SoC02 Kufanya kazi na vijana wa kitanzania walio feli kidato cha nne na wapo nyumnani bila kazi yeyote ili wakue kiuchumi na kuajiri vijana wengine

SoC02 Kufanya kazi na vijana wa kitanzania walio feli kidato cha nne na wapo nyumnani bila kazi yeyote ili wakue kiuchumi na kuajiri vijana wengine

Stories of Change - 2022 Competition

Kombac69

New Member
Joined
Aug 21, 2022
Posts
1
Reaction score
0
MOTTO: Kijana na mabadiliko ya uchumi.

LENGO: Kusaidia kukua kiuchumi vijana walio hitimu kidato cha nne na kufeli mitihani yao wakiwemo pia vijana wa makundi maalum na wapo nyumbani hawana vyanzo vya kujiingizia vipato na kuwabadilisha kiuchumi wale wasio na elimu kabisa.

DIRA: Kuhakikisha mabadiliko ya kiuchumi yanafanyika nchini kwa kuanza na vijana waliopata angalau elimu ya kidato cha nne wakiwemo pia wa makundi maalumu bila kujali jinsi na baadae wao kuwabadilisha kiuchumi pia wale ambao hawakupata elimu kabisa kwa kufanya nao kazi mbalimbali za kujipatia kipato na elimu ya kujitegemea.

Mimi naitwa Cosmas Flavian Komba, ni kijana wakiume, mtanzania na nina umri wa miaka 38. Elimu yangu ni stashahada ya elimu ya sekondari na ninaishi Galapo Babati Manyara.

Kama nilivyo onesha kwenye kichwa cha habari baada ya kuona vijana wengi wanapita na kuteseka na maisha, nipo tayari kujitolea kuibadilisha jamii kiuchumi kupitia ajira na elimu ya kujitegemea.

Nitaanza na vijana wanao nizunguka waliomaliza kidato cha nne na kutopata matokeo mazuri ambayo yaliwafanya wao kukosa sifa za kuendelea mbele kimasomo.

Nikiipata hiyo hela ya kiasi cha shilingi 5,000,000/= itakuwa kama mtaji ambao ntautumia kuwabadilisha vijana hao kiuchumi na waweze kujitegemea.

Ningependa weka wazi kitu ambacho ntafanya nao na kuwabadilisha na wao kuwabadilisha vijana wengine ambao hawakuweza pata elimu au walikatisha masomo yao kwasababu nyingi kama mimba za utotoni, madawa ya kulevya na umasikini.

Nitanunua Mashine ya kutotolesha vifaranga na nitaiweka kwenye eneo ambalo lipo tayari na linaumeme kabisa, kupitia mashine hiyo nitaanza na vijana 20 katika mradi huu, mradi unavyozidi kukua nitaongeza vijana wengine na hata wale ambao hawana elimu kabisa nitawapa elimu ya vitendo na kujitambua umuhimu wake kama vijana.

Ufuatao ni mchanganuo wa shilingi 5,000,000/= itakavyo tumika,

1,000,000 - Kununulia mashine ya kutotolesh vifaranga ya mayai 352 na usafiri wa kuileta Galapo babati Manyara.

2,200,000 - Kujengea Banda bora la mfano la kufugia hao kuku.

100,000 - Vifaa vya kulishia na kunyweshea.

100,000 - Tiba kwa vifaranga.
1,000,000 - Mavazi maalumu, buti na vifaa vingine vya kuvaa na dawa ili kujifunza vyema na kuepusha vimelea vya magonjwa kuwafikia kuku.

550,000 - Chakula cha kuku kuanzia wadogo hadi kufikia kuuzwa.
50,000 - Umeme.

Huu mchanganua ni mwanzo wa kuanza mradi wetu, baada ya kukua hao kuku mradi utajiendedha vyema kabisa wenyewe kwa kuuza mayai, vifaranga na kuku wakubwa, kutotolesha mayai kwa wafugaji wengine, kuuza mbolea itokanayo na kinyesi cha kuku, kuanzisha bustani za mbogamboga tutaongeza aina mbalimbali za mifugo kama kanga, sungura,kondoo,mbuzi na ng'ombe.

Pia tutakisajili na kutoa vyeti na kuhakikidha kutoa japo mashine chache za kutotolesha vifaranga kwa wahitimu kila mwaka ili wajiunge kimakundi na kujiajiri. Pia na kupokea wahitimu wapya na tutakuwa tunaongeza mashine za kutotolesha kuendana na ukubwa wa soko.

Mwisho napenda kushukuru kwa jambo hili mlilolitoa kwani kwenye jamii tunazoishi na zinazotuzunguka kuna ndoto nyingi zenye malengo chanya kabisa kwa vijana na hata watu wengine kama wazee na makundi maalumu, ila tatizo huwa ni mtaji.

Naimani mtalisoma andika langu, mtalifanyia kazi na linaweza shinda kabisa ili tusaidie vijana hawa kwani wanahitaji sana elimu ya kujitegemea katika safari yao ya kujikomboa katika umasikini, na kuelekea kwenye uchumi mzuri na kuwa na familia bora ambazo zitaleta vizazi bora kwa manufaa ya Taifa zima.

Asanteni sana, na naimani andiko langu litapitiwa vyema na kufanyiwa kazi.
Simu: 0689772886
 
Upvote 0
Sa
MOTTO: Kijana na mabadiliko ya uchumi.

LENGO: Kusaidia kukua kiuchumi vijana walio hitimu kidato cha nne na kufeli mitihani yao wakiwemo pia vijana wa makundi maalum na wapo nyumbani hawana vyanzo vya kujiingizia vipato na kuwabadilisha kiuchumi wale wasio na elimu kabisa.

DIRA: Kuhakikisha mabadiliko ya kiuchumi yanafanyika nchini kwa kuanza na vijana waliopata angalau elimu ya kidato cha nne wakiwemo pia wa makundi maalumu bila kujali jinsi na baadae wao kuwabadilisha kiuchumi pia wale ambao hawakupata elimu kabisa kwa kufanya nao kazi mbalimbali za kujipatia kipato na elimu ya kujitegemea.

Mimi naitwa Cosmas Flavian Komba, ni kijana wakiume, mtanzania na nina umri wa miaka 38. Elimu yangu ni stashahada ya elimu ya sekondari na ninaishi Galapo Babati Manyara.

Kama nilivyo onesha kwenye kichwa cha habari baada ya kuona vijana wengi wanapita na kuteseka na maisha, nipo tayari kujitolea kuibadilisha jamii kiuchumi kupitia ajira na elimu ya kujitegemea.

Nitaanza na vijana wanao nizunguka waliomaliza kidato cha nne na kutopata matokeo mazuri ambayo yaliwafanya wao kukosa sifa za kuendelea mbele kimasomo.

Nikiipata hiyo hela ya kiasi cha shilingi 5,000,000/= itakuwa kama mtaji ambao ntautumia kuwabadilisha vijana hao kiuchumi na waweze kujitegemea.

Ningependa weka wazi kitu ambacho ntafanya nao na kuwabadilisha na wao kuwabadilisha vijana wengine ambao hawakuweza pata elimu au walikatisha masomo yao kwasababu nyingi kama mimba za utotoni, madawa ya kulevya na umasikini.

Nitanunua Mashine ya kutotolesha vifaranga na nitaiweka kwenye eneo ambalo lipo tayari na linaumeme kabisa, kupitia mashine hiyo nitaanza na vijana 20 katika mradi huu, mradi unavyozidi kukua nitaongeza vijana wengine na hata wale ambao hawana elimu kabisa nitawapa elimu ya vitendo na kujitambua umuhimu wake kama vijana.

Ufuatao ni mchanganuo wa shilingi 5,000,000/= itakavyo tumika,

1,000,000 - Kununulia mashine ya kutotolesh vifaranga ya mayai 352 na usafiri wa kuileta Galapo babati Manyara.

2,200,000 - Kujengea Banda bora la mfano la kufugia hao kuku.

100,000 - Vifaa vya kulishia na kunyweshea.

100,000 - Tiba kwa vifaranga.
1,000,000 - Mavazi maalumu, buti na vifaa vingine vya kuvaa na dawa ili kujifunza vyema na kuepusha vimelea vya magonjwa kuwafikia kuku.

550,000 - Chakula cha kuku kuanzia wadogo hadi kufikia kuuzwa.
50,000 - Umeme.

Huu mchanganua ni mwanzo wa kuanza mradi wetu, baada ya kukua hao kuku mradi utajiendedha vyema kabisa wenyewe kwa kuuza mayai, vifaranga na kuku wakubwa, kutotolesha mayai kwa wafugaji wengine, kuuza mbolea itokanayo na kinyesi cha kuku, kuanzisha bustani za mbogamboga tutaongeza aina mbalimbali za mifugo kama kanga, sungura,kondoo,mbuzi na ng'ombe.

Pia tutakisajili na kutoa vyeti na kuhakikidha kutoa japo mashine chache za kutotolesha vifaranga kwa wahitimu kila mwaka ili wajiunge kimakundi na kujiajiri. Pia na kupokea wahitimu wapya na tutakuwa tunaongeza mashine za kutotolesha kuendana na ukubwa wa soko.

Mwisho napenda kushukuru kwa jambo hili mlilolitoa kwani kwenye jamii tunazoishi na zinazotuzunguka kuna ndoto nyingi zenye malengo chanya kabisa kwa vijana na hata watu wengine kama wazee na makundi maalumu, ila tatizo huwa ni mtaji.

Naimani mtalisoma andika langu, mtalifanyia kazi na linaweza shinda kabisa ili tusaidie vijana hawa kwani wanahitaji sana elimu ya kujitegemea katika safari yao ya kujikomboa katika umasikini, na kuelekea kwenye uchumi mzuri na kuwa na familia bora ambazo zitaleta vizazi bora kwa manufaa ya Taifa zima.

Asanteni sana, na naimani andiko langu litapitiwa vyema na kufanyiwa kazi.
Simu: 0689772886
safi mkuu lengo ni kuwainua waliofail au kuwainua vijana?
Maana kufail kwa mtu ni mchakato ambao kwa namna yeyote muhusika anapaswa atambue wapi alipokosea hasa kwa vijana wetu ambao wanamiliki simu ya laki 3,ambayo matumizi yake nisawa na angekuwa na cmu ya 25000 nikimaanisha cmu anayomiliki ni mtaji tosha wa kumsaidia kupiga hatuA ya kimabadiliko kwa kupata taarifa zenye kumsaidia na kupata elimu itakayo mfungua uelewa wake.
umasikini au utajiri wa kipato huanzia mbaali sana chini kabisa katika level ya familia na jamii inayokuzunguka,hivi unadhani Kama kijana tangu anazaliwa mpaka anaanza nae familia amezungukwa na huo umaskini unadhani huyu hata ukimwambia kunamaisha bora zaidi ya aliyokuwa nayo atakuelewa?no hatoweza Ila Kama atatoka hapo alipo akaenda mahali pengine akajionea tofauti ya maisha na akapata nia ya kujifanyia mabadiliko huyu ni rahisi kumsaidia na akasaidia wengine,
Sasa kwavile ni ngumu kuwatoa wote kuwapeleka sehemu ya kuona mwanga tofauti,Mimi ningeshauri pamoja na matarajio yako,hebu rudi chini kidgo anza na kuwafungua macho hawa vijana andaa video zako za namna ya kubadili maisha kupitia rasilimali zinazowazunguka,kilimo,ufugaji,biashara,ufundi n.k then andaa program ya kuwafikia kupitia vile vibanda vyao wanavyokutana kuangalia EPL au movies kuwaonyesha mambo yanawezekana iwapo wataamua then kwa wale watakaokuwa tayari kuamua ndio sasa uwasaidie katika safari Yao bila kujali amefail au hakwendashule kabisa au amefika chuo Ila elimu yake hajaweza kuiunganisha na mazingira yanayomzunguka huku wewe ukiwa umejikita kwenye ufugaji na kilimo
Mimi naamini umasikini ni fursa Kama fursa nyingine uzuri wake fursa hii wengi tumeipenda kwasabbu hutoijasho kuifikia,just Kuwa easy kwa kilakitu maisha as usually
 
Back
Top Bottom