Kuelekea AFL Tujipange kuepuka aibu ndogo ndogo

MTAZAMO

JF-Expert Member
Joined
Feb 8, 2011
Posts
19,675
Reaction score
33,583
Wakuu,

Ufunguzi wa michuano mikubwa zaidi barani Afrika inafanyika ijumaa hapa kwenye ardhi yetu. Kama kawaida yetu tunaweza kuchukulia rahisi sana fursa hii na tusijiandae kwenye mambo ya msingi kabisa. Hapa naweka dondoo chache za kuwa makini nazo

1) Mashabiki wataokuwa uwanjani

Tuwe wastarabu na miundombinu ya uwanja. Kila mmoja awe mlinzi wa mwenzake! Kutakuwa na wageni wengi ni aibu kukuta vyoo vina hali mbaya sababu ya kukosa ustaarabu.

2) Ushangiliaji wa wapenda soka

Tusianze uswahili wa kuzomea wachezaji wetu pale tumefungwa au anaingia mchezaji msiompenda. Kila mchezaji atayepewa nafasi tumpe hamasa sio vitimbwi na zomeazomea.

Pia si lazima tushangilie kama Mashabiki wa EPL, Tunaweza kushangilia kwa styles zetu na kucheza kivyetu kama singeli n.k

3) Vyombo vya usalama

Hapa sasa ndio muhimu zaidi. Wapewe seminar namna ya ku handle Mashabiki sio kupiga virungu huku International media zina rekodi itakuwa aibu.

Askari wetu wavae uniform za kupendeza wawe smart na zana zao. Askari waelekezwe namna ya ku behave dunia isitushangae.

4) Utaratibu wa kuingia uwanjani

Uwekwe utaratibu mzuri wa kistaarabu na mageti yafunguliwe mapema. Ni aibu pia watu wenye tiketi kushindwa kuingia. Kuwe na udhibiti mkali wa tiketi feki.

5) Ulinzi nje ya uwanja

Vyombo vya usalama viimarishe ulinzi eneo lote kuzunguka uwanja. Hizi siku vibaka hawana rangi, unaweza kupigwa roba na mtu kavaa reflector kama mmoja ya wahusika wa ulinzi shirikishi.

Mwisho, hili ni tukio kubwa na la kihistoria, tuepuke aibu ndogo ndogo kwa kukosa tu ustaarabu. Tutatia aibu zaidi ikitokea hilafu za umeme kama kawaida yetu. Tuipe heshima taifa letu alafu Simba SC wamalize na ushindi kunogesha zaidi.

Kila lakheri Mnyama, Lunyasi!
 
Umeandika kitu Cha maana Mno mkuu.

Hii ndio Michango tunayo itaka.

N B
MIKOMBATI YA POLISI NA MIMBWA HAITAKIWI KUONEKANA UWANJANI.
(kunatakiwa stewards WA uwanja sio migwanda ya POLISI)
Bravo

MTAZAMO
 
No.3 ni muhimu Sana. Polisi wa Tanzania hawana weledi katika kudeal na mikusanyiko. Hawawezi kumuelekeza Mtu badala ya kumfokea, kumkaripia au kumpiga. Matumizi ya nguvu ni Makubwa mno badala ya akili. Usishangae mabomu ya machozi yakapigwa kutawanya watu wakati wakijipanga mapema wakafika kabla ya mashabiki wataweza kudhibiti Kila kitu. Unakuta mashabiki wamefika uwanjani saa 4 asubuhi, Polisi wanafika saa 7 mchana ndo wanaanza kurudisha watu nyuma matokeo yake wanakanyagana kama Mechi ya Yanga mwaka Jana. Ushahidi ni kwenye mikutano ya kisiasa, Polisi wanakwenda kwenye mkutano saa moja kabla ya mgeni rasmi kufika wanaanza kusukuma watu. Mgeni akifika ndo unawaona wanahangaika kutafuta njia apite wapi apande jukwaani.
 
Umeandika kitu Cha maana Mno mkuu.

Hii ndio Michango tunayo itaka.

N B
MIKOMBATI YA POLISI NA MIMBWA HAITAKIWI KUONEKANA UWANJANI.
(kunatakiwa stewards WA uwanja sio migwanda ya POLISI)
Bravo

MTAZAMO
Tukikaa vibaya tutajikuta tumegeuka mjadala kwenye International platforms. Polisi wetu waelimishwe vizuri sana. Nguvu kidogo akili mingi.
 
Ng'ombe hanenepi siku ya mnada, tuna jamii ambayo ni kama mnyama aitwae nyumbu anayefuata mkumbo ambaye huaahirisha kufikiri kwa nafsi anapo amua kuifuata njia ya safari yake muda wake ukiwadia , jamii ambayo inatokana na kutelekezwa na mama Tanzania. Taifa linakosa muunganiko fulani hivi ambapo kila mtu anafanikiwa kutokana na juhudi zake binafsi siyo kwa mfumo wa kitaifa
 
Angalizo la umeme ndio la kuzingatia, mengine tuyaache.
 
Aibu kubwa itakuwa ni kupigwa goli zaidi ya 5


Mfungwe chache itasaidia hata kuzugia hapa mjini

Mwenye nguvu ashinde
 
Simba.... Simba.. mjipange,mcheze kama Simba wale wa zamani.Mkicheza hovyo,hakika mtapigwa mvua ya magoli na mtatuona mashabiki wa Yanga kama hatuna adabu na staha baada ya matokeo mabovu.Nawaombea muanze,muendelee na mumalize vyema.Kila la heri.
 
Vyote watu watafuata tanesko Sasa!,ngojeni mje muone muujiza..๐Ÿ˜‚
 
fainali ya yanga ilitia aibu mageti kucheleww kufunguliwa. Nafikiri mamlaka zimejifunza
 
MICHUANO MIKUBWA ZAIDI AFRIKA KWA NGAZI YA KLABU NI KLABU BINGWA AFRIKA TU.
 
Mm naomba tu umeme ukatike wakat WA ufunguzi jenereta nalo liwe na hitilafu๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†๐Ÿ˜† simu ziite
 
NILITEGEMEA Huu Uzi Uwe juu front

Ila Jamii Forum ya Leo!!!!!

Inaumiza sana lakini.....

Anyway

Active
 
Ustaarabu ni muhimu,ushauri mzuri sana.
Kuna mashabiki wanatabia za ajabu mpaka wanakojoa๐Ÿ‘‡ jukwaani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ