Wakuu habar zenu natumai mko poa..naomba kueleweshwa km hii kitu inafanya kazi katika kupata mimba pindi ufanyapo mapenzi siku ya 3 au ya 4 kabla ya kupata period na ikiwa umeshaona dalili zote za kupata hedhi chuchu za maziwa kuuma,chunusi,miguu kuchoka..kuna uwezekano wa kupata mimba?period atapata tarehe20 mwez huu..mzunguko 28dayz!
Jifunze elimu ya uzazi kabla ya kufanya lolite lile linalopelekea wewe kuingia kwenye uumbaji wa kiumbe katika mwili wako
Njia ya asili ya kuzuia mimba hutumiwa na wanawake ambao kwa namna moja au nyingine hawataki kutumia madawa ya kisasa ili kuepuka mabadiliko ya miili yao kama vile kunenepa, kutokwa na majimaji ukeni na pia kuna tetesi kuwa yanaongeza uwezekano kwa mwanamke kupata Saratani ya Kizazi na Matiti.
Kuzuia mimba kwa kutumia tarehe inauhakika ikiwa mzunguuko wako ni uleule na sio mrefu (siku 32-35) wala mfupi (siku 18-24) bali ni ule wa kawaida ambao ni siku 28.
Ili kutumia mtindo/mbinu hii ya kuzuia mimba unapaswa kuanza kuhesabu siku zako sasa na fuatilia kwa karibu mzunguuko wako na kuhakikisha kuwa una siku 28 sio chini wala juu ya hapo. Kwa kawaida unaaza akufuatilia kwa miezi mitatu hadi sita (kama umewahi kutumia madawa ya kuzuia mimba) kabla hujaanza kuitumia njia hii
Namna ya kuhesabu
Ili kuwa na uhakika na urefu au ufupi wa mzunguuko wako unapaswa kuhesabu siku ya kwanza utakayo ona damu mpaka utakapo ona damu ya mwezi utakao fuata. Mfn; leo tarehe 9 mwezi wa nane ndio umeanza hedhi basi hedhi ya mwezi ujao itakuwa tarehe 7 mwezi wa tisa.....hii ni kama mzunguuko wako usiobadilika (sio mrefu au mfupi) ambao ni siku ishirini na nane tu.
Siku ya kwanza ya hedhi mpaka siku ya tisa ni salama na huwezi kushika mimba.
Baada ya hapo mpaka siku ya kumi na nne (yai linapevuka) unakuwa hatarini.
Siku ya kumi na saba mpaka siku ya ishirini na mbili unakuwa salama tena mpaka siku ya ishirini na tatu mpaka ishirini na saba (yai pevu linashuka) hatarini
Lakini ile ya ishirini na nane siku ya hedhi nyingine unakuwa salama tena....
Ili kuwa na uhakika kuwa uko kwenye mstari kuliko kuegemea kwenye tarehe tu unatakiwa kujua mabadiliko ya mwili wako.
Unapokuwa hatarini kushika mimba mara nyingi utahisi nyege zaidi n avilevile utoko wako utabadilika na kuwa mlaini zaidi (kama lotion) na wakati mwingine utahisi ute unatoka (ule kama udenda/mlenda)....ukiona hivyo hakikisha unatumia Condom vinginevyo utashika mimba.
Unapokuwa salama mara nyingi hamu ya kufanya mapenzi inakuwa haipo sana labda "uchokozwe", vilevile utoko wako unakuwa mzito (kama cream/mafuta mazito)na mweupe sana yaani hata wakati wa kujisafisha inakuwa tabu na inaweza kukuchukua muda mrefu zaidi.