Hoja ya Mh. Mbatia ilikuwa imesimama hasa ukizingatia hali mbaya ya elimu inayolikabili taifa letu.
Mh. Mbatia alitaka iundwe tume ya Bunge kuchunguza sababu za kuanguka kwa elimu nchini na kutoa maelekezo kwa serikali ya hatua za kuchukua kunusuru hali hiyo.
Hata hivyo, kama ilivyo kawaida yake, Spika mara nyingi huegemea upande wa serikali, ...hoja hiyo haikupita.
Kuna madudu mengi sana katika sekta ya elimu, ila kwa mfumo huu wa Bunge letu ambalo linasimamiwa na serikali badala ya kuisimamia serikali, ...hatufiki popote !