Kuelekea mechi ya 'VPL' Kagera Sugar dhidi ya Simba SC, Wamezoea Lakini Leo Tunao!

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Kuelekea patashika ya ligi kuu Tanzania, Vodacom Premier League (VPL), nyasi za Uwanja wa Kaitaba Stadium, mkoani Kagera kuwaka moto ambapo leo September 26, 2019 Kagera Sugar, Wana Nkurukumbi, wanawakabili vilivyo Mabingwa wa Nchi Simba SC, Mnyama Mkali Mwituni, kutoka jijini Dar es salaam.

Mchezo huu kati ya Kagera Sugar na Simba SC, una vuta hisia za wapenda kandanda kote nchini, hivyo basi unatarajiwa kuwa mkali na wenye kusisimua kwa muda wote wa dakika tisini, kutokana na rekodi za timu hizi mbili hivi karibuni zinapokutana.

Kocha Patrick Aussems, amesema safari hii hawachomokei na amedhamiria kuondoka na alama tatu muhimu, huku akiongeza kuwa;

"Yaliyotokea msimu uliopita ni hamasa kwa wachezaji kufanya vizuri kuelekea mchezo huu, na nimeshawaambia kwamba lazima tuwaonyeshe kuwa sisi ni Simba SC". alisema Kocha Aussems.

•••Usikose Ukaambiwa, kuhusu burudani ya kandanda itakayovurumishwa kwenye dimba la Kaitaba Stadium. Kumbuka kipute hiki ni kuanzia saa 10:00 jioni.

•••Wamezoea Lakini Leo Hii Tunao
 
Kila la heri Mnyama Mkali Mwituni..Bingwa ni Bingwa hata kama yupo likizo..!
 
Taarifa;

Simba SC, itaendelea kumkosa nahodha wake John Bocco kwenye mchezo huu, baada ya kupatiwa muda wa mapumziko ili arudi katika hali yake ya kawaida..! Pamoja Clatous Chama kutokana na kuwa majeruhi.

NguvuMoja
 
Simba SC, upande wa washambuliaji, inatarajiwa kuongozwa na MK 14, Maddie Kagere na Wilker Henrique da Silva..!

SimbaNguvuMoja
 
Hakuna njia nyingine ya kutazama hii mechi zaidi ya Azam App?
 
Pole mikia..mnaanikiza vimechi vya mchangani...AS Kagera sugar wako vizuri mechi tatu wameshinda mfululizo na babu Nyoso ndani Kagere na Mbrazil wavalisheni pampas...
 
07' Upande wa kushoto sasa kwake Miraji anacontrol na kupenyeza mpenyezo hatari, anauwahi Wilker da Silvaaaaaa Oooooooooyes..!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…