Uchaguzi 2020 Kuelekea 25/08/2020: Mbona CHADEMA mmeanza kuhangaika sana?

Uchaguzi 2020 Kuelekea 25/08/2020: Mbona CHADEMA mmeanza kuhangaika sana?

Mr Tyang

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2018
Posts
1,728
Reaction score
6,806
Kwenu Viongozi na wanabodi;

Bila kupoteza Muda naomba niende kwenye mada moja kwa moja; Leo nimekuwa nikijipa Muda wa kuchungulia kinachoendelea huku mitandaoni hasa JF na Twitter lakini Cha kushangaza nikuwa post nyingi nilizozipitia zimejaa hofu kubwa juu ya zoezi la kuwapata Wagombea urais wa JMT.

Hasa upande wa CHADEMA, baadhi ya Viongozi na wadau wa Chama hicho wamepost posts za hofu sana wakitahadhalisha Mgombea wao asienguliwe kwa Namna yeyote Ile, wengine wakaenda mbali zaidi kwa kusema kesho(25/08/2020) Dunia nzima itakuwa inatazama kinachoenda kutokea.

Je, hofu na wasiwasi huu uliotawala CDM Tatizo Ni Nini? Mgombea wa Chama hicho Hana vigezo kwa mjibu wa Sheria na taratibu za NEC?

Je, ni mbinu za kisiasa ili kuipa hofu NEC katika kufanya maamuzi yake sahihi kisheria na kitaratibu?.

Je kuanza kujiona umefeli angali matokeo hayajatoka Wala kusahihishwa nisawa?

Je, ikitokea NEC wamemupitisha huyo wanaezani hapiti Watakuja kuongea Nini tena au ndo wataivua nguo Tena NEC kuwa kusema bila wao NEC wasingempitisha?

Na je asipopitishwa kisheria Watachukua hatua gani?

Je, fomu za ugombea urais wamechukua Chama kimoja tu? Maana sioni Viongozi Wala wadau wa vyama vingine wakipost Wala kuwa na hofu juu ya mchakato wa kuwapata Wagombea urais wa JMT Hapo kesho isipokuwa CDM tu.

Ushauri Wangu; Naishauri NEC ifanye maamuzi yake yaliyo kwenye msitari wa Sheria na haki pasipo kuyumbishwa na mtu,Chama Wala kitu chochote kile. Pia Wagombea naomba Kama ukienguliwa kisheria Basi tafuta haki yako kisheria, siyo ukatwe kisheria halafu utafute haki yako kwa Nguvu Tena ya kuwatumia wenzio hizo siyo Akili za kiongozi aliye Bora.

Kila la heri kuelekea tukio kubwa la kuwapata Wagombea urais wa JMT 2020 pia tusisahau kuwa palipo na ushindani lazima Kuna kushindwa na kushinda.
 
Naomba watu wenye akili timamu wakupuuze, UPUUZWE TU.
Mkuu umesoma Hadi level gani?
Ulishawahi hata kutembelea nchi jirani ya Kongo na kuongea mawili matatu na wakongo?

Kama jibu Ni ndio Basi utakuwa unasumbuliwa na mihemuko za kisiasa Ila ukweli unaujua.

Kama jibu Ni hapana, Basi usitake kupuuza kujadili juu ya kinachoenda kutokea kesho kwa maana ndo kinaweza amua amani mpya ya Tanzania.

Mwisho; nafikiri huna uelewa zaidi juu ya kitu kinaitwa "Fundamental sources of political instability"
 
Mkuu umesoma Hadi level gani?

Ulishawahi hata kutembelea nchi jirani ya Kongo na kuongea mawili matatu na wakongo?....
Usiniletee civics ya form 3 sijui form 4.

Narudia kusema kuwa UNAPASWA KUPUUZWA.
 
Juzi nimetoka malaba Uganda na roli kupeleka mchele kutoka Mwanza. Mtaa mzima wanaambiana kunamgeni kaja kutoka Tanzania.mimi sina ili wala lile wakawa wanapishana kujakuniuliza kuhusu Magufuli maswali meengi mengi sana.

Wanakwambia Museven atoke wampe Bob Wine aongoze Uganda kama anavyoongoza Rais Magufuli Tanzania.
 
Niko pamoja nawe Mkuu,
Pia tuwakumbushe wanasiasa kuheshimu maamuzi ya NEC endapo yatakuwa ya haki kisheria.

NEC ipi inayoamuwa maamuzi ya haki hapo wagombea lazima kupigania haki yao hakuna NEC ya kutoa haki mbona kwenye majimbo huku ni vurugu tu na hiyo NEC haisemi chochote. Wapambane hadi mwisho kitaeleweka tu
 
This time tuamue kula mbivu au mbichi. CCM pumzi imeisha
 
Juzi nimetoka malaba Uganda na roli kupeleka mchele kutoka Mwanza. Mtaa mzima wanaambiana kunamgeni kaja kutoka Tanzania.mimi sina ili wala lile wakawa wanapishana kujakuniuliza kuhusu Magufuli maswali meengi mengi sana.

Wanakwambia Museven atoke wampe Bob Wine aongoze Uganda kama anavyoongoza Rais Magufuli Tanzania.
Wakati huku kwetu kuna watu wanataka Magufuli atoke wampe kichaa atuongozee nchi.
 
Sasa kwanini usimwambie akaongoze huko Uganda anakohitajika kuna ubaya gani kama wanamuhitaji
Kuna ubaya mkuu, Kyaguranyi a.k.a Bobi ni raia wa Uganda, Pombe ni raia wa hapa hapa, sasa sijui kama umepitia vipengele vinavyomhusu mgombea uraisi katika nchi husika kikatiba ama ni hangover.
 
Siku moja nilikuwa naangalia mashindano haya hapa chini ambapo yule jamaa wa Kenya alianza kwa kasi sana na kuonekana kuwa amewaacha wenzake mbali sana na akadhani ameshashinda. Angalia matokeo yalivyokuwa

 
NEC ipi inayoamuwa maamuzi ya haki hapo wagombea lazima kupigania haki yao hakuna NEC ya kutoa haki mbona kwenye majimbo huku ni vurugu tu na hiyo NEC haisemi chochote. Wapambane hadi mwisho kitaeleweka tu
Nafikiri tusubiri maamuzi ya leo Hapo baadae ndo yatatosha kuijaji NEC Kama ipo kutenda haki au blaablaa.
 
Back
Top Bottom