Kufungwa kwa biashara Kariakoo, ni aibu kwa Serikali

Kufungwa kwa biashara Kariakoo, ni aibu kwa Serikali

Magufuli 05

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2023
Posts
1,433
Reaction score
2,791
Sina kumbukumbu sahihi kuwa ni lini wafanyabiashara wa Kariakoo wamewahi kugoma kwasasabu yoyote. Kariakoo ndiyo Dubai ya nchi yetu, ina wafanyabiashara wa kila aina, wakiwemo wenye mitaji mikubwa, ya kati na midogo.

Kikubwa zaidi wanajitambua, naamini hawawezi tu wakakurupuka kugoma bila kuvumilia na kufika mwisho. Hapa ni kwamba tatizo hili limeanza zamani, wamejitahidi kwa namna moja ama nyingine kuihusisha serikali lakini imeshindikana.

Lakini kilicho nisikitisha zaidi ni madai yao kwamba Bandarini kuna urasimu. Daaa, aibu iliyoje, kama ni kweli kuna urasimu kwenye lango kuu la uchumi na biashara za nchi yetu, tunakwenda wapi? Nchi nyingine zinatamani kuwa na bandari kama yetu tu, ili ziweze kulisha Afrika yote, sisi kuna urasimu?

Tunakwenda wapi, mbona hatukuyaona haya awamu ya tano? Rais JPM aliweka macho yote pale,mambo yalikuwa shwari, mbona ghafla hivi? Changamoto wanazopitia wafanyabiashara wa kariakoo ndiyo hizo wanapitia wafanyabiashara nchi nzima.

Serikali hii ni sikivu kweli?
Serikali hii ina nia ya dhati kweli?
Serikali hii mbona mambo yapo vululu valala kiasi hiki?
Nchi hii tunaipeleka wapi?

Mungu isaidie na Watanzania amkeni. Wakati ni sasa wakujenga nchi yetu kwa kuondoa wasioweza kuongoza na kuchagua wale wenye dhamira ya kweli.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Naamini Kariakoo ndio soko linaloongoza kwa ukusanyaji wa mapato kwa siku, hapo lazima kuna kiasi kikubwa cha pesa kimepotea, anyway, kama ambavyo CAG anatuonesha kila mwaka tunavyopoteza mapesa kwenye kila sekta, ndio tabia yetu.
 
Mwenye data za containers za wafanyabiashara zinazoingia banadarini kila mwezi atujuze hapa ili twende sawa

Hizo storage za badhaa ndio zinalengwa hapo na kama wana nia ya dhati waonyeshe tu ila mapato yakusanywe kwa uhalali
Na kama hao wakusanyaji wamenyimwa rushwa na kuamua kulipua haya basi tujue pia
 
Hakuna mkono wa Silent Ocean hapa? Nimesikia wakisema huko kijiweni, kuwa kwasasa, ama uwatumie wao au uundiwe zengwe. Wanasema, dini imekuwa mwamvuli sasa!

Inawezekana hili la storage likawa ni zengwe pia kama wasemavyo kijiweni?
 
Afadhali awamu hii watu wanaweza kugoma na kuongea wazi wazi kuhusu matatizo yao kwenye vyombo vya habari, wakati wa dikteta magufuli saa hii ungekuta mabomu yanarushwa Kariakoo. Tunashukuru Mungu kwa uhuru wetu kurudi!
 
Back
Top Bottom