Kufuatia kusambaa kwa Corona (covid-19); Nakusudia kumshitaki Waziri wa Afya, Miundombinu na Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Mbona kama umeandika kama una hasira mkuu?
Kweli kabisa waache corona ituathiri hivi hivi ?
hasira lazima iwepo hivi unaona wanavotufanyia ni sawa? huyu bashite anaitisha mikusanyiko akijua hairuhusiwi inamana huyu kajitoa ufaham kaamua wacha niwakusanye watanzania waambukizane alafu sirikale inamtazama tu kisa ni MTOTO WA MZEE BABA alafu huku kwenye madaldala ukisimamisha tu mtu mmoja unashushwa na bakora juu.. sasa hii utasema nchi inapambana au inatesa wananchi
 
Sio lazima itangazwe kuwa mipaka imefungwa. Kila nchi inaiona hali halisi na ndio sababu huoni ndege angani tangu ugonjwa huu upambe moto.

Halafu dhana ni mbovu kuamini kwamba kila mgeni wa sasa ndio mleta ugonjwa, kuna watu kwa sasa wanaendeleza kusambaza hii kitu na ni ndugu na jamaa zetu wa karibu.
 
Umshtaki mwanasheria na waziri wa afya wakati huu ugonjwa ukiwa umepamba moto, hizo ni akili fulani ndogo sana.

La muhimu ni kisisitizia juu ya namna za kujingika ili ugonjwa usiendelee kusambaa. Tanzania haijawahi kuwa kisiwa na haitakuja iwe.

Tunapoijadili corona tuwe na mtazamo wa janga la dunia.
 
Kwa hapa tulipofikia idadi ya wagonjwa 20,naweza kusema bado haujapamba moto, serikali inatakiwa kufunga airports, bandari,mipaka ili kuzuia kupamba moto na kumaliza kabisa new cases za wagonjwa wa corona,
Nasisitiza ugonjwa haujapamba moto hapa nchini kwetu ila tuna uwezo pia wa kuzuia usipambe moto
 
Hao wanaosambaza chanzo ni mgeni aliyeshuka kwenye ndege,kuvuka mipaka na kuingia Tanzania.
 
Mamaangu wewe hivi unajitambua kweli au ''COLONA'' imekupitia?
Kama huamini basi endelea na story zako za kijiweni. Panua ubongo wako.

Ndiyo RESOCHIN dawa ambayo inatumika kutibu malaria pa ni dawa ambayo inaweza kuondoa maradhi yanayo sababishwa na CORONAVIRUS 100%.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Achana na ndoto hizo mkuu. Hivyo wewe unacheza na wadhifa wa waziri au Rais? Mimi nakuomba usipoteze mda wako. Tafuta mambo mengine ambayo atakusaidia katika katika maisha yako.

Kama unausaka umaarufu please, fanya hakuna mtu atakaye kuzuia. Lakini huwezi kumshtaki Rais Tanzania na ukashinda. Hiyo sahau.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Simshitaki rais namshitaki waziri
 
Pingamizi la kwanza litakuwa ni kwamba mahakama huwa haishughuliki na hypothetical issues, kwa hiyo usipoteze muda.
 
Pingamizi la kwanza litakuwa ni kwamba mahakama huwa haishughuliki na hypothetical issues, kwa hiyo usipoteze muda.
Nimemuuliza mwanasheria wangu kaniambia pingamizi lolote lile lazima li-base kwenye purely point of law yaani lihusu hoja za kisheria, kaniambia pia ukasome kesi ya Mukisa biscuit imeeleza vizuri kuhusu pingamizi.

Land saveya
 
wana bodi bado lengo langu na kufungua kesi lipo,
Natunaona jinsi waziri wa uchukuzi alivyokaidi kufunga mipaka,viwanja vya ndege,bandari jinsi linavyoleta madhara kwetu watanzania
 
Umekosa kazi za kufanya, ndo nyie Makonda anawatafuta mkazibue mitaro

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…