Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Kuelekea mchezo wa VPL ambapo Watani wa Jadi Tanzania (Kariakoo Derby) Simba SC dhidi ya Yanga SC mchezo ambao utapigwa Jumamosi ya July 3, 2021. Klabu ya Simba imeliomba Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF kuwa, kama kuna uwezekano wapelekewe kombe lao la VPL katika Uwanja wa Benjamin Mkapa siku ya mchezo.
Akizungumza na Waandishi wa Habari leo, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo Haji Manara amesema, wano wanaamini kuwa tayari ni Mabingwa wa VPL, kutokana na kuwaacha mbali watani wao kwa Alama na Mbao ya kufunga.
Ni mara chache kukutana na mazingira ambayo mmoja akishinda anachukua ubingwa, sikumbuki kama iliwahi kutokea labda mwaka 1985 ambapo Simba akishinda anachukua ubingwa na Yanga akishinda anachukua ubingwa.
Mechi ya Jumamosi ukiangalia hesabu wenzatu wakipata sare wanakuwa na ukomo wa alama 74 ambazo sisi tutakuwa nazo, Simba ili ikose ubingwa afungwe mechi zote 4 na Yanga washinde zote 2 tena na mabao ya kufunga yasiopungua 29, kitu ambapo katika hesabu za kawaida haiwezekani.
Kimsingi kombe la ubingwa lipo mikononi wa Simba, matarajio yetu ni kushinda mchezo wa Jumamosi na kutangazwa Mabingwa wa Nchi ili kuwapa furaha Wanasimba.
Akizungumza na Waandishi wa Habari leo, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo Haji Manara amesema, wano wanaamini kuwa tayari ni Mabingwa wa VPL, kutokana na kuwaacha mbali watani wao kwa Alama na Mbao ya kufunga.
Ni mara chache kukutana na mazingira ambayo mmoja akishinda anachukua ubingwa, sikumbuki kama iliwahi kutokea labda mwaka 1985 ambapo Simba akishinda anachukua ubingwa na Yanga akishinda anachukua ubingwa.
Mechi ya Jumamosi ukiangalia hesabu wenzatu wakipata sare wanakuwa na ukomo wa alama 74 ambazo sisi tutakuwa nazo, Simba ili ikose ubingwa afungwe mechi zote 4 na Yanga washinde zote 2 tena na mabao ya kufunga yasiopungua 29, kitu ambapo katika hesabu za kawaida haiwezekani.
Kimsingi kombe la ubingwa lipo mikononi wa Simba, matarajio yetu ni kushinda mchezo wa Jumamosi na kutangazwa Mabingwa wa Nchi ili kuwapa furaha Wanasimba.