Kufanana na kutofautiana kwa Majaji Tiganga na Siyani

Kufanana na kutofautiana kwa Majaji Tiganga na Siyani

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Wawili hawa ni majaji ambao wote wameshughulika na kesi inayomhusu Mh. Mbowe na wenzake.

Wote ni wateuliwa mahiri wa hayati Magufuli. Wote kwa maamuzi yao wameuacha ulimwengu wa haki ukiwa umepigwa butwaa.

Kwa hakika hawajaonekana hadharani wenye kuyafagilia kwa dhati yao, maamuzi yoyote ya wawili hawa.

Haijulikani kama wote watadumu na kesi hii hadi mwisho.

Wakati Siyani alikuwa ni mswalihina ustaadhi wa swala tano (tukipisha adhana muda ukitimu), japo yeye alizingatia muda. Kwake saa tatu yake ilikuwa saa tatu kweli. Baada ya dakika 10 yake ilikuwa kweli baada ya muda huo.

Tofauti na hapo, leo ya Tiganga inaweza kumaanisha kesho vile vile na bila hata ya neno la samahani. Akisema saa tatu ujue saa nne au hata saa tano. Kwake huyu saa au muda hauna maana.

Siyani mahakamani alikuwa na authority japo yenye kuashiria uwezekano wa haki kutendeka.

Hakukuwa na mzaha mzaha wa mashahidi kuthubutu hata kutupia au kupiga chabo. Sasa Tiganga.

Yote kwa yote wawili hawa kwenye kuuma na kupuliza au kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa - wako vizuri (au kama asemavyo beberu -- wake perfect)!
 
Hivi haiwezekani kuwa na sheria ya DPP awe na idara maalumu yakuchambua vielelezo vya mashahidi kabla yakumshitaki mtu.

Naona kama watetezi na waendesha mashitaka wanasababisha chuki kwenye jamii
 
Hivi haiwezekani kuwa na sheria ya DPP awe na idara maalumu yakuchambua vielelezo vya mashahidi kabla yakumshitaki mtu.

Naona kama watetezi na waendesha mashitaka wanasababisha chuki kwenye jamii

Kwenye katiba mpya hakutakiwi kufanyiwa ajizi.

Katiba inayowapa nafasi ya kujikwapulia mamlaka ya kumshikilia mtu kama wanavyotaka na bila kuwajibika kwa lolote ndiyo madhara yake haya.
 
Ndiyo kinachokuja

Huyu aliyepo wapi penye la maana? Ni proceedings? Ni kwenye muda? Ni kwenye hukumu?

Si Bora hata akumbuke japo adhana basi tujue anajua kuna na Mungu pia?
 
Hivi haiwezekani kuwa na sheria ya DPP awe na idara maalumu yakuchambua vielelezo vya mashahidi kabla yakumshitaki mtu.

Naona kama watetezi na waendesha mashitaka wanasababisha chuki kwenye jamii
Huyo DPP mwenyewe mnamuamin?
Tuanzie hapo
 
Alaaaaaaaa! Kumbe!

Kipi hukukijua mkuu?

1. "Wawili hawa ni majaji ambao wote wameshughulika na kesi inayomhusu Mh. Mbowe na wenzake."

2. "Wote ni wateuliwa mahiri wa hayati Magufuli."

3. "Wote kwa maamuzi yao wameuacha ulimwengu wa haki ukiwa umepigwa butwaa."

Au kuna niliposema uongo ndugu yangu?
 
Back
Top Bottom