Kufungua kampuni ya kuagiza bidhaa

Africa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2015
Posts
1,504
Reaction score
2,272
Habari za jioni wakuu!

Naomba niulize moja kwa moja hili swali ili niweze kupata majibu na mchanganuo kwa kina.

Ni hivi......

Je, ninaweza kufungua kampuni kwa ajili ya kumwagizia mteja vitu, vifaa, au kuwaletea chochote wanachohitaji kutoka nje ya nchi na kumkabidhi mteja mkononi?

Kama ni ndiyo, ni hatua zipi nianze nazo?
 
Tafuta lawyers
 
Nimekuelewa vyema mkuu, tovuti na app unanisaidiaje kuipata gharama zake zikoje? Vipi kuhusu sheria za nchi maana nataka niwe na ofisi rasmi.
 
Karibu, tunaweza kulifanya hili
Cell: 0777777766
Email: info@afrolink.co.tz
 
Gharama za kumsaidia mtu kufungua kampuni zikoje,? Iwe limited zinakuaje?
1. Gharama za Consultation inategemea kutokana na Mtaji unaosajili. Gharama zetu ni kati ya TZS. 150,000 hadi TZS. 250,000 kwa kampuni yenye ukomo.
Note
A: Gharama za BRELA atalipa mteja mwenyewe ila ataambiwa
B: Gharama za Consultation ni VAT EXCLUSIVE hapo

2. Consulatation fee
Kwa maongezi ya ushauri ni TZS. 20,000
Waweza kuja ofisini au online (simu, whatsapp, email, et al)
 
Mkuu idea yangu ndio hiyo, unanisaidiaje kufungua kampuni, cost zake mpka kukamilisha vibali vyote?
Idea yako ni nzuri. Ila hadi kufikia lengo lako la kampuni kusimama kuna hatua. Kwa kifupi hatua zake ni:

1. Sajili kampuni yenye ukomo -BRELA
Hapa ina maana utatakiwa kusajili/kusajiliwa kampuni ambapo wanahisa mtatakiwa kuanzia 2 hadi 50. Gharama zake inategemea na MTAJI kwani kwa gharama za BRELA ni kuanzia TZS. 167,200 hadi TZS. 512,200
Biashara utakazo kufanya zitaandikwa ktk MEMARTS

2. TIN ya kampuni -TRA
Ukikamilisha usajili wa kampn hatua ya pili ni kupata TIN ya kampuni ambayo itakusaidia kulipia kodi na mojawapo ya uhalali wa kampuni na biashara unazofanya kuwa halali

3. Vibali
Kama ni biashara itakayohitaji vibali maalumu itakubidi kukata then ndo upewe leseni. Mkuu nimerejea pale juu ulipoandika. Biashara unayotaka kufanya ni ya 'corrier' ada zake zipo ktk ukurasa wa TCRA pitia. Ila jipange gharama kidogo. Ukipata kibali hk ndo utapata leseni

4. LESENI
Hapa inategemea na biashara unayofanya. Kama biashara za zinazogusia sera ya Taifa utalazimika kulipia leseni wizara ya viwanda biashara uwekezaji upande wa BRELA au ktk manispaa husika ya eneo lako

5. Gharama kwa ujumla wake
Siwezi kusema TSHS ngapi exactly kwa sababu taasisi mbalimbali zinahusika. Huu ninmwaka mpya wa fedha hivyo kuna mabadiliko ya hapa na pale

Regards
 
Kuanza huu mchakato nategemea ushirikiano kutoka kwako, nikijua A-Z tutafanya kazi
 
Nimekwama mkuu, sijajua bado gharama ya kibali kutoka TCRA Ni kiasi gani, na kule viwanda na biashara nako sijafanikiwa kuona nitalipia Tzs ngapi!

Hapa ndio kwenye changamoto!
Sometimes docs utakazo wasilisha hutoa makadirio ya gharama halisi za kulipa. Hivyo km ulishaanza na docs unazo ungewasilisha maombi rasmi
 
Mkuu kutengeneza website na app mfano wa Alibaba au eBay ni Tzs ngapi unatoza?
Waweza wasiliana nami kwa namba hii +255-657-685-268

Kupata makadirio ya ada ya kazi

Kwa sheria
- fungua kampuni
- jisajiri tcra
- lipia leseni zinazotakiwa

Your done
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…