Pre GE2025 Kuelekea uchaguzi mkuu ili kukabiliana na rushwa TAKUKURU Tumieni maafisa vipenyo na mawakala vicheche

Pre GE2025 Kuelekea uchaguzi mkuu ili kukabiliana na rushwa TAKUKURU Tumieni maafisa vipenyo na mawakala vicheche

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

TheForgotten Genious

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2014
Posts
2,087
Reaction score
3,156
90% chaguai nyingi zinagubikwa na rushwa kuanzia ndani ya vyama na nje ya vyama .

Wagombea wengi huwatumia viongozi katika serikali za mitaa ili kupenyeza rushwa zao kwenda kwa wananchi hili ninelifanyia utafiti kwa kuwahoji baadhi ya vijana na wakakiri kwamba huwa wanapewa around 15k kupitia wajumbe wa serikali za mitaa ambao wapo jiran na wananchi.

Lakini zipo rushwa nyingine kama rushwa ya ngono kwa wanasiasa wa kike ili wapewe teuzi za kugombea ndani ya vyama vyao.

TAKUKURU itumie maafisa vipenyo ndani ya taaaisi mbalimbali ambao ni wafanyakazi wa taasisi hizo,maafisa hawa wadumu hapo kama wafanyakazi wengine,kazi yao itakuwa ni kuchunguza kisirisiri masuala ya rushwa ndani ya taasisi nakupeleka ripoti kwa namna bora .

Mawakala vicheche watumike katika serikali za mitaa,kata nk maeneo mbali mbali,mawakala hawa wapatiwe mafunzo kuhusu namna spying inafanya,hapa watachukuliwa wale vijana ambao ni wajanja na wapo jirani na wajumbe kisha taarifa hizo watazituma kila asubuhi.
 
Back
Top Bottom