Kufanyike ukaguzi wa maghorofa ya muda mrefu kabla hayajaleta maafa kwa watu

Kufanyike ukaguzi wa maghorofa ya muda mrefu kabla hayajaleta maafa kwa watu

mwakavuta

Member
Joined
Sep 22, 2020
Posts
99
Reaction score
306
Wakuu habari? Nina imani wiki imeanza vyema kwenu.

Nimekuwa nikijizuia kuleta hii mada hapa kwa muda mrefu lakini nakosa amani sana.

Kuna tatizo linakuja huko mbeleni kwenye majengo kama hayatatuliwa mapema.

Kwenye harakati zangu za kutafuta maisha kama kibarua wa ujenzi nilikutana na hali iliyonipa mashaka ya usalama kwenye jengo linalotumiwa na watu zaidi ya mia mbili sehemu mojawapo niliyofanya kazi.

Jengo la ghorofa 4 limekatika nyufa kubwa nyingi mno kazi yetu ilikua ni kuziba nyufa hizo. Kwenye uchunguzi wangu nilikuta yafuatayo,

* Nondo za nguzo za jengo zimeoza kwa kutu kiasi ukipiga tindo kidogo tu inakatika nyingine zimeisha kabisa.

Kuna sehemu ilibidi kukata ngazi maana imeoza kabisa na kuotesha nyingine.

* Nguzo zimekatika nyufa kuanzia ground floor mpaka floor ya nne juu, tunajua nguzo ndizo uti wa mgongo wa gorofa, kwa hali niliyoiona pakitokea mtikisiko kidogo jengo litakuwa chini.

Zimetumika kokoto nyeupe za uswahilini sio nyeusi ambazo ni imara zaidi. Sijajua tatizo lilikuwa ni nini "inawezekana walitumia maji ya chumvi kuchanganya zege ndio sababu ya kuozesha nondo".

NB: Sina uhakika kama wataalamu wa majengo walishirikishwa kutoa maoni yao juu ya aina ya marekebisho hayo, lakini kwa upande wangu njia pekee ya kutatua tatizo ilikua kubomoa jengo lote lisitumike zaidi ya miaka kumi.

Naomba kuwe na Sera ya ukaguzi wa wa usalama wa haya majengo kila baada ya muda, tatizo likitokea yatakua maafa maafa makubwa.
 
Sawa mkuu wahusika watakuwa wamekusikia watalifanyia kazi
 
Dah aisee, very serious alert hii lakini shida mkuu ni zile zile PUMBAVU ambazo zinakusanya mlungula hata kwa mambo serious.

Maghorofa mengi Dar es Salaam na Tanzania haya ya watu binafsi na makampuni binafsi ni hatari sana kwa maisha ya watu, kwanza mengi usimamizi wake ni wakienyeji, mamlaka zinazohuzika hazishiriki kikamilifu, makampuni mengi yanayojenga ni ya kihuni kihuni with no qualified people. HILI LINAHITAJI USERIOUS WA HALI YA JUU
 
Dah aisee, very serious alert hii lakini shida mkuu ni zile zile PUMBAVU ambazo zinakusanya mlungula hata kwa mambo serious

Maghorofa mengi Dar es salaam na Tanzania haya ya watu binafsi na makampuni binafsi ni hatari sana kwa maisha ya watu, kwanza mengi usimamizi wake ni wakienyeji, mamlaka zinazohuzika hazishiriki kikamilifu, makampuni mengi yanayojenga ni ya kihuni kihuni with no qualified people. HILI LINAHITAJI USERIOUS WA HALI YA JUU
Kweli mkuu ubaya zaidi linatumiwa zaidi na watoto najaribu kuwaza tatizo likitokea hao wazazi watakua kwenye hali gani.

Kuna wakati wahusika wanatakiwa kujali zaidi utu kuliko kitu chochote.
 
Ulichoongea ni sahihi kabisa mkuu,
Majengo mengi ya ghorofa yanayojengwa hapa nchini ubora wake ni wakutilia mashaka sana, kinachotunusuru ni tupo kwenye ukanda ambao hauathiriwa sana na matetemeko ya ardhi.
Ila kama itatokea siku tukapitiwa na tetemeko kubwa kiasi majengo mengi yatashuka chini.
 
Wakuu habari? Nina imani wiki imeanza vyema kwenu.

Nimekua nikijizuia kuleta hii mada hapa kwa muda mrefu lakini nakosa amani sana.

Kuna tatizo linakuja huko mbeleni kwenye majengo kama hayatatuliwa mapema.

Kwenye harakati zangu za kutafuta maisha kama kibarua wa ujenzi nilikutana na hali iliyonipa mashaka ya usalama kwenye jengo linalotumiwa na watu zaidi ya mia mbili sehemu mojawapo niliyofanya kazi.

Jengo la ghorofa 4 limekatika nyufa kubwa nyingi mno kazi yetu ilikua ni kuziba nyufa hizo. Kwenye uchunguzi wangu nilikuta yafuatayo,

* Nondo za nguzo za jengo zimeoza kwa kutu kiasi ukipiga tindo kidogo tu inakatika nyingine zimeisha kabisa.
Kuna sehemu ilibidi kukata ngazi maana imeoza kabisa na kuotesha nyingine.

* Nguzo zimekatika nyufa kuanzia ground floor mpaka floor ya nne juu, tunajua nguzo ndizo uti wa mgongo wa gorofa, kwa hali niliyoiona pakitokea mtikisiko kidogo jengo litakua chini.

Zimetumika kokoto nyeupe za uswahilini sio nyeusi ambazo ni imara zaidi. Sijajua tatizo lilikua ni nini "inawezekana walitumia maji ya chumvi kuchanganya zege ndio sababu ya kuozesha nondo".

NB: Sina uhakika kama wataalamu wa majengo walishirikishwa kutoa maoni yao juu ya aina ya marekebisho hayo, lakini kwa upande wangu njia pekee ya kutatua tatizo ilikua kubomoa jengo lote lisitumike zaidi ya miaka kumi.

Naomba kuwe na Sera ya ukaguzi wa wa usalama wa haya majengo kila baada ya muda, tatizo likitokea yatakua maafa maafa makubwa.
Nondo za nguzo za jengo zimeoza kwa kutu kiasi ukipiga tindo kidogo tu inakatika nyingine zimeisha kabisa.
Kuna sehemu ilibidi kukata ngazi maana imeoza kabisa na kuotesha nyingine.

* Nguzo zimekatika nyufa kuanzia ground floor mpaka floor ya nne juu, tunajua nguzo ndizo uti wa mgongo wa gorofa, kwa hali niliyoiona pakitokea mtikisiko kidogo jengo litakua chini.

Zimetumika kokoto nyeupe za uswahilini sio nyeusi ambazo ni imara zaidi. Sijajua tatizo lilikua ni nini "inawezekana walitumia maji ya chumvi kuchanganya zege ndio sababu ya kuozesha nondo".[emoji15][emoji15][emoji2827][emoji2827][emoji2827]
 
Wakuu habari? Nina imani wiki imeanza vyema kwenu.

Nimekua nikijizuia kuleta hii mada hapa kwa muda mrefu lakini nakosa amani sana.

Kuna tatizo linakuja huko mbeleni kwenye majengo kama hayatatuliwa mapema.

Kwenye harakati zangu za kutafuta maisha kama kibarua wa ujenzi nilikutana na hali iliyonipa mashaka ya usalama kwenye jengo linalotumiwa na watu zaidi ya mia mbili sehemu mojawapo niliyofanya kazi.

Jengo la ghorofa 4 limekatika nyufa kubwa nyingi mno kazi yetu ilikua ni kuziba nyufa hizo. Kwenye uchunguzi wangu nilikuta yafuatayo,

* Nondo za nguzo za jengo zimeoza kwa kutu kiasi ukipiga tindo kidogo tu inakatika nyingine zimeisha kabisa.
Kuna sehemu ilibidi kukata ngazi maana imeoza kabisa na kuotesha nyingine.

* Nguzo zimekatika nyufa kuanzia ground floor mpaka floor ya nne juu, tunajua nguzo ndizo uti wa mgongo wa gorofa, kwa hali niliyoiona pakitokea mtikisiko kidogo jengo litakua chini.

Zimetumika kokoto nyeupe za uswahilini sio nyeusi ambazo ni imara zaidi. Sijajua tatizo lilikua ni nini "inawezekana walitumia maji ya chumvi kuchanganya zege ndio sababu ya kuozesha nondo".

NB: Sina uhakika kama wataalamu wa majengo walishirikishwa kutoa maoni yao juu ya aina ya marekebisho hayo, lakini kwa upande wangu njia pekee ya kutatua tatizo ilikua kubomoa jengo lote lisitumike zaidi ya miaka kumi.

Naomba kuwe na Sera ya ukaguzi wa wa usalama wa haya majengo kila baada ya muda, tatizo likitokea yatakua maafa maafa makubwa.
Asante kwa alert Ila ungekuwa Bora ilo jengo ungelitaja na location lilipo ili kunusuru janga tarajiwa lisitokee na kuleta madhara watu. Ni kweli hili Ni tatizo kubwa mno, majengo mengi ubora wake Ni wa kutumiwa Shaka Sana. Kuna jengo moja la ghorofa nne Kama sikosei liko Namanga mtaa Kama unaingia Don Bosco Lina matank ya maji kadhaa kwa juu (summit floor). Ilo jengo siku so nyingi litaleta maafa kwa watumishi na majirani, tafadhari mamlaka husika fanya uchunguzi na chukua hatua
 
Asante kwa alert Ila ungekuwa Bora ilo jengo ungelitaja na location lilipo ili kunusuru janga tarajiwa lisitokee na kuleta madhara watu. Ni kweli hili Ni tatizo kubwa mno, majengo mengi ubora wake Ni wa kutumiwa Shaka Sana. Kuna jengo moja la ghorofa nne Kama sikosei liko Namanga mtaa Kama unaingia Don Bosco Lina matank ya maji kadhaa kwa juu (summit floor). Ilo jengo siku so nyingi litaleta maafa kwa watumishi na majirani, tafadhari mamlaka husika fanya uchunguzi na chukua hatua
Hili jengo liko mbweni,
Ni shule ya English medium kubwa tu wahusika wafatilie.
Nina imani sijaharibu brand ya mtu
 
Nondo za nguzo za jengo zimeoza kwa kutu kiasi ukipiga tindo kidogo tu inakatika nyingine zimeisha kabisa.
Kuna sehemu ilibidi kukata ngazi maana imeoza kabisa na kuotesha nyingine.

* Nguzo zimekatika nyufa kuanzia ground floor mpaka floor ya nne juu, tunajua nguzo ndizo uti wa mgongo wa gorofa, kwa hali niliyoiona pakitokea mtikisiko kidogo jengo litakua chini.

Zimetumika kokoto nyeupe za uswahilini sio nyeusi ambazo ni imara zaidi. Sijajua tatizo lilikua ni nini "inawezekana walitumia maji ya chumvi kuchanganya zege ndio sababu ya kuozesha nondo".[emoji15][emoji15][emoji2827][emoji2827][emoji2827]
Ushangae mkuu hicho nilichokioni mwenyewe kuna wakati nilikuwa naogopa kutembea kwenye canopy zake tabu tupu.
 
Mkuu ebu tupia kapicha tulijue na sisi tuchukue tahadhari...
 
Hili jengo liko mbweni,
Ni shule ya English medium kubwa tu wahusika wafatilie.
Nina imani sijaharibu brand ya mtu

Hatari Sana , MOGA au GHOMME? Weka wazi usaidie watoto wasije wakapata madhara.
 
Back
Top Bottom