi awajui nani anastaafu lini?

Lakini kibaya zaidi, wakubwa wote mara tu wanapostaafu wanaingiziwa chao. Hakuna mbunge, mkurugenzi, DC, Katibu tawala na wakuu wa Idara anayestaafu akakaa mwaka bila kulipwa mafao....je Hawa watumishi wa chini wanatofauti gani na hao wakubwa zao?

Tuwaonee huruma Hawa maana stress na umri zinawaondoa mapema bila hata kupata mafao yao matokeo yake watoto wanapigania mafao na wengine kufarakana Kama siyo kuuwana.

WALIPENI HAKI YAO, HATI MKIWALIPA FEDHA WALIZOKUWA WANAKATWA ITASAIDIA WAKATI MNATAFUTA FEDHA ZA MWAJIRI NA MFUKO HUSIKA.

MWENYENZI MUNGU ALAINISHE MIYOYO YENU MKAWATAZAME HAWA WAZAZI WENU KWA JICHO LA HURUMA
 
Nina mzee Wangu amestafu toka mwezi wa NNE hadi leo hajapata mafao yake kila akienda kuulizia kuli ni hizi zifatazo,

Faili liko ukaguzi, faili bado liko uhasibu ,faili liko malipo, faili liko kwenye kuandikiwa Hundi , ghafl kalete taarifa ya uhakiki wa vyeti Mara nenda tu tutakujulisha, Mara kuna michango ya miezi miwili haikuwasilishwa Mara ....

Ki ukweli mzee amemaliza nauli kutoa misenyi kwenda dodoma . ina kera sana.
 
Na kuanzia mwakani ni lazima wastaafu wote ni wawe na uthibitisho wa kustaafu ikiwemo barua vinginevyo hawatalipwa haki zao. Mkakati wa hawa madhalimu kuwadhulumu wastaafu mabilioni yao waliyoyatolea jasho kwa miaka chungu nzima.
 
Aisee...

This is too bad...

Liko tatizo mahali, sio bure...

Hata mimi ninao wazee wawili ninaowafahamu wamestaafu tangu January, 2020 mpaka sasa hawajalipwa hata senti tano...

Tatizo ni nini? Mpango wa serikali ni nini kwenye eneo hili la mafao ya wastaafu? Wamekosa nini hawa wazee?

Mbona kweli nyie wabunge mafao yenu huwa yanalipwa hata kabla bunge halijavunjwa? Nini tatizo kwa watumishi wadogo hawa walioitumikia nchi hii kwa miaka wengine kati ya 30 - 35...??

Pesa zao ziko wapi?
 
Kuna Mzee AMESTAAFU toka Julai 2018 mpaka leo Wanazungushwa anaambiwa Apeleke Majalada binafsi ya Sehemu zote alizofanya kazi(kuhamishwa)
 
Itakuwa hela zinapelekwa katika ununuzi wa ndege.
 
Acha uongo hakuna mstaafu ambaye inapita miezi mitatu bila kulipwa mafao yake ya kustaafu kama taarifa za kuajiriwa kwake zipo sawa na penseni ya kila mwezi hulipwa baada ya mwezi mmoja ama miwili baada ya kustaafu. Kitu kikubwa ni kuweka taarifa zake za uajili vizuri mapema ikiwemo Salary Slip.
Nimeamini kuna watu wanachangia mambo wasiyoyajua , huyu ni mmoja wapo!
 
Mwenyewe hata ajali yy bora na familia yake na washirika wake wana kula bac yy anaona okay .
Hili litaleta changamoto kwa serikli ya awamu ya 6 watakuwa na.mzigo wa madeni kulipa sijui itakuwaje duh
 
Jiwe yuko juu ya sheria (ni dikteta). Hata akiwanyima mafao au kuwapunguzia mishahara hakuna la kumfanya. Yeye ndiye "mungu" wa watanganyika
 
Wapo baadhi ambao kweli kwa hili nitawaonea Huruma na naomba Wahusika wahakikishe wanalifanyia Kazi haraka hili Jambo na wapate Haki yao. Ila kuna wale ambao walikuwa kabisa katika 'Mfumo' na walikuwa wakipata 'Kipato' kikubwa mno tu walipokuwa Kazini lakini 99% ya Pesa zao zimeishia katika Kutombea, Kuhonga, Kujengea Vimada Nyumba na kuwa 'very extravagant in spending' huku 'wakijisahau' Kujipanga kwa Maisha yao ya 'Uzeeni' ya sasa. Hawa wala siwaonei Huruma na kama kwa sasa 'Cha Moto' wanakiona naomba waendelee 'Kupigika' tu Kudadadeki!
 
Acha uongo hakuna mstaafu ambaye inapita miezi mitatu bila kulipwa mafao yake ya kustaafu kama taarifa za kuajiriwa kwake zipo sawa na penseni ya kila mwezi hulipwa baada ya mwezi mmoja ama miwili baada ya kustaafu. Kitu kikubwa ni kuweka taarifa zake za uajili vizuri mapema ikiwemo Salary Slip.
Mwogope Mungu ndugu, hao wanaozungumziwa hapo ni wazee.. Ikitokea Mwalimu kalipwa ndani ya mwaka ujue ana ndugu huko nssf.
 
Acha uongo hakuna mstaafu ambaye inapita miezi mitatu bila kulipwa mafao yake ya kustaafu kama taarifa za kuajiriwa kwake zipo sawa na penseni ya kila mwezi hulipwa baada ya mwezi mmoja ama miwili baada ya kustaafu. Kitu kikubwa ni kuweka taarifa zake za uajili vizuri mapema ikiwemo Salary Slip.
Wewe hata shetani akikuona atakuwa anajiuliza imewezekanaje binadamu kuwa na roho mbaya kumzidi yeye
 
Wazazi hawa na wastaafu walizembea kudai katiba mpya enzi zao,walipoona shwari wakanyamaza,sasa farao asiyemjua yusuph anatawala
 
Acha uongo hakuna mstaafu ambaye inapita miezi mitatu bila kulipwa mafao yake ya kustaafu kama taarifa za kuajiriwa kwake zipo sawa na penseni ya kila mwezi hulipwa baada ya mwezi mmoja ama miwili baada ya kustaafu. Kitu kikubwa ni kuweka taarifa zake za uajili vizuri mapema ikiwemo Salary Slip.
Ungeacha ku comment,ingetosha!!
 
Ikiwa watahurumiawa tumshukuru Mungu! Yangu macho. Aliyeshiba hamkumbuki mwenye njaa!
 
Acha uongo hakuna mstaafu ambaye inapita miezi mitatu bila kulipwa mafao yake ya kustaafu kama taarifa za kuajiriwa kwake zipo sawa na penseni ya kila mwezi hulipwa baada ya mwezi mmoja ama miwili baada ya kustaafu. Kitu kikubwa ni kuweka taarifa zake za uajili vizuri mapema ikiwemo Salary Slip.
Tofauti yako na kondoo ni harufu tu
 
Acha uongo hakuna mstaafu ambaye inapita miezi mitatu bila kulipwa mafao yake ya kustaafu kama taarifa za kuajiriwa kwake zipo sawa na penseni ya kila mwezi hulipwa baada ya mwezi mmoja ama miwili baada ya kustaafu. Kitu kikubwa ni kuweka taarifa zake za uajili vizuri mapema ikiwemo Salary Slip.
Wewe mlamba viatu vya magu hujatosheka Hadi uamue kutumia avatar yenye jina lake? Ulichoandika hapo juu kinaonyesha mahaba matakatifu iliyokuwa nayo juu yake hata Kama Kuna eneo halitendei haki hasa hili la mafao ya wastaafu na ulimbikwaji wa madeni alioapa kutokuyafumbia macho kwa wanaochelewesha!
Kwa kuwa unaishi kimhemko na huna ushahidi wa yanayoendelea ground Basi unahorojeka tu!
 
Back
Top Bottom