Kudaiwa maegesho yasiyo halali

Kudaiwa maegesho yasiyo halali

bnhai

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2009
Posts
2,832
Reaction score
2,390
Kuna tukio limetokea naona ni vyema niwaambie na wengine ili muwe waangalifu. Nina kawaida ya kuingia termis ya TARURA kucheki gharama ya maegesho na wakati fulani hupata alert za kuonesha ninachodaiwa.

Nimekuwa nikilipa kweli. Nikaamua kufuatilia hizo bili. Kucheki, nyingi huwa gari haitumiki na ipo nyumbani.
Kuweni waangalifu na huu ulipaji kuna jambo halipo sawa.

Ni bora wanavyofanya ticketing waweke camera au user awe anathibitisha huo usahihi
 
Kuna tukio limetokea naona ni vyema niwaambie na wengine ili muwe waangalifu. Nina kawaida ya kuingia termis ya TARURA kucheki gharama ya maegesho na wakati fulani hupata alert za kuonesha ninachodaiwa.

Nimekuwa nikilipa kweli. Nikaamua kufuatilia hizo bili. Kucheki, nyingi huwa gari haitumiki na ipo nyumbani.
Kuweni waangalifu na huu ulipaji kuna jambo halipo sawa.

Ni bora wanavyofanya ticketing waweke camera au user awe anathibitisha huo usahihi
Vijana wanapewa target kubwa ya makusanyo, matokeo yake wanaumiza watu sana ili kufikia malengo. Kuna unfair ticketing, yani ni kama wizi uliohalalishwa. Halafu ni majeuri na wako hostile sana.. kwa sasa ni kawaida kuja mtaani nyumbani kukuandikia hata mahala ambapo si hifadhi ya barabara alimradi wawe wanaiona plate number yako.. DHULMA NA UONEVU
 
Vijana wanapewa target kubwa ya makusanyo, matokeo yake wanaumiza watu sana ili kufikia malengo. Kuna unfair ticketing, yani ni kama wizi uliohalalishwa. Halafu ni majeuri na wako hostile sana
Huu upuuzi inabidi kwenda nao mahakamani
 
mara kadhaa nimewekewa bill toka dodoma na morogoro na nilipojaribu kufuatilia hapo anatouglou zilipo ofisi za tarura sikupata majibu stahiki zaidi ya kuambiwa suala langu litafanyiwa kazi.
 
Taarifa zote ziungwe na namba za simu, haiwezi mpaka leo bado hatujaweza kuunga hizo taarifa na mifumo ikawa ama inasoma au ukawa mmoja wenye level tofauti za access kulingana na idara.

- Cheti cha kuzaliwa, hapa ni lazima wakusanya taarifa za wazazi wote wawili, zote.

- Kitambulisho cha mpiga kura, hapa pia wanakusanya taarifa zote za mhusika ambazo zitalinganisha na hapo juu kimfumo! Mawasiliano lazima yawepo.

-
NIDA, hii ni lazima wachukue taarifa za kutosha kabisa, ambapo ulinganifu utafanywa na hivyo vilivyotangulia...hapa ni lazima iwe kitambulisho chenye sim/chip, kibebe mpaka taarifa za blood group, rangi ya macho, nywele, urefu, disability, next of kin, wazazi wote wawili, watoto, mwenza, level ya elimu, ajira, TIN, etc.

- Pasi ya kusafiria, inapata taarifa zote kutoka zilizotangulia juu pote, iwe ni suala la kuomba, weka finger print, kitu unaipata ndani ya masaa 24.

- Leseni ya udereva, hii pia iwe ni ya kupakuliwa kutoka kwenye taarifa zilizopo, kwenye display ioneshe na blood group.

Usajili wa vingine vyote ujikite kwenye kupata taarifa kwenye hivyo vitambulisho, kadiri maboresho yanavyotakiwa, kuna idara zipewe uwezo wa ku-update(bila kufuta taarifa zilizokwisha tangulia, ioneshe nani ameongeza taarifa pia) profile ya mhusika, iwe Hospitali, Polisi na Mahakama, Mamlaka ya vyuo na Shule.

Wanawezaje kupata namba kutuambia habari za utapeli na shughuli za kizimkazi washindwe kuunga taarifa zote?
- Number plate ikishakuwa scanned, itume ujumbe moja kwa moja kwa namba sajiliwa kwa taarifa zaidi!
 
Kuna tukio limetokea naona ni vyema niwaambie na wengine ili muwe waangalifu. Nina kawaida ya kuingia termis ya TARURA kucheki gharama ya maegesho na wakati fulani hupata alert za kuonesha ninachodaiwa.

Nimekuwa nikilipa kweli. Nikaamua kufuatilia hizo bili. Kucheki, nyingi huwa gari haitumiki na ipo nyumbani.
Kuweni waangalifu na huu ulipaji kuna jambo halipo sawa.

Ni bora wanavyofanya ticketing waweke camera au user awe anathibitisha huo usahihi
Sometimes napata bill alert ya maegesho kwa gari iliyo Kahama ambako hakuna utaratibu huu wa TARURA wa madai ya kielektroniki coz huku tunalipa cash mkononi tu
 
Back
Top Bottom