Kufikia guest vs kufikia kwa ndugu

Kufikia guest vs kufikia kwa ndugu

cold water

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2021
Posts
238
Reaction score
954
Let s say unaenda sehemu fulani ni ugenini na hiyo sehemu unayoenda inaweza kuwa na ndugu zako au marafiki vipi ni bora ufikie guest au kwa ndugu? Hilo ni swali sasa twendeni kwenye point au ujumbe niliotaka ku-share hapa.

Nilisafiri last month kutoka mkoa ninaoishi kwenda mkoa fulani, nilifikia kwa rafiki jamani nilitumia gharama nyingi nikajisemea moyoni bora ningefikia guest

Nilivyofika tu ile siku ya kwanza kunipokea nikampa elfu tano kama matumizi aongezee kwenye suala la chakula, nimefika kwake kama leo, kesho yake akanambia sina vitu ndani (chakula) twende town, nikamwambia sawa.

Anapoishi ni mbali kidogo na mji japo sio sana ni kama dk 10_15, ukipanda boda boda. Katika hiyo safari cost zilivyoanza sasa tukapanda boda hadi sehemu Fulani, muda wa kumpa nauli boda boda sasa, friend akatoa elfu kumi boda akasema sina chenji, rafiki yangu akaniuliza huna ela ndogo hapo nitakurudishia, kweli nilikuwa nayo ela ndogo nikaitoa,ilo likapita

Tukaenda tena sehemu fulani kununua maji kwenye dumu kubwa la lita 10, akatoa hela muuzaji akasema hana chenji, friend akaniuliza tena huna ela ndogo hapo nitakupa nikatoa tena. Sokoni sasa kufanya hiyo shopping yake ya chakula kila ela anayotoa wauzaji hawana chenji mimi ndio nilikuwa na ela ndogo ndogo bwana nikajikuta nimetumia ela nyingi

Tulivyokuwa tunarudi tulipanda bajaji, anaambiwa nauli friend hana ela ndogo tena ikabidi niendelee kutoa zangu. Tumerudi home hakunipa zile ela mi nikampotezea wala sikumkumbusha.

Siku ya tatu nikasepa maana nilikaa siku tatu tu.

Kisa cha kwenda kwa rafiki ni hiki mkoa huo huo kuna ndugu yangu kiukoo ila sio ndugu kivile alinipokeaga Mara ya kwanza before sijafikia kwa friend, ndugu yangu alipika chips muda wa kunisevia chakula akawa anatumia mikono, yaani zile chips anazichota kwa mikono kama kijiko ivi huku naona na bwana ake anamuangalia tu, bwana ake ndo ndugu yangu mimi, nyama ya kuku alikaanga kavu, nayo akawa ananitilia kwa mikono, though nilikula hivyo hivyo kwa kujikaza lakini kitendo hicho hakikunifurahisha ndo maana awamu ya pili nikaamua kufikia kwa rafiki angu, coz niliona guest gharama japo maisha ya guest ni ya ku-relax sana.
 
Kila upande una changamoto zake mkuu, ungeenda guest pia ungekutana na kashkash zake uwenda zingekukera pia, usisahau kupitia uzi mmoja humu jukwaani unaelezea vituko vya lodge.
 
Kuna makabila haya uoni aya kuwapa ndugu zao shida ya kuwalaza siku nyingi haliakua wamekuja kufanya biashara zao mijini, ........kuna kabila ni wasitarabu hufikia guest na kuenda kusalimia ndugu zao mchana na kurudi guest mpaka aombwe kulala ndo atalala.

Watanzania tuache ushamba hamna haja ya kuenda kwa ndugu kuishi bila mualiko, watu hiushi kwa bajeti hukuna vyumba vya wageni siku hizi acheni kukosesha watoto wa wenzenu raha kuwalazimisha kulala sebuleni,na nyie kulala kwenye vyumba vya watoto.
 
Mkuu unalalamika na hela ambazo mwenyewe unaziita hela ndogo.

1. Kwa jinsi ulivyoeleza hapo ni kama ulikuwa unatoa hela ndogo ndogo za boda, kununua maji nk. Mbona kama hizi kwa ujumla wake itakuwa ni ndogo kuliko ungefikia gest?

2. Hata kama hizo hela zitalingana au kuzidi kidogo gest lakini husikii vizuri mkuu kuthaminisha urafiki wenu? Kamwe haifai kuthaminisha urafiki/undugu against hela

3. Umekonsida ishu ya usalama huko mkoani ulipoenda. Huoni kulala kwa rafiki/ndugu ni bora kuliko gest kiusalama mkuu? Thamani ya usalama na afya yako oviasi inazidi hizo hela za boda unazolalamikia

4. Akiwa kama rafiki yako, hakuna ishu yoyote umewahi kumuomba akakusaidia? Kwanini roho ikuume kwa kumlipia rafiki yako ambae kimsingi kajitolea kukuhifadhi ugenini hela ndogo hizo ulizosema mkuu
 
Let s say unaenda sehemu Fulani ni ugenini na iyo sehemu unayoenda inaweza kuwa na ndugu zako au marafiki vipi ni bora ufikie guest au kwa ndugu? Ilo ni swali sasa twendeni kwenye point au ujumbe nilotaka kushare hapa. nilisafiri last month kutoka mkoa ninaoishi kwenda mkoa Fulani,nilifikia kwa rafiki jamani nilitumia gharama nyingi nikajisemea moyoni bora ningefikia gest,nilivyofika tu nikampa elfu tano kama matymizi aongezee kwenye swala la chakula,nimefika kwake kama Leo kesho yake akanambia sina vitu ndani (chakula) twende town,nikamwambia sawa. anapoishi ni mbali kidogo na mji japo sio sana ni kama dk 10_15,ukipanda boda boda, katika safari iyo cost zilivyoanza sasa tukapanda boda hadi sehemu Fulani mda wa kumpa ela boda boda sasa,friend akatoa elfu kumi boda akasema sina chenchi rafiki angu akaniuliza una ela ndogo hapo nitakurudishia, kweli nilikuwa nayo ela ndogo nikaitoa,ilo likapita tukaenda tena sehemu Fulani kununua maji akatoa ela muuzaji akasema hana chenchi friend akaniuliza tena huna ela ndogo hapo nitakupa nikatoa tena,sokoni sasa kufanya iyo shopping yake ya chakula kila ela anayotoa wauzaji hawana chenchi Mimi ndo nilikuwa na ela ndogo ndogo bwana nikajikuta nimetumia ela nyingi,tulivyokuwa tunarudi tulipanda bajaji,anaambiwa nauli friend hana ela ndogo ikabidi niendelee kutoa zangu, tumerudi home hakunipa zile ela mi nikampotezea wala sikumkumbusha. siku ya pili nikasepa mana nilikaa siku tatu tu.
umejifunza na kupata somo songa mbele acha lawama......

kuna siku utaenda huko tena kimyakimya eti kwa kukwepa hizo gharama unakaa kimya humwambii kama upo town na bahati mbaya utapamiwa na baiskeli au mkokoteni ukaumia vibaya, bila shaka bado huyo mjamaa unaemlaumu atakua msaada sana kwako......

Yaliyopita si ndwele tugange yajayo......
 
Uchumi mdogo, huna pesa ya guest house, nako kwa ndugu uchumi mdogo, mwendo wa kusitiriwa malazi ya fedheha!!
 
Uchumi mdogo, huna pesa ya guest house, nako kwa ndugu uchumi mdogo, mwendo wa kusitiriwa malazi ya fedheha!!
Kama huna kwanini usafiri kuapa watu wengine shida zako tulia kwako, mpaka pale utakapo pata pesa.
 
Mkuu unalalamika na hela ambazo mwenyewe unaziita hela ndogo.

1. Kwa jinsi ulivyoeleza hapo ni kama ulikuwa unatoa hela ndogo ndogo za boda, kununua maji nk. Mbona kama hizi kwa ujumla wake itakuwa ni ndogo kuliko ungefikia gest?

2. Hata kama hizo hela zitalingana au kuzidi kidogo gest lakini husikii vizuri mkuu kuthaminisha urafiki wenu? Kamwe haifai kuthaminisha urafiki/undugu against hela

3. Umekonsida ishu ya usalama huko mkoani ulipoenda. Huoni kulala kwa rafiki/ndugu ni bora kuliko gest kiusalama mkuu? Thamani ya usalama na afya yako oviasi inazidi hizo hela za boda unazolalamikia

4. Akiwa kama rafiki yako, hakuna ishu yoyote umewahi kumuomba akakusaidia? Kwanini roho ikuume kwa kumlipia rafiki yako ambae kimsingi kajitolea kukuhifadhi ugenini hela ndogo hizo ulizosema mkuu
Tena kwa kuongezea Mkuu Rafiki yake sio kamuomba au alikuwa hana hela ya kununua chakula!! Ila alikuwa anatoa tshs10000/= inakosekana chenji sasa swali la kujiuliza yeye kula vya Rafiki yake na kulala kwake anaona sawa ila yeye vyakwake kuliwa kidogo anaona maumivu!!!

Ila uzuru umeidhirisha tabia yako hapa JF kuwa wewe ni mchoyo(mgila) mtu anapenda kula peke yake cha kwake chake cha wenzie chake
 
Let s say unaenda sehemu fulani ni ugenini na hiyo sehemu unayoenda inaweza kuwa na ndugu zako au marafiki vipi ni bora ufikie guest au kwa ndugu? Hilo ni swali sasa twendeni kwenye point au ujumbe niliotaka ku-share hapa.

Nilisafiri last month kutoka mkoa ninaoishi kwenda mkoa fulani, nilifikia kwa rafiki jamani nilitumia gharama nyingi nikajisemea moyoni bora ningefikia guest

Nilivyofika tu ile siku ya kwanza kunipokea nikampa elfu tano kama matumizi aongezee kwenye suala la chakula, nimefika kwake kama leo, kesho yake akanambia sina vitu ndani (chakula) twende town, nikamwambia sawa.

Anapoishi ni mbali kidogo na mji japo sio sana ni kama dk 10_15, ukipanda boda boda. Katika hiyo safari cost zilivyoanza sasa tukapanda boda hadi sehemu Fulani, muda wa kumpa nauli boda boda sasa, friend akatoa elfu kumi boda akasema sina chenji, rafiki yangu akaniuliza huna ela ndogo hapo nitakurudishia, kweli nilikuwa nayo ela ndogo nikaitoa,ilo likapita

Tukaenda tena sehemu fulani kununua maji kwenye dumu kubwa la lita 10, akatoa hela muuzaji akasema hana chenji, friend akaniuliza tena huna ela ndogo hapo nitakupa nikatoa tena. Sokoni sasa kufanya hiyo shopping yake ya chakula kila ela anayotoa wauzaji hawana chenji mimi ndio nilikuwa na ela ndogo ndogo bwana nikajikuta nimetumia ela nyingi

Tulivyokuwa tunarudi tulipanda bajaji, anaambiwa nauli friend hana ela ndogo tena ikabidi niendelee kutoa zangu. Tumerudi home hakunipa zile ela mi nikampotezea wala sikumkumbusha.

Siku ya tatu nikasepa maana nilikaa siku tatu tu.

Kisa cha kwenda kwa rafiki ni hiki mkoa huo huo kuna ndugu yangu kiukoo ila sio ndugu kivile alinipokeaga Mara ya kwanza before sijafikia kwa friend, ndugu yangu alipika chips muda wa kunisevia chakula akawa anatumia mikono, yaani zile chips anazichota kwa mikono kama kijiko ivi huku naona na bwana ake anamuangalia tu, bwana ake ndo ndugu yangu mimi, nyama ya kuku alikaanga kavu, nayo akawa ananitilia kwa mikono, though nilikula hivyo hivyo kwa kujikaza lakini kitendo hicho hakikunifurahisha ndo maana awamu ya pili nikaamua kufikia kwa rafiki angu, coz niliona guest gharama japo maisha ya guest ni ya ku-relax sana.
Bure gharama, unapenda kitonga sana ndo maana unapigwa matukio tumia chako kwa ndugu kasalimie tuu kama umeenda kikazi.
 
Sasa unavyolalamika umenunua maji ulitaka ukae bure,ule bure usichangie chochote?Huoni kama umesave 10k ya gesti Sasa maji ya elfu tatu lazima ununue,maisha yamebadilika kila kitu kinalipiwa
 
Bora guest aise kilichokuwa kinanikera kufikia kwa ndugu ni kila ahsubuhi wana kaibada na usiku kabla ya kulala wana kaibada nilikuwa najilazimisha tu hivyohivyo kingine huwa napenda kurudi home usiku pale nilikuwa najaribu kujizuia lakini nashindwa nilikuwa naingia wakiwa wamelala.Tatizo la guest unakuwa kama homeless vile
 
Ukishakua mtu mzima jitahidi sana kuishi kwenye serikali yako....waache watu wengine na serikali zao, kwanini mkerane kisa vitu vidogo vidogo??? Safiri kakae lodge utaenda kusalimia
 
Kila upande una changamoto zake mkuu, ungeenda guest pia ungekutana na kashkash zake uwenda zingekukera pia, usisahau kupitia uzi mmoja humu jukwaani unaelezea vituko vya lodge.
Ivi izo uzi unazpatqjee wazee
 
Mtoa mada ni jinga sana ,yani mtu aliyekupokea kwa upendo na huko kote alikua anatoa pesa zake hizo changamoto za chenji kwani yeye ndio sababu?

Sent from my Infinix X6517 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom