Kudadeki

Nazjaz

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2011
Posts
7,730
Reaction score
9,088
Nini maana ya masamiati huu "kudadeki"?
 
Neno hili nadhani linatokana na neno afanaleikh. Kwa kweli sifahamu maana ya neno afanaleikh.
Kudadeki leo limekuwa neno la kuonyesha mshangao au hamaki.
Zaidi hutumiwa na vijana
 
nielewavyo hiyo kudadeki ni swahili slang...kuashiria mshangao au kuduwazwa na kitu..
 
Neutralization ya term nyingine inayotumia ile jinsi nyingine (ke), tusi linalotumika katika muktadha usiokuwa rasmi kuonesha mshangao pia!

tusi likiwa neutralized je linaendelea kuwa tusi au?
 
tusi likiwa neutralized je linaendelea kuwa tusi au?

Kwa kesi ya hili nadhani linaendelea kuwa tusi, sababu hapa linatumika tu pale ambapo mzungumzaji yupo kwenye mazingira ambayo anahisi hataweza kutumia neno lile la mwanzo

Wachagga (wa Marangu) wakishangaa wanaweza kutumia neno 'mbula' ambayo ni tusi ila kutokana na mazingira wanaweza kutumia 'mbura' ambayo haina hata maana.
 
kudadeki ni mzizi wa neno.
Kudadeki ni shina la neno
kudadeki ni tawi la neno.
Kudadeki ni majani ya neno.
Kudadeki ni kila kitu kudadadeki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…