Kufeli kwa watu shule ya sheria (Law School)

tangopoli

Member
Joined
May 8, 2014
Posts
5
Reaction score
0
Kabla sijaingia shule ya sheria nilikuwa nashangaa kuona wingu la wanafunzi wakifeli, lakini sasa baada ya kuingia nimeona kwa nini watu wanafeli. Sababu kubwa ni mrundikano wa masomo na ratiba.

We fikiria watu wanaingia darasani mpaka sasa kufundishwa na jumatatu ya terehe 19/5 wanaanza Individual Continue Assessment (ICA). Na ikiwa wiki hii wanafundishwa probate and adminstration of estate law na tena wamenyimwa siku za kujiandaa.

Hii sio haki, wapeni muda wajiandae.
 
Ndo ujipinde. Kwa taarifa yako tu shule ya sheria ya sasa sio kama tulikotoka yawning from 1st-5th cohort. Wakati Wanatumia majengo ya Udsm au Duce. Kuna marekebisho mengi saana yamefanyika hata sheria ya LST Ilifanyiwa marekebisho. Masomo yalikuwa mengi mnoo ukilinganisha NA sasa. Kwa hyo SOMA kwa bidiii sana. Ukitaka zaidi uliza tukujibu.
 
uongozi wenu wa wanafunzi ni mbovu. wako jamaa zangu walikuwa kohort ya tisa walipata muda wa kutosha wa kujiandaa.hii ilitokana na uongozi shupavu wa Petro E. Mselewa katika kohort hiyo. mtafuteni awafunde
 
Last edited by a moderator:
Kwa sasa hamsomi. Hakuna kitu kigumu. Someni mtafaulu. Tatizo la baadhi ya wanafunzi hawasomi wanadhani wakimaliza LLB huko walikosoma basi wanajua sana hawasomi wengine wanajivunia vyuo walivyosoma huku wakiwa hawana kitu kichwani. Mimi nimesoma cohort ya tatu na nilifaulu Moja kwa Moja. Sikuona kitu cha ajabu au kigumu huko 'Law School of Tanzania'. Hii ni kwa upande mmoja.

Kwa upande wa pili vyuo vingi hapa nchini haviwaandai vizuri wanafunzi wao kwa hiyo wakifika huko wanasumbuka sana. Pia Kuna wahadhili walifundisha law school Halafu nikaapishwa nao uwakili. Wahadhili hawa naamini hawafai kufundisha shule ya Sheria kwa kuwa hawana uzoefu Wa kutosha katika 'practice'.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…