Kufukuzwa kwa Gamondi shida ilianzia kuibukia kwenye mkutano mkuu wa Yanga na kutangazwa akitokea Club kula Bata

Kufukuzwa kwa Gamondi shida ilianzia kuibukia kwenye mkutano mkuu wa Yanga na kutangazwa akitokea Club kula Bata

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mapema mwezi Juni Yanga walifanya Mkutano Mkuu na hapo ndipo walimtangaza Miguel Ángel Gamondi kuwa ameongeza mkataba wa mwaka mmoja na kutokana na mafanikio yake na Wananchi ya msimu wa 2023/24 basi walikuja na msemo wa "TABU IKO PALE PALE" kutokana kuwatesa sana Watani zao Simba SC.

Soma, Pia: Rasmi: Yanga yavunja Mkataba na Gamondi

Kama surprise mbele ya Wanachama wa Yanga Gamondi alidai ametokea Club kwenye show ya Marioo baada ya kuulizwa na Rais wa Yanga, Eng. Hersi na ukumbi mzima ukaripuka kwa furaha bila kufikiria kuwa wanatengeneza tatizo.

Kwenye moja ya sababu za kutimuliwa Master Gamondi inadaiwa kuwa ni ishu ya kinidhamu ambayo ilipelekea kuwa na kundi la wachezaji ambao inaelezwa alikuwa anatoka nao kwenda kula bata.

Tatizo la kinidhamu waliendekeza wenyewe viongozi ila limeondoka na kibarua chake

Miguel Ángel Gamondi aliteuliwa kuwa kocha mkuu wa Yanga, akichukua nafasi ya Nasreddine Nabi. Aliongoza Yanga kushinda taji la Ligi Kuu ya Tanzania kwa mara ya 30 na kufikia robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.


Soma: Kocha Kheireddine Madoui wa CS Constantine kuchukua Mikoba ya Gamondi Jangwani
 
Mbona mnatoa sababu nyingi mara ivi mara vile,
Leteni basi sababu moja iliomtoa ile tuelewe nyie wachambuzi wakujitegemea.
 
Sababu nyingine na ya msingi ni yeye Gamond kukataa viongozi wasinunue mechi na madawa/sindano za kusisimua misuli ya wachezaji hasa pale timu inaposhambuliwa kwa sababu kocha alikataa hayo yote kwa sababu yanadhoofisha vipaji vya wachezaji
 
Sababu nyingine na ya msingi ni yeye Gamond kukataa viongozi wasinunue mechi na madawa/sindano za kusisimua misuli ya wachezaji hasa pale timu inaposhambuliwa kwa sababu kocha alikataa hayo yote kwa sababu yanadhoofisha vipaji vya wachezaji
Hahaha ila bangi mbaya sana, kwahiyo sindano zinapigwa wakati timu inashambuliwa?
 
Sababu nyingine na ya msingi ni yeye Gamond kukataa viongozi wasinunue mechi na madawa/sindano za kusisimua misuli ya wachezaji hasa pale timu inaposhambuliwa kwa sababu kocha alikataa hayo yote kwa sababu yanadhoofisha vipaji vya wachezaji
wewe ndo huwa unatumwa kupeleka hivyo vitu? Ukitakiwa kupeleka ushahidi wa dhahiri uta kua nao? Acha kuropoka vitu visivyo na maana. Usitumie bando, kifaa na muda vibaya.
 
Ile ya Aziz ki nz shisha pia niliiona, nanikajua ipo shida smwhr, kocha amepoteza heshima kwa wachezaji koz hez doing the same!
 
Binafsi naunga mkono kutimuliwa kwake. Kocha unaposhindwa kudhibiti nidhamu ya timu, tayari unakuwa umepoteza sifa ya kuiongoza hiyo timu.
 
Back
Top Bottom