KUFUNGWA KWA SIMBA NA RAJA SIYO BAHATI MBAYA NI UWEZO.

KUFUNGWA KWA SIMBA NA RAJA SIYO BAHATI MBAYA NI UWEZO.

MLA PANYA SWANGA

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2015
Posts
5,184
Reaction score
5,435
Nitoe Pole kwa wanasimba wenzangu kwa kichapo tulichopokea jana nyumbani.
Ni wazi mpira ulichezwa vizuri na timu zote mbili kwa ufundi mkubwa. Wachezaji wa simba pamoja na kufungwa walionyesha uwezo wao na kasoro zao pia.

Ukweli mchungu ni kuwa Raja wamewekeza na wamekamilika idara zote kwa gharama kubwa. Timu hii ipo afrika lakini inaweza ikaingia ligi kuu ktk nchi yoyote duniani na ikamaliza top 7 kama kila kitu kitabaki sawasawa.

Hii ndiyo timu iliyovunja mwiko wa simba iliyoshindwa kukamilika baadhi ya idara kwasababu ya pesa. Lakini kufungwa kwa simba hakuifanyi simba iwe mbovu.Nampongeza mwekezaji MO kwa maono yake bado atafika mbali sana.

Ushauri wangu kwa sasa namuona kocha wetu mkuu amepwaya sana. Timu aachiwe mgunda amalizie mechi zilizosalia nafasi ya pili INAWEZEKANA.

SIMBA NGUVU MOJA.
 
Tatizo la Simba sio kocha kwa sasa, tatizo ni wachezaji viwango vyao ni vibovu. Huwezi kupima uwezo wa kocha kama wachezaji hawaeleweki viwango vyao. Cha msingi kocha avumiliwe mpaka mwisho wa msimu kisha aletewe wachezaji wenye uwezo mkubwa.
 
Back
Top Bottom