Kulwa Jilala
JF-Expert Member
- Sep 6, 2022
- 3,891
- 8,448
Pori tengefu la Msomera mkoani Tanga limefutwa rasmi na Serikali na sasa litapangiwa matumizi mengine ikiwemo kuwapa wamasai wanaohamishiwa kutoka Mbugani ambako wamefurushwa ili kumpisha mwarabu ajenge mahoteli.
Kinachoshangaza zaidi ni watu waliojitanabaisha kuwa ni watetezi wa mazingira kukaa kimya bila kupinga kwa pori hili ambalo limekuwa chanzo cha maji kwa muda mrefu.
Wakati ulipotangazwa ujenzi wa bwawa la kufua umeme la Mwl. Nyerere mara moja watetezi wa mazingira kutoka ndani na nje ya nchi waliibuka na kupinga ujenzi huo kwa sababu utasababisha uharibifu mkubwa wa mazingira.
Je, kufuta pori tengefu la Msomera siyo uharibu wa mazingira ila ujenzi wa bwawa ni uharibifu wa mazingira?
Kinachoshangaza zaidi ni watu waliojitanabaisha kuwa ni watetezi wa mazingira kukaa kimya bila kupinga kwa pori hili ambalo limekuwa chanzo cha maji kwa muda mrefu.
Wakati ulipotangazwa ujenzi wa bwawa la kufua umeme la Mwl. Nyerere mara moja watetezi wa mazingira kutoka ndani na nje ya nchi waliibuka na kupinga ujenzi huo kwa sababu utasababisha uharibifu mkubwa wa mazingira.
Je, kufuta pori tengefu la Msomera siyo uharibu wa mazingira ila ujenzi wa bwawa ni uharibifu wa mazingira?