05 May 2022
SIKU YA KUADHIMISHA URITHI WA DUNIA AFRIKA, WIZARA KUBOMOA MAJENGO YA URITHI KILWA
Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia mamlaka ya usimamizi wanyama-pori TAWA ikiadhimisha siku ya urithi wa dunia Afrika imesema ina mpango wa kuboresha mazingira ya Kilwa Kisiwani kwa kubomoa nyumba zenye urithi wa historia, tamaduni ambazo zimenakiliwa katika historia ya eneo hilo.
Wizara imesema kuwajengea nyumba mpya za kisasa kutafanya wenyeji kuweza kuwa na nyumba za kisasa kuweza kuwa B& B ya vyumba viwili, chumba cha wageni, jiko na maliwato ili kunufaisha wenyeji wa Kilwa na pia malazi kwa wageni na watalii watakaotembelea eneo hilo lenye urithi wa majengo, utamaduni na mila zinazotambulika kama urithi wa dunia kupitia UNESCO
Hata hivyo wenyeji wa Kilwa wanajivunia historia yao na wanapenda nyumba chakavu za kihistoria kufanyiwa ukarabati na kuongezewa vitu vya kisasa bila kupoteza asili ya nyumba hizo zenye muundo, nakshi, sanaa za asili, nyimbo, tamaduni na muonekano wa kusimulia historia ya karne kadhaa za wenyeji na wageni walioishi hapo kwa mamia ya miaka ambavyo huwezi kuvikuta isipokuwa Kilwa Tanzania.
Kule nchini Ugiriki, Italian n.k maeneo ya urithi wa kihistoria na utamaduni wa karne nyingi huhifadhiwa na kubakishwa kwa muonekano huo wa kale huku mazingira yake yakiboreshwa bila kuathiri urithi unaovutia watalii na wenyeji pia wanaopenda kutembelea eneo linaloweza kufananishwa na makumbusho ya wazi ( Open Museum).
Msanii wetu mtanzania alitumia fursa kama hiyo ya mandhari ya kipekee ya historia ya Ugiriki na kutengeneza wimbo wake ambao pia kiaina umefanikiwa kutangaza mandhari zilizotunzwa kwa mamia ya miaka na kuwa sehemu inayovutia watalii kwa mamia kutembelea Greece kutokana na upekee wa eneo hilo linalobebwa kihistoria na kitalii .
MAONO YA MH. RAIS, ZIARA YAKE KUITANGAZA KUPITIA TANZANIA ROYAL TOUR
SIKU YA KUADHIMISHA URITHI WA DUNIA AFRIKA, WIZARA KUBOMOA MAJENGO YA URITHI KILWA
Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia mamlaka ya usimamizi wanyama-pori TAWA ikiadhimisha siku ya urithi wa dunia Afrika imesema ina mpango wa kuboresha mazingira ya Kilwa Kisiwani kwa kubomoa nyumba zenye urithi wa historia, tamaduni ambazo zimenakiliwa katika historia ya eneo hilo.
Wizara imesema kuwajengea nyumba mpya za kisasa kutafanya wenyeji kuweza kuwa na nyumba za kisasa kuweza kuwa B& B ya vyumba viwili, chumba cha wageni, jiko na maliwato ili kunufaisha wenyeji wa Kilwa na pia malazi kwa wageni na watalii watakaotembelea eneo hilo lenye urithi wa majengo, utamaduni na mila zinazotambulika kama urithi wa dunia kupitia UNESCO
Hata hivyo wenyeji wa Kilwa wanajivunia historia yao na wanapenda nyumba chakavu za kihistoria kufanyiwa ukarabati na kuongezewa vitu vya kisasa bila kupoteza asili ya nyumba hizo zenye muundo, nakshi, sanaa za asili, nyimbo, tamaduni na muonekano wa kusimulia historia ya karne kadhaa za wenyeji na wageni walioishi hapo kwa mamia ya miaka ambavyo huwezi kuvikuta isipokuwa Kilwa Tanzania.
Kule nchini Ugiriki, Italian n.k maeneo ya urithi wa kihistoria na utamaduni wa karne nyingi huhifadhiwa na kubakishwa kwa muonekano huo wa kale huku mazingira yake yakiboreshwa bila kuathiri urithi unaovutia watalii na wenyeji pia wanaopenda kutembelea eneo linaloweza kufananishwa na makumbusho ya wazi ( Open Museum).
Msanii wetu mtanzania alitumia fursa kama hiyo ya mandhari ya kipekee ya historia ya Ugiriki na kutengeneza wimbo wake ambao pia kiaina umefanikiwa kutangaza mandhari zilizotunzwa kwa mamia ya miaka na kuwa sehemu inayovutia watalii kwa mamia kutembelea Greece kutokana na upekee wa eneo hilo linalobebwa kihistoria na kitalii .
MAONO YA MH. RAIS, ZIARA YAKE KUITANGAZA KUPITIA TANZANIA ROYAL TOUR