Napajua hapo mahali wanapolima maharage katika eneo hilo la KIA, hata sisi tuliwahi kukodisha shamba katika eneo hilo, nadhani panaitwa MATIBA au MAKIBA, kama sikosei............
Je sasa unadhani kilichimuua huyo mzee ni mazao kukauka au mkopo wa benki?
Kwa tulivyoumbwa binadamu mioyo yetu imekaa na alwayz huwa inajiandaa kupokea habari nzuri na zile ambazo tunazipenda. Ni vigumu sana kiakili na kimwili kubaki in normal situation pale ambapo unapata habari usiyoipenda.
Any wayz kitu ninachoweza kujifunza hapa ni kwamba kila jambo lina pande nyingi..every problem has opportunities in it!!
ukiwa kijana hizi theory zina maana ila kadiri unavyozeeka hizi theory huziwezi.
Kwa mtu wa miaka 45+ kupoteza nyumba ni msiba kabisa kuliko kijana wa miaka 26 kupoteza nyumba hiyo hiyo.
Maumivu huwa makubwa kulingana na nguvu uliyotumia kupata nyumba hiyo, imagine at my age nipotze nyumba sasa si nitarukwa akili?? Ila nilipokuwa kijana ningeweza vumilia au kuchukulia positively.
Kongosho bana.............
Awali uli-comment vizuri, lakini sasa unaharibu..........................
Ni vyema tukajifunzxa kwamba kamwe hatuwezi kushindana na hali halisi, kama nyumba inaungua hatuwezi kubadili hali hiyo, kikubwa ni usalama wa afya zetu na afya za wale waliotuzunguka, kuumia kihisia au kulia sana kamwe hakuwezi kubadili hali hiyo. Jambo muhimu hapo ni kuangalia maisha yatakuwaje baada ya hapo na si kuendelea kujuta na kujilaumu au hata kumtafuta mchawi. Hatuwezi kubadili jambo ambalo limekwishatokea ni sawa na kufanya juhudi kubwa kujaribu kufufua mzoga..........................
Labda niwape kisa kingine ambacho ni maarufu sana. Kuna bwana mmoja ambaye anajulikana kama ni bingwa wa kutokata tamaa naye si mwingine bali ni mgunduzi wa balbu hii ya umeme, bwana Thomas Edison. Labda kwa kifupi kwa wale wasiomjua Thomas Edison, huyu jamaa alifanya majaribio 1000, wakati akiwa katika mchakato wa kugundua Balbu. Ingawa wakati mwingine watu wanatofautiana ki takwimu katika kuelezea habari zake, lakini mimi kitabu nilichosoma kinasema alifanya majaribio 1000 ya kutengeneza balbu ndipo akafanikiwa kuwasha hii balbu ya umeme tunayotumia,
Hebu fikiria majaribio 1000 ndio ufanikiwe, ajabu ee!!
Lakini pia katika majaribio hayo alikuwa anapata vikwazo kadhaa, mojawapo ya tukio kubwa ni lile la maabara yake kuungua na hivyo kupoteza mafaili yake yote ya kumbukumbu za ugunduzi wake. Cha kushangaza wakati anaangalia yale majivu ya makabrasha yake aliwaambia wasaidizi wake kuwa imekuwa vyema yale mafaili yaliyohifadhi kumbukumbu za majaribio yake yaliyoshindwa yameungua kwa hiyo hakuna haja ya kuhangaika na majaribio yaliyoshindwa na badala yake waanze upya.
Si hivyo tu bali alikiri kwamba katika majaribio hayo pia amejifunza kushindwa!
Baadae ndipo wakafanikiwa kuwasha balbu.
Je umeona jinsi mtu huyu alivyo na akili za ajabu?
Hivi ni mara ngapi sisi tunakwama katika shughuli zetu na kujipongeza japo kwa kushindwa kwetu?
Rafiki yangu SnowBall amezungumzia kitu kinachoitwa Dialectic Thinking. Amesema kila jambo lina pande mbili, kwa mfano kama kuna kushinda basi kuna kushindwa, na kama kuna kupata, kuna kukosa pia.
Mifano iko mingi sana.
Lakini swali la msingi hapa ni, je tumefundishwa nini kuhusiana na hizi pande mbili?
Je ni kweli kuna upande mbaya na mzuri?
Ni nani aliyekufundsha hivyo?
Ukweli ni kwamba hakuna upande mbaya katika kila jambo, bali tafsiri zetu ndizo zinazotupotosha. Kufanikiwa na kutokufanikiwa kwa jambo lolote ni mojawapo ya changamoto za kujifunza. Tunaweza kujifunza kutokana na kufanikiwa na pia tunaweza kujifunza kutokana na kutofanikiwa.................
Kongosho katika mambo ambayo nimejifunza na ninashukuru nimemudu, ni kutoumizwa na tukio lolote linaloitwa baya. kwanza mimi siamini kama kuna tukio baya, ninachofanya ni kuyapokea matukio yote yawe mabaya au mazuri na kuangalia namna gani nitajifunza kutokana na tukio hilo.........
kama umesoma vizuri posti yangu utagundua kwmaba kinachotuumiza wengi ni namna tunavyotafsiri matukio yanayotutokea na ndio sababu yanatuumiza.
Kama tukiyapokea matukio kwa namna ya kujifunza, mara nyingi huwa washindi, lakini tukibaki kujuta, na kuomboleza maisha yetu yatakuwa ya ajabu sana na afya zetu zitakuwa nyondenyonde na kuna uwezekano wa kupoteza maisha....