Kuelekea laini za simu zisizosajiliwa kuzimwa; Ushauri wa namna bora ya kufanya ili kutovunja sheria za nchi

Mimi ndio kwanza nina mpango wa kwenda kwa mtendaji jmosi ijayo then j3 ndio niende ofisi za nida kuanza michakato.. nikikuta foleni kubwa itabidi nipotezee hadi foleni itakapoisha..

Kama kufungiwa line nimeshafungua moyo kitambo sana
 
ukienda airtel wanakwambia netwok ipo down njoo kesho... ukifika kesho wanakwambia ipo pending njoo kesho
aliyetoa siku 20 haja calculate haya ya njoo kesho sijui mtandao uansumbua. dah mashaka haya mpaka lini sijui
 
[emoji15][emoji15][emoji15][emoji848][emoji848][emoji848]
Jr[emoji769]
 
Kuthibitisha kama laini yako ya simu imesajiliwa kwa alama za vidole piga *106# chagua 1


Kwanza niwape pole wale wote ambao wanashinda ofisi za NIDA bila kufanikiwa.

Ukweli process ya vitambulisho ni ndefu sana.

Kwa wale ambao hawana vitambulisho vya NIDA unaweza tafuta ndugu yako ukasajili kwa kutumia kitambulisho chake, kitambulisho kimoja kinaruhusiwa kusajili laini 10.

Kwa wale ambao hawajasajili hakikisha fedha zote umezitoa na kama umezoea kutumia mobile banking hakikisha kadi yako ya ATM ipo valid otherwise utapata usumbusu mkubwa sana kupanga foleni bank na kupata ATM mpya inachukua more than one week.

Kwa NIDA nashauri watume majina na namba za wananchi ambao wameshajaza form na hawajapata namba zao ili mitandao ya simu (MNO) wasiwafungie kwa sababu hawana hatia.

Nawatakia weekend njema.

------
Waziri Nditiye asema hekima itatumika usajili wa laini kwa wasio na vitambulisho vya Taifa


Serikali ya Tanzania imesema itatumia hekima kuwasaidia wananchi walioshindwa kusajili laini za simu kwa sababu ya kukosa kitambulisho cha Taifa na namba licha ya kuanza mchakato wa kupata kitambulisho hicho.

Imesema wananchi hao taarifa zao zipo katika Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), huenda wamekosa kitambulisho au namba kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao.

Hayo yameelezwa leo Jumapili Januari 19, 2020 na naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye katika mkutano wa ndani wa CCM mkoani Kigoma.

"Serikali itaona jinsi ya kutumia hekima kwa wananchi ambao taarifa zao zipo katika ofisi za Nida kuona namna ya kufanya lakini kwa wengine ambao hawajajaza fomu laini zao zitazimwa,” amesema Nditiye.

Amesema ambao laini zao zitazimwa ni wale waliosajili laini chache na kuacha nyingine licha ya kuwa na kitambulisho hicho.

Amebainisha kuwa usajili wa laini za simu ni endelevu licha ya baadhi ya wananchi kupuuza.

Chanzo: Mwananchi

 
Naona mnadanganyana hahahaha mlikuwa wapi siku zote? NIDA kuna shida lakini watanzania tuna shida zaidi,,,,, kuna namba nyingi sana zimeshatoka lakini hadi leo hazijasajiliwa ,,,,,,,,
Hata pale mwananchi anaponyanyaswa na serikali yake bila hatia kazi yako ww nikujikomba kwa jiwe ili upate mlo!
Nani kalalamika hapa kwamba ana namba ya NIDA na ameshindwa kusajiri?

Hata hivyo, wakati wewe unasifu na kuabudu watawala walio kosa hekima, ukidhani mnawakomoa wapinzani,
ndg zako huko kijijini wanasota na NIDA na hawajafanikiwa kupata hata namba na ni miongoni mwa watakaofungiwa line zao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nina line 2. Moja nimesajili kwa kitambulisho cha jamaa (ili nijihadhari na kutokuwepo kwenye mawasiliano)... Nyingine (ya kwangu ya siku zote) sijasajili. Hii ya kwangu ikifungiwa haina shida coz watu wangu hawatonikosa hewani kwa hii nyingine na JF nitaendelea kuenjoy πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€

HIVI NDIVYO NILIVYOJIANDAA KISAIKOLOJIA.
 
Ahahahah.
Mpaka najiona wa ajab.Maana sina hata was was na wakat hata namba ya NIDA sina!!!!
Naona normal tu na tarehe 20 mdio hii.

Acha wanifungie nadhan ndio akil itanikaa sawa sawa.
Ahahahahah
 
Bonge la point...pia tutajipunguzia usumbufu wa matangazo yao kwa njia ya sms
 
Huo muda unao.
Sisi waajiliwa tusio na off na tunaingia asubuhi kutoka usiku ndo wenye kimbembe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa jamaa wana nongwa sana,nikidhamilia kutosajiri line,juzi nataka niwakope songesha wananigomea mpaka nikamilishe,nikaona duh hii sasa balaaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ahahahahahahahah.
Mkuu umenifungua macho.ndio maana songesha wananikomalia kila saa wanatuma sms ya deni lao.Kumbe wanapiga hesab kuwa tar 20 ishafika wanaona watanikosa!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…