Kudeka na Kuringa

CAMARADERIE

JF-Expert Member
Joined
Mar 3, 2011
Posts
4,419
Reaction score
1,923
Jana nikiwa kaunta ulizuka mjadala kuhusu mdau mwenzetu na ndoa yake. Kuna waliodai kuwa mkewe ana maringo sana na wengine wakidai mume anamdekeza sana. Binafsi sikuchangia kwa kuwa haya maneno yalinichanganya na wanywaji wale hawakunisaidia kuelewa japo sikuwa nimelewa. Nini tofauti ya hizi hali na madhara yake?
 

Mi naona maringo ni tabia ya mtu ambayo ni mbaya sana(technically speaking no human being is better than another). Kudekezwa ni mtu kuelekea kwenye maringo na tabia zingine mbovu kwa sababu tu mtu muhimu aliyetakiwa kumkataza na kumuelekeza kwema ameshindwa kuplay hiyo part yake muhimu, halafu mbaya zaidi unakuta anashabikia kuharibika huko...
 
Watu kazi kutazama ya wengine, mke wa jamaa akiringa, au asiringe inawahusu nini.

Kadekezwa na mme wake au asidekezwe...ni mke wake sio wenu.

Afu cha jabu wanaume ndo wanao ongea maneno hayo, yani ajabu siku hizi wanawake wamekuwa hawana maneo kama wanaume, kweli dunia inaenda kwenye speed za mwisho.
 
Hii ya kudeka kuna watu huwa wana mitazamo ya kipumbavu sijapata kuona. Mtu hawamjui lakini wanahitimisha kuwa anadeka.

Kwanza kudeka ndiyo nini?
 
kudekeshwa automatically kunaletwa maringo and not vice versa. I have live evidence on this I can vouch for
 

Simple minds discuss people but great minds discuss issues and events. Shame on you!!
 
mhhh??kudekezwa ni hali ya kuendekezwa na mtu,kwa kukupa au kukufanyia kila unachotaka hata kama una uwezo wa kufanya au kupata mwenyewe au kina madhara fulani.na mara nyingi anaedeka huwa anaomba tu kufanyiwa na utekelezaji unafuata,na mdekaji huwa huru kufanya atakavyo.
 
Watu wengine bana.......kama huwezi kuchangia bora kukaa kimya.......hoja ni maana na tofauti kati ya kudeka na kuringa......watu wanajadili mfano uliotumika
 

Marhabaaaaa..........................


Ashakum si matusi....acha tu tuletewe ile hoja ya huko kwa waingereza

Mke wa mtu anajiringia zake na wala hajamdharua mtu la hashaaaa
Anadekezwa na mumewe maashallah na wala hajawa mvivu binti huyu

Hao wanaume au hata wanawake hapo shida nini???? Hivi wanajua hayo yote ni sehemu tu na ishara kwamba mapenzi na mumewe yapo mujarrab???

Kuna mwanamke anayenyanyasika na kukumbuka kuringa na kudeka?????? hongera kwa mumewe kwa kujua kazi yake na wanatakiwa wajifunze kutoka kwa huyo jamaa
 

Right on the money homeboy. The good thing about it is, 9 times out of 10 people's hallucinations and opinions about other people whom they don't even know is not reality.
 
Watu wengine bana.......kama huwezi kuchangia bora kukaa kimya.......hoja ni maana na tofauti kati ya kudeka na kuringa......watu wanajadili mfano uliotumika

If that is the case;

Kudeka; Kuhitaji kufanyiwa mambo (mind human limits please) ambayo hata wewe mwenyewe kwa uwezo wako unaweza kufanya
Kuringa;Kujikubali na kujiona wewe ni bora na hii si lazima kujilinganisha na wengine as hapo huzaa kitu inaitwa madhereu
 
Kwa hiyo mapenzi yaweza kuleta kudeaka au maringo?........Au vyote

Kwa kweli sijui.

Ila ninachojua, mimi binafsi napendelea zaidi kupendwa hususan na ndugu wa karibu (baba, mama, watoto) kuliko kuchukiwa.

Sasa wengine wakiona mtu anapendwa wanahitimisha eti anadekezwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…