Kufahamu mambo yako hapa: Ramli ya kutizama mambo unayotaka

Aisee mm niwatahadharishe na huyu mtu
Mchawi huweza kukuroga haraka sana akijua jina lako na la mama ako mzazi tahadharini jamani huyu jamaa ataenda kuwatia mikosi maishani mwenu
Ushirikina haufai tena ni.dhambi kubwa mno
we jiulize kwanini utizamie jambo ambalo Mungu kalificha ww untka kuliona ili iweje na isitoshe ety unamuamini binadamu mwenzako ndo akufanyie ivo

Mimi nawatahadharisha na huyu mtu sio mtu mzuri.ata kidogo
 
Mkuu naomba kujua hii ya maradhi yasiyo pona kwa mwene nyota ya masuke
Nyota ya mashuke ni nyota ambayo inatawala mlango wa sita asili ikiwa mashuke anatawala mlango wa maradhi basi anatakiwa kuchagua moja either kusaidia watu katika kutibu au yeye kuwa muhanga wa kutibiwa maradhi ya mara kwa mara
 
Hongera mkuu. au wewe ndio unahofu wanaweza kusaidika na yale ambayo vyama vyenu vimekuwa vikiyafanya?
 

Kum 18:10-12​

Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri, wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu. Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa BWANA; kisha ni kwa sababu ya hayo BWANA, Mungu wako, anawafukuza mbele yako.
 
“Makuhani Walawi, naam, kabila lote la Lawi, halitakuwa na fungu au urithi pamoja na Waisraeli. Watakula dhabihu zinazochomwa kwa moto zinazotolewa kwa Yehova, ambazo ni urithi wake.+ 2 Kwa hiyo hawapaswi kuwa na urithi kati ya ndugu zao. Yehova ndiye urithi wao, kama alivyowaambia.

3 “Sasa hii ndiyo haki ambayo makuhani wanastahili kutoka kwa watu: Mtu yeyote anayetoa dhabihu, iwe ni ng’ombe dume au kondoo anapaswa kumpa kuhani mguu wa mbele, mataya, na tumbo. 4 Mnapaswa kumpa mazao ya kwanza ya nafaka yenu, divai yenu mpya, mafuta yenu, na manyoya ya kwanza yaliyokatwa ya kondoo wenu.+ 5 Yehova Mungu wenu amewachagua wao pamoja na wana wao kutoka kati ya makabila yenu yote ili wahudumu katika jina la Yehova daima.+

6 “Lakini ikiwa Mlawi ataondoka katika mojawapo ya majiji yenu katika Israeli alimokuwa akiishi,+ naye angependa kwenda mahali ambapo Yehova anachagua,*+ 7 anaweza kuhudumu huko katika jina la Yehova Mungu wake kama wanavyofanya ndugu zake wote, Walawi, wanaosimama huko mbele za Yehova.+ 8 Atapokea kiasi kilekile cha chakula pamoja nao,+ mbali na malipo anayopata baada ya kuuza mali za mababu zake.

9 “Mtakapoingia katika nchi ambayo Yehova Mungu wenu anawapa, msijifunze kuiga mazoea yenye kuchukiza ya mataifa hayo.+ 10 Asipatikane miongoni mwenu mtu yeyote anayemteketezahttps://wol.jw.org/sw/wol/fn/r13/lp-sw/1001061109/118 motoni+ mwanawe au binti yake, mtu yeyote anayefanya uaguzi,https://wol.jw.org/sw/wol/fn/r13/lp-sw/1001061109/119https://wol.jw.org/sw/wol/fn/r13/lp-sw/1001061109/119+ mtu yeyote anayefanya uchawi,+ mtu yeyote anayetafuta ishara za ubashiri,+ mlozi,+ 11 mtu yeyote anayewafunga wenzake kwa uchawi, mtu yeyote anayetafuta ushauri kutoka kwa watu wanaowasiliana na roho,+ mpiga ramli,+ au mtu yeyote anayetafuta habari kuhusu wafu.+ 12 Kwa maana mtu yeyote anayefanya mambo haya ni chukizo kwa Yehova, na kwa sababu ya mazoea haya yanayochukiza, Yehova Mungu wenu anayafukuza mataifa hayo kutoka mbele yenu. 13 Mnapaswa kudhihirisha kwamba hamna lawama mbele za Yehova Mungu wenu.+

14 “Kwa maana mataifa haya mnayomiliki nchi yao yalikuwa yakiwasikiliza wale waliozoea uchawi+ na uaguzi,https://wol.jw.org/sw/wol/fn/r13/lp-sw/1001061109/120+ lakini Yehova Mungu wenu hajawaruhusu mfanye jambo lolote kama hilo. 15 Yehova Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka kati ya ndugu zenu. Ni lazima mumsikilize.+ 16 Kwa sababu hilo ndilo mlilomwomba Yehova Mungu wenu kule Horebu katika siku ya kusanyiko,https://wol.jw.org/sw/wol/fn/r13/lp-sw/1001061109/121https://wol.jw.org/sw/wol/fn/r13/lp-sw/1001061109/121+ mliposema, ‘Usiache tusikie sauti ya Yehova Mungu wetu au kuona tena moto huu mkubwa, tusije tukafa.’+ 17 Kisha Yehova akaniambia, ‘Jambo walilosema ni sawa. 18 Nitawainulia nabii+ kama wewe kutoka kati ya ndugu zao, nami nitaweka maneno yangu katika kinywa chake,+ naye atawaambia mambo yote nitakayomwamuru.+ 19 Naam, nitamwadhibu kila mtu ambaye hatasikiliza maneno yangu ambayo nabii huyo atasema katika jina langu.+

20 “‘Ikiwa nabii yeyote atasema kwa kimbelembele katika jina langu neno ambalo sikumwamuru aseme au kusema katika jina la miungu mingine, nabii huyo lazima afe.+ 21 Lakini huenda mkasema hivi mioyoni mwenu: “Tutajuaje Yehova hajasema neno hilo?” 22 Nabii akisema neno katika jina la Yehova na neno hilo lisitimie au kufanyika, basi Yehova hakusema neno hilo. Nabii huyo alilisema kwa kimbelembele. Hampaswi kumwogopa.’

N.B:
Vitabu vya dini havisomwi kama mipasho wala hayatakikani hayo kwa Mungu na wala sio aya za kutumia kudidimiza mmoja kwa mwingine elewa maana nzima ya kifungu na usichukuw kinachokufaa na kuacha kingine ukiyavulia maji yaoge na ukishindwa usiyakaribie vile vile usinene usilolijua mwisho wake nena mwanzo wa jambo na mwisho wake na ujue kisha chake.

Rakims
 
Karibu Mkuu mention your name and your moms name,
names ipi ,maana mtu anweza kuwa na majina mengi tu alilopewa na baba,na mama,na shangazi,alilojipa mwenyewe ,alilopewa na watu na kila jina likawa linatumika kwenye mazingira fulani,hii sayansi ya kutumia jina sidhani kama ina effect maana jina ni identity tu mtu anaweza akamuita mwane cristiano ronaldo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…