Kuhudumia Mwanaume Kabla ya Kuoana.

kuna kitu mnatoa hata?unakuta mdada ana kazi yake ila anaishi tu na mwanaume bila ndoa matumizi anaafford naona ni maadili tu kushnei

Sasa hapa tatizo ni la mwanamke au mwanaume? Kama una kazi na matumizi una afford nini kinakuhamisha kwako kwenda kwa mwanaume ambaye haujafunga naye ndoa? Sasa kama mtu anaweza kununua maziwa na nyama ya ngombe kwa wakati anaotaka yeye kwa nini aingilie kazi za wamasai za ufugaji?
 

Nimekosa ile sehemu ya kukujulisha kuwa ninakubaliana na mtazamo wako.
 
sio kwamba wamama wana matatizo sema la life cycle inachangia mama kushindwa kumudu majukumu ya nyumbani mfano mama unatakiwa kazini saa moja na nusu na upo dar inamaana unatakiwa uondoke home saa kumi na moja na kurudi umewai sana saa 2 sasa hapo majukumu yanaenda kwa housgirl ndo maana mimi sidhani kama mwanaume ananioa ili nimfanyie kazi za nyumbani na siwezi kuishi na mwanaume eti nimsaidie kazi za home atafute mtumishi.mimi nikiishi nae ni mambo mengine maana automatically kama lengo lake ni kumfanyia kazi za nyumbani,naeza kushindwa kuzifanya sio kwamba sipendi ila ni kutokana na situation tu ya maisha
 
..sasa huduma hizo zinakuwa two way trafic, wewe utapika pakua fua sijui nini, mwisho wa siku utaniambia nna shida ya laki.... nataka ku..... mzee natoa so haina shida wote tunatumikiana sio bure kabisaaaaaaaaaaa
 
Nimecheka sana, hata kufua?

We cheka tu my dear lakini kuna vituko wewe acha tu! Haya malezi ya siku hizi.... unaweza kutana na mzigo hadi ushangae...
 
imeandikwa mwanamke atamwacha baba yake na mama yake nae ataambatana na mume wake nao watakuwa si wawili tena bali mwili mmoja so kila mtu asubiri wakati wake aambatane na mwenzake alietoka kwa bwana tuache uzinzi usiokuwa wa maana
 

Binafsi sikatai kwani wengine wako busy kuliko waume zao....hilo linajulikana. Lakini wapo wengine ni akina mama wa nyumbani lakini hajui hata maji ya kunywa yanachemshwaje.. kila kitu house girl...ndo maana akina baba wasio wavumilivu hufikia mahali pa kuwapandisha madaraja hao ma hausegirl na some of them wamefikia hatua ya kuwapindua waajiri wao. Kwa asili na hata huko ulauya walikoendelea zaidi yetu haya ndio majukumu ya kimsingi ya kina mama.... Bebii ukiteleza hapo ndoa umeiweka rehani!
 
sasa tutafanyeje na mafoleni tuwai kupika jamani?nitakuchukulia chips kuku movenpick eeeeeeeeeeh
 
imeandikwa mwanamke atamwacha baba yake na mama yake nae ataambatana na mume wake nao watakuwa si wawili tena bali mwili mmoja so kila mtu asubiri wakati wake aambatane na mwenzake alietoka kwa bwana tuache uzinzi usiokuwa wa maana

Kama ni hilo la kutokuonjana kabla, Kwakuwa dini yangu inakataza kuzini na uzinzi nami nakubaliana nawe lakini tuje kwenye ukweli wa maisha tuliyo nayo... Nani anaweza? Wewe uliweza? Tuwe wakweli tuishi kwa vitendo sio kwa nadharia.
 
Sasa ntjuaje kuwa unaweza kukpika, kufua nk?

Kama una uhusiano "mwema" na huyo binti, siyo lazima aje kwako kukupikia na kukufulia. Kuna namna nyingi ya kujua kama aweza kupika na kufua.

Itakapofikia ukakaribishwa kutambulishwa rasmi kwao, maana usasa na mambo ya kileo siyo ajabu kutambulishwa kwao msichana.Utakapokaribishwa basi yale maandalizi yatakupa picha. Usafi wa msichana mavazi yake na mambo mengine yatakupa dalili hata kama ni minimum utakazoweza kuja kuzinoa zaidi lol.

Ukiacha hayo hapo juu, basi kama msichana ni rafiki yako na una nia naye basi akija kwako au wewe ukaenda kwake mnaweza kusaidiana kupika, kusafisha nyumba na hata kufua. Usitake wewe kumgeuza msichana kuwa "mke" wakati bado muda haujafika na hujakamilisha taratibu.
 
sasa tutafanyeje na mafoleni tuwai kupika jamani?nitakuchukulia chips kuku movenpick eeeeeeeeeeh

Chipsi kuku kila siku bebiii? oteeeeee! Hata wikiendi jamani... ah mi usiponipikia hata nikila huo msosi basi tu siamini nakula kitu safi na salama.... Nitakumezea tu weekdays ila isiwe tuu much!
 
Kama ni hilo la kutokuonjana kabla, Kwakuwa dini yangu inakataza kuzini na uzinzi nami nakubaliana nawe lakini tuje kwenye ukweli wa maisha tuliyo nayo... Nani anaweza? Wewe uliweza? Tuwe wakweli tuishi kwa vitendo sio kwa nadharia.
kuonja/ kuonjeshwa/ kuonjeshana ni tofauti na kuhamia sasa msichana utawaambia wazazi na ndugu unaishi wapi?
 
Kutokana na wasichana wengi kutoa mimba "ovyo ovyo" sio mbaya mkapata mtoto halafu ndoa,ili ujue kama anazaa au vipi,
 
Chipsi kuku kila siku bebiii? oteeeeee! Hata wikiendi jamani... ah mi usiponipikia hata nikila huo msosi basi tu siamini nakula kitu safi na salama.... Nitakumezea tu weekdays ila isiwe tuu much!
siku niko off na wkend nitapika na kufanya kila kitu hata siku nimewai ila msaidizi kwangu ni muhimu sitaweza kufanya shughuli zote especially wkdays.
 

Kusaidiana sikatai kwani binafsi nikiingia jikoni utapenda.... Lakini kuangalia tu usafi wa mavazi yake huyu binti si anaweza kuwa hayo mavazi yake naye anafuliwa? Na msosi kapika mama yake au Housegirl wao?
 
Kusaidiana sikatai kwani binafsi nikiingia jikoni utapenda.... Lakini kuangalia tu usafi wa mavazi yake huyu binti si anaweza kuwa hayo mavazi yake naye anafuliwa? Na msosi kapika mama yake au Housegirl wao?

Kumbe kazi wazijua weye, sasa unataka aje akupikie na kukufualia ya nini? Utamfundisha endapo bahati mbaya hajui.
 
kuonja/ kuonjeshwa/ kuonjeshana ni tofauti na kuhamia sasa msichana utawaambia wazazi na ndugu unaishi wapi?

Hapa nilikuwa najibu hoja yako "Tuache uzinzi jamani"..... ila pia simaanishi kuwa lazima uje huamie kwangu.... unakuja wikiendi unapika, unafua halafu tunananilihii then unarudi kwenu..... ni then ukifuzu katika hayo maeneo matatu naleta mahari!
 
Na nyie huwa mwafuata nini kwenye mageto ya hawa mabachela. Tena huwa mnajioza wenyewe. Utasikia tu: "Wikiendi hii ntalala kwa mme wangu". Sasa kama huyo ni mmeo usilalamike kufanya majukumu ya mke, si umeshajioza..!
 
Ni kama vile wanatufanyia Interview! hapo hujanipata. Hayo nitafanya ukinivisha pete wangu. kama inakushindaa kwaheri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…