Etugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 6,514
- 15,247
Alhamdulillah Ijumaa ishaingia na si vibaya kukumbushana mawili matatu.
Hakika Ulimi ni kiungo kidogo lakini hakika madhara yake ni makubwa mno katika Maisha yetu hapa duniani na kesho Akhera.
Watu wengi huenda hatutambui kuwa hakika halitoki Neno lolote kinywani kwetu isipokuwa linaandikwa na Waandishi watukufu ambao ni Malaika,hata huku kuandika kwetu kuna ratibiwa pia.
Mwanadamu hujiona yupo huru kuongea chochote atakacho lakini hajui hakika Mwenyezi Mungu ana waandishi Maalum ambao wapo tayar 24/7 kuweka kumbukumbu zetu katika madaftari maalum ambayo yataletwa siku ya Mwisho kama ushahidi WA Yale tulivyo Kwisha kuyatanguliza.
Allah (Subhanahu wataala) anasema:
(Hatoi kauli yoyote isipokuwa karibu naye yupo mpokeaji tayari (kuandika)).
[Hujurat : 6 ]
Katika hadith Mtume (rehma na Amani iwe juu yake) amesema "Yule atakayenipa dhamana ya kile kilichopo baina ya midomo yake miwili,na kile kilicho baina ya miguu yake miwili. Nitampa dhamana ya Jannah."
(Bukhari).
Kwa maana Yule atakaye chunga Ulimi wake na kulinda tupu yake asifanye zinaa basi ataombewa aingie peponi
Harith bin Hishim (r.a) amesimulia "Nilimuomba Mtume (s.a.w) "Nipe habar juu ya Jambo ninalo weza kulishika vizuri". Mtume akamwambia "akiashiria katika Ulimi wake na kusema: "Udhibiti huu" akimaanisha ULIMI.
Uqbah bin Amr (r.a) amesimulia kuwa nilisema "Ewe Rasullallahi! Ni ipi njia ya uokovu?" Akasema " Uchunge Ulimi wako,Baki ndani ya nyumba yako na Lia Kwa madhambi yako" (Tirmidhi).
Maelezo: Kuuchunga Ulimi wake ina maana usitumiwe Kwa maovu mfano kusengenya,kuzua,mazungumzo ya utovu wa adabu, mazungumzo yasiyo ya lazima, mazungumzo ya ovyo ovyo, kuzozana, kutukana, kuwalaani watu na wanyama, kushughulika na mashairi Kwa wingi, kufanya mzaha, kufichua Siri, kutoa ahadi za uongo, viapo vya uongo, udanganyifu, kusifu mno Bila kiasi na kuuliza maswali yasiyo hitajika.
Kwahiyo hakika Ulimi ni wa Kuuchunga Sana, mifarakano mingi katika familia zetu na jamii yetu chanzo chake ni Ulimi, mtu atatoa huku neno na kuipeleka Kule na mwisho wa siku fitina inaanzia hapo.
Ndio maana watu wenye hekima zao wanasema "Kunyamaza wakati mwingine ni Bora zaidi kuliko Kuongea". Na mara nyingi mtu atakujaji kutokana na mazungumzo yako, kutokana na kauli zako utafahamika Tabia zako na mitazamo yako pia.
Kama hakuna sababu ya kuzungumza basi kaa kimya kwani ni kheri kwako kuliko kuzungumza mazungumzo yasiyo faa na yenye kuchukiza na matokeo yake unapata dhambi.
Na vile vile tunashauriwa Sana tuepuke Sana mazungumzo ya kipuuzi, Mwenyezi Mungu anasema waumini WA kweli ni wale ambao hata wanapo kuta mazungumzo ya kipuuzi wao hupita mbali na kuyaepuka.
Mtume Muhammad (rehma na Amani ziwe juu yake) aliulizwa ni mambo gani yatawaingiza watu Sana Motoni? Akajibu ni kile kilicho katikati ya midomo miwili na kilicho katikati ya miguu miwili, navyo ni Ulimi na Uchi ( Kwa maana ya zinaa).
Waswahili Wana msemo wao wanasema "Mdomo uliponza kichwa" kuashiria kwamba hakika mdomo ndio chanzo cha matatizo na mabalaa yote.
Nakala Kwa:
Nurain
Msonjo
baby zu
Kazakh destroyer
Ni hayo tu!
Hakika Ulimi ni kiungo kidogo lakini hakika madhara yake ni makubwa mno katika Maisha yetu hapa duniani na kesho Akhera.
Watu wengi huenda hatutambui kuwa hakika halitoki Neno lolote kinywani kwetu isipokuwa linaandikwa na Waandishi watukufu ambao ni Malaika,hata huku kuandika kwetu kuna ratibiwa pia.
Mwanadamu hujiona yupo huru kuongea chochote atakacho lakini hajui hakika Mwenyezi Mungu ana waandishi Maalum ambao wapo tayar 24/7 kuweka kumbukumbu zetu katika madaftari maalum ambayo yataletwa siku ya Mwisho kama ushahidi WA Yale tulivyo Kwisha kuyatanguliza.
Allah (Subhanahu wataala) anasema:
(Hatoi kauli yoyote isipokuwa karibu naye yupo mpokeaji tayari (kuandika)).
[Hujurat : 6 ]
Katika hadith Mtume (rehma na Amani iwe juu yake) amesema "Yule atakayenipa dhamana ya kile kilichopo baina ya midomo yake miwili,na kile kilicho baina ya miguu yake miwili. Nitampa dhamana ya Jannah."
(Bukhari).
Kwa maana Yule atakaye chunga Ulimi wake na kulinda tupu yake asifanye zinaa basi ataombewa aingie peponi
Harith bin Hishim (r.a) amesimulia "Nilimuomba Mtume (s.a.w) "Nipe habar juu ya Jambo ninalo weza kulishika vizuri". Mtume akamwambia "akiashiria katika Ulimi wake na kusema: "Udhibiti huu" akimaanisha ULIMI.
Uqbah bin Amr (r.a) amesimulia kuwa nilisema "Ewe Rasullallahi! Ni ipi njia ya uokovu?" Akasema " Uchunge Ulimi wako,Baki ndani ya nyumba yako na Lia Kwa madhambi yako" (Tirmidhi).
Maelezo: Kuuchunga Ulimi wake ina maana usitumiwe Kwa maovu mfano kusengenya,kuzua,mazungumzo ya utovu wa adabu, mazungumzo yasiyo ya lazima, mazungumzo ya ovyo ovyo, kuzozana, kutukana, kuwalaani watu na wanyama, kushughulika na mashairi Kwa wingi, kufanya mzaha, kufichua Siri, kutoa ahadi za uongo, viapo vya uongo, udanganyifu, kusifu mno Bila kiasi na kuuliza maswali yasiyo hitajika.
Kwahiyo hakika Ulimi ni wa Kuuchunga Sana, mifarakano mingi katika familia zetu na jamii yetu chanzo chake ni Ulimi, mtu atatoa huku neno na kuipeleka Kule na mwisho wa siku fitina inaanzia hapo.
Ndio maana watu wenye hekima zao wanasema "Kunyamaza wakati mwingine ni Bora zaidi kuliko Kuongea". Na mara nyingi mtu atakujaji kutokana na mazungumzo yako, kutokana na kauli zako utafahamika Tabia zako na mitazamo yako pia.
Kama hakuna sababu ya kuzungumza basi kaa kimya kwani ni kheri kwako kuliko kuzungumza mazungumzo yasiyo faa na yenye kuchukiza na matokeo yake unapata dhambi.
Na vile vile tunashauriwa Sana tuepuke Sana mazungumzo ya kipuuzi, Mwenyezi Mungu anasema waumini WA kweli ni wale ambao hata wanapo kuta mazungumzo ya kipuuzi wao hupita mbali na kuyaepuka.
Mtume Muhammad (rehma na Amani ziwe juu yake) aliulizwa ni mambo gani yatawaingiza watu Sana Motoni? Akajibu ni kile kilicho katikati ya midomo miwili na kilicho katikati ya miguu miwili, navyo ni Ulimi na Uchi ( Kwa maana ya zinaa).
Waswahili Wana msemo wao wanasema "Mdomo uliponza kichwa" kuashiria kwamba hakika mdomo ndio chanzo cha matatizo na mabalaa yote.
Nakala Kwa:
Nurain
Msonjo
baby zu
Kazakh destroyer
Ni hayo tu!