Uchaguzi 2020 Kuelekea Oktoba 28, yahitajika busara zaidi sasa

Uchaguzi 2020 Kuelekea Oktoba 28, yahitajika busara zaidi sasa

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Mabibi na mabwana heshima kwenu na moja kwa moja kwenye mada.

Ni wazi kuwa kama nchi hapa tulipo tukielekea Oct. 28 hatuko vizuri. Kwamba tunawagombea ambao wamejizatiti vilivyo kutokukubali kushindwa? Hili si jambo la afya hata kidogo.

Kwamba kuna mazingira ya kuwekeana vikwazo labda kutumia hata tume ya uchaguzi kuengua baadhi ya wagombea mezani kabla ya kufika kwa wananchi kuliko na nguvu ya sanduku la kura? Hili nalo si la afya kidogo.

Kwamba kuna mikakati labda ya kutumia hata mahakama kwa mgongo wa uhuru wake na au labda eti kufuata mkondo wa sheria? Hili nalo wala si la afya tena.

Kwamba pamejitokeza matumizi ya nguvu dhidi ya watu walioko katika shamrashamra zao zisizokuwa na athari na mtu yeyote kutoka kwa wengine au mamlaka? Ni wazi kuwa kama nchi tunaelekea kubaya.

Katika hali ya dharura sana, haya ni mambo ya kulaaniwa vilivyo na kila mpenda haki na mwenye kuipenda nchi hii. Mfano dhahiri wa ya kulaaniwa ni haya ya uvunjifu wa amani yaliyotokea Arusha, Hai, Ruangwa nk na hata Mbeya. Wasiotutakia mema wanapaswa kufahamishwa bayana hivyo.

Mazingira wanayotaka kuyajenga kuwa hawatakuwa tayari kukubali kushindwa ni mambo ya kukemewa sasa kabla hatujachelewa kabisa.

Tunakwenda kwenye uchaguzi tukiwa na watia nia walio huru na sawa. Hakuna aliye na haki zaidi kuliko mwingine. Hakuna aliye mtanzania zaidi kuliko mwingine wala mwenye uzalendo zaidi kuliko mwingine. Uchaguzi si ugomvi.

Hatunaye leo Mzee Nyerere (rip). Hayupo Mzee Mkapa (rip). Busara zao zilihitajika mno sasa labda kuliko wakati mwingine wowote.

Mungu si Athumani mpo Mzee Kikwette na Mzee Mwinyi. Ni muda muafaka sasa labda zaidi sana kwa mzee Kikwette kutokulinyima taifa hili hazina ya busara zake.

Ni muhimu sana kwa Mzee Kikwette katika hali ya sasa akahusishwa moja kwa moja katika kuweka mazingira mazuri ya kufahamiana. Mustakabala na ujenzi wa salama katika nchi yetu hauwezi kuwa mikononi mwa "wawamba ngozi au ngoma" peke yao.

Uchaguzi si uadui. Uongozi ni wa Watanzania si wa mtu binafsi wala chama binafsi.

Yasemekana tayari tumekwisha poteza mtu mmoja. Hebu na asipotee wala kuumizwa mwingine kwa sababu ya uchaguzi tu.

Matumizi yoyote ya nguvu, janja janja, laghai, hila, husuda na vyote vya namna hiyo tokea kokote visipewe nafasi.

Polisi, mahakama, tume ya uchaguzi na msajili wa vyama vya siasa wajikite kwenye majukumu yao yaliyo ya msingi zaidi. Hebu wasiwabughudhi au kutumika kuwabugudhi wanasiasa au watia nia. Tuipe nafasi busara kutawala kuliko mabavu.

Hatukujifunza bado tokea katika matukio mengi mema tu yaliyo kwenda kinyume na matakwa ya maadui zetu?

Muda wa kuiponya nchi yetu ni sasa

Tulipo tunahitaji busara zaidi kuliko vinginevyo. Kwa kiswahili fasaha tuseme, "anahitajika zaidi sasa mwenye kuweza kumfunga paka kengele."

Wito: Huu ni muda muafaka wa maongezi. Kumhusisha rais mstaafu Mzee Kikwette sasa, angalipo lingekuwa jambo la heri sana.

Busara za mzee huyu zisizokuwa na upendeleo wowote zisikilizwe na pande zote. Tanzania ni kuu mno kuliko mtu au chama chochote:

Wito: Chonde chonde, Tanzania ni zaidi mno ya yeyote

Nawasilisha.
 
Anayesababisha yote Haya ni tume mbovu na polis wasiotambua wajibu wao....

Hatujachelewa kabisa kabisa. It's not over yet. Kunahitajika busara zaidi sasa.

Waungwana wote bila kujali vyama: viongozi wa dini, asasi za kiraia na wapenda haki wote muda wa kuwasiliana kwa mazungumzo na Mzee Kikwette ni sasa.

Kwa hakika muda wa mazungumzo kwa ajili ya kufahamiana ni huu. Vinginevyo tupo njiani uelekeo "Pagak."
 
Tarehe 28.08.2020 Tume ya Uchaguzi itayafuta majina ya wagombea urais wafuatao.
1. Tundu Lissu
2. Bernard Membe
3. maalim Seif
Kwa kisingizio kwamba hawana sifa

Wasifanye hivyo. Tusiwaruhusu kufanya hivyo.

Hatutawaruhusu kufanya hivyo.

Busara isipotumika tunaelekea kubaya. Tunaelekea kwenye kuandika historia mbaya kwa taifa hili ambayo haitafutika daima.

Historia itakuwapo kwa ajili ya hukumu ya haki.

Kwetu sote: "Asiyekubali kushindwa si mshindani"
 
brazaj unategemea Mzee Mwinyi atasema nini wakati mwanae yuko kwenye mchakato wa kukabidhiwa kisiwa!

Mkuu Sky Eclat ni kwa kutambua hilo na pia kuwa Mzee Mwinyi yu mtu mzima sana kwa sasa ndiyo maana:

1. Nikaandika kwenye mada kama ilivyo pale kwenye red:

"Mungu si Athumani mpo Mzee Kikwette na Mzee Mwinyi. Ni muda muafaka sasa labda zaidi sana kwa mzee Kikwette kutokulinyima taifa hili hazina ya busara zake."

2. Pia kusisitiza kutowaachia "wawamba ngoma na wawamba ngozi." Maana hao watavutia kwao.

3. Pia kuweka msisitizo zaidi kwa Kikwette na bila kuacha kukumbushia:

"Busara za mzee huyu zisizokuwa na upendeleo wowote zisikilizwe na pande zote."

Kwamba pana watu wana maslahi binafsi na fukuto hili? Hilo mbona ni wazi mno?

Ndiyo maana hata kwa bandiko hili tu wawamba ngozi hao hata wa humu JF, wapo waliofura vilivyo kwa hasira kuliko vifutu.

Wachawi wakubwa!
 
Mkuu Sky Eclat ni kwa kutambua hilo na pia kuwa Mzee Mwinyi yu mtu mzima sana kwa sasa ndiyo maana:

1. Nikaandika kwenye mada kama ilivyo pale kwenye red:

"Mungu si Athumani mpo Mzee Kikwette na Mzee Mwinyi. Ni muda muafaka sasa labda zaidi sana kwa mzee Kikwette kutokulinyima taifa hili hazina ya busara zake."

2. Pia kusisitiza kutowaachia "wawamba ngoma na wawamba ngozi." Maana hao watavutia kwao.

3. Pia kuweka msisitizo zaidi kwa Kikwette na bila kuacha kukumbushia:

"Busara za mzee huyu zisizokuwa na upendeleo wowote zisikilizwe na pande zote."

Kwamba pana watu wana maslahi binafsi na fukuto hili? Hilo mbona ni wazi mno?

Ndiyo maana hata kwa bandiko hili tu wawamba ngozi hao hata wa humu JF, wapo waliofura vilivyo kwa hasira kuliko vifutu.

Wachawi wakubwa!

Eti kumbe

Mkuu wa Wilaya ya #Hai Lengai Ole #Sabaya ndiye Aliyeratibu Zoezi la Kuchoma Moto ofisi za Chadema Arusha Jana Usiku, Pia ndiye ameratibu Zoezi la kupiga Mawe msafara wa Lissu leo.

#Makamanda Najua Hamshindwi, Popote alipo aliwe kichwa.
1597462828972.png
 
Hawataki wimbo wa taifa, hawataki muungano.
Huo ni mwanzo wa kukosa sifa

Ndiyo sababu ya njama hizi za kuzuia watia nia hawa wasisikike wao wenyewe kwenye vyombo vyovyote vya habari kwa wanayoyasimamia?

Lengo likiwa ni kuwabana vilivyo ili wasisikike hivyo kufanikisha nia zao ovu za kuwawekea maneno mdomoni ili waweze kuwatia munda vilivyo?

Mbona hata Mungu anawaona?

"Kwa hakika mngekuwa na hekima mngejihoji wenyewe au muulize sababu za kutokubalika kwenu kuliko kupambana na nyota za wengine?"
 
Magufuli mbona mwingine anafaa lakini maagizo anayotoa kwa wasaidizi wake yana haribu Taswira yake.
 
Yaliyopangwa Kule Brussels Yanashtusha...

Huyu Arvinder Deepel,Marcus McManon na Mchoraji Mkuu Wa VIBARAKALA Wenye Nia Ya Kuendelea Kuikwiba Afrika Kwa Zama Hizi Bwana Mkubwa Johnson Stielenger Kazini Tena....

Wakubwa Hao Wametoa Mchango Sana Kwa Ndg.Yetu Kipindi Akiwa Kule......daaah Beberu Ni Mtu Mbaya Sana....

Ilianza kuletwa BARUA.....
Na Sasa Tunashuhudia Magaidi Na VIBARAKALA Wakitumiwa Kuwashambulia Wanachama Wasio na Makosa ili tu Serikali Ya CCM ichafuke mbele Ya Macho Ya Watanzania.....

Kule Msumbiji Kunaendelea Kufukuta....

Yaani Tanzania Pekee Ndipo Amani Ilipojichimbia....

Shtuka Ndugu Yangu,Usiwakubalie VIBARAKALA na Mabwana Zao KUTUCHOMEA NCHI YETU JAMALI...

Hatuna Pa Kukimbilia Sisi...
Twende Wapi Sisi......

Wanasiasa Wachumia Matumbo ni Wa kuwaogopa Zaidi Ya Ebola...

Mungu Atalipigania Taifa Letu Pendwa aaamin aaaaamin.
 
Yaliyopangwa Kule Brussels Yanashtusha...

Huyu Arvinder Deepel,Marcus McManon na Mchoraji Mkuu Wa VIBARAKALA Wenye Nia Ya Kuendelea Kuikwiba Afrika Kwa Zama Hizi Bwana Mkubwa Johnson Stielenger Kazini Tena....

Wakubwa Hao Wametoa Mchango Sana Kwa Ndg.Yetu Kipindi Akiwa Kule......daaah Beberu Ni Mtu Mbaya Sana....

Ilianza kuletwa BARUA.....
Na Sasa Tunashuhudia Magaidi Na VIBARAKALA Wakitumiwa Kuwashambulia Wanachama Wasio na Makosa ili tu Serikali Ya CCM ichafuke mbele Ya Macho Ya Watanzania.....

Kule Msumbiji Kunaendelea Kufukuta....

Yaani Tanzania Pekee Ndipo Amani Ilipojichimbia....

Shtuka Ndugu Yangu,Usiwakubalie VIBARAKALA na Mabwana Zao KUTUCHOMEA NCHI YETU JAMALI...

Hatuna Pa Kukimbilia Sisi...
Twende Wapi Sisi......

Wanasiasa Wachumia Matumbo ni Wa kuwaogopa Zaidi Ya Ebola...

Mungu Atalipigania Taifa Letu Pendwa aaamin aaaaamin.
Unaota?
 
Yaliyopangwa Kule Brussels Yanashtusha...

Huyu Arvinder Deepel,Marcus McManon na Mchoraji Mkuu Wa VIBARAKALA Wenye Nia Ya Kuendelea Kuikwiba Afrika Kwa Zama Hizi Bwana Mkubwa Johnson Stielenger Kazini Tena....

Wakubwa Hao Wametoa Mchango Sana Kwa Ndg.Yetu Kipindi Akiwa Kule......daaah Beberu Ni Mtu Mbaya Sana....

Ilianza kuletwa BARUA.....
Na Sasa Tunashuhudia Magaidi Na VIBARAKALA Wakitumiwa Kuwashambulia Wanachama Wasio na Makosa ili tu Serikali Ya CCM ichafuke mbele Ya Macho Ya Watanzania.....

Kule Msumbiji Kunaendelea Kufukuta....

Yaani Tanzania Pekee Ndipo Amani Ilipojichimbia....

Shtuka Ndugu Yangu,Usiwakubalie VIBARAKALA na Mabwana Zao KUTUCHOMEA NCHI YETU JAMALI...

Hatuna Pa Kukimbilia Sisi...
Twende Wapi Sisi......

Wanasiasa Wachumia Matumbo ni Wa kuwaogopa Zaidi Ya Ebola...

Mungu Atalipigania Taifa Letu Pendwa aaamin aaaaamin.
Yaani hata hueleweki unasimamia wapi, ndio maana mtoa mada kasema tuweke ushabiki pembeni tuliokoe Taifa
 
Eti kumbe

Mkuu wa Wilaya ya #Hai Lengai Ole #Sabaya ndiye Aliyeratibu Zoezi la Kuchoma Moto ofisi za Chadema Arusha Jana Usiku, Pia ndiye ameratibu Zoezi la kupiga Mawe msafara wa Lissu leo.

#Makamanda Najua Hamshindwi, Popote alipo aliwe kichwa.
View attachment 1537605
Kati ya watu hatari kabisa kwa amani ya Taiga hili, na ambao kama Rais atakosa namna ya kuwadhibiti wanaweza kuliletea Taifa hili matatizo makubwa, ni pamoja na:

1) Sabaya
2) Gambo
3) Makonda
4) Chalamila
5) Mambosasa

Rais akiendelea kuwachekea hawa, kuna siku atakuja kujutia. Hawa busara na hekima, haipo kabisa. Wanaendeshwa na mahaba na unafiki uliopindukia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom