Kuhusu Corona, Serikali isiturudishe nyuma

Kuhusu Corona, Serikali isiturudishe nyuma

MenukaJr

Member
Joined
Apr 24, 2021
Posts
50
Reaction score
128
Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Serikali iliyotolewa tarehe 05 June, 2021 imebainisha kwamba Rais wa JMT amepokea tayari taarifa mbili kutoka katika Kamati aliyoiunda kwa ajili ya kufuatilia na kuishauri Serikali namna ya kupambana na gonjwa la corona. Taarifa ya kwanza ilikua ni yenye maoni ya namna Serikali inavyoweza kupambana na corona na taarifa ya pili inahusu namna ambavyo Serikali inaweza kupata rasilimali (nadhani fedha) kwa ajili ya kupambana na corona.

Kwa mantiki ya kawaida, taarifa ya pili ya Kamati imeamua tayari msimamo wa Serikali juu ya corona. Kwa kawaida huwezi kufikiria kutafuta fedha kwa jambo ambalo bado kulifanyia uamuzi. Kwa hiyo, taarifa ya kwamba Baraza la Mawaziri litaketi hivi karibuni kuamua iwapo Serikali ikubaliane na chanjo au la ni ya uongo (danganya toto). Ukweli Serikali itakua tayari imeamua kuruhusu chanjo ndio maana imeagiza Kamati kupendekeza namna ya kupata fedha kwa ajili ya kununulia na kusambaza chanjo. Ndiyo maana pia imeruhusu Watanzania wenye kufanya kazi katika mashirika na taasisi za nje hapa nchini kuchanjwa.

Kwa sababu hiyo, kama Mwananchi mwenye HAKI ya kutoa maoni kwa mujibu wa Katiba, kama raia mwenye kuhusika na chanjo hiyo moja kwa moja, kwa ajili ya kumbukumbu natoa maoni yangu binafsi kwa Serikali kuelekea kikao cha Baraza la Mawaziri la uamuzi.

1. Kabla ya kuamua kutangaza kuleta chanjo Serikali itambue kuwa chanjo ya corona haizuii maambukizi ya corona wala haiondoi masharti ya kujikinga na corona kwa uzoefu wa taarifa zilizopo. Taarifa zinasema mwenye kuchanjwa anaweza kuambukizwa sawa na asiyechanjwa. Tutafakari umhimu wake kulinganisha na madhara ya corona katika nchi yetu tusije kurudi nyuma.

2. Kabla ya kuamua kutangaza kuleta chanjo, Serikali itambue kuwa chanjo ya corona ni biashara ya Mataifa yenye nguvu. Kwa vyovyote ili tuhimili gharama za chanjo itatupasa kukopa pesa zaidi kwao pamoja na mashirika ya fedha Duniani. Hadi sasa nchi yetu inadaiwa zaidi ya Tshs. 60 trioni. Hiki ni kiasi cha juu ukilinganisha na mahitaji ya pesa yaliyopo ili kugharamia miradi ya maendeleo. Kama hatukuwa makini, tunaweza kukopa pesa nyingi kwa ajili ya corona na kulifanya deni letu kuwa kubwa zaidi lisilohimilika au kushindwa kukamilisha miradi yetu ya maendeleo, tutarudi nyuma.

3. Kabla ya kuamua kutangaza kuleta chanjo, Serikali itambue kuwa nchi yetu haina uwezo wa kuchanja hata theluthi moja ya watu wake kwa miaka mingi zaidi. Mathalani, tangu February mwaka huu nchi ya Afrika Kusini imechanja watu 481k tu sawa na wastani wa watu 160k kwa mwezi. Kwa takwimu hii, itawahitaji miaka 30 kuwachanja watu wake wote. Idadi ya Wa-South Africa haitofautiani sana na sisi. Swali la kujiuliza, tunawezaje kuchukua jitihada za kukinga watu wetu ili tuikamilishe miaka 30 ijayo. Kati ya sasa na wakati huo tutakua tumepoteza watu wangapi (kama kweli tatizo lipo), tutakua tumepoteza pesa kiasi gani. Kwa vyovyote vile njia hii haiwezi kuwa na maana yoyote zaidi ya upotevu wa pesa.

4. Kabla ya kutangaza kuleta chanjo, Serikali yetu itambue kuwa kwa sasa corona sio tishio tena Duniani na kwa sababu hiyo isifanye uamuzi under a such serious tension. Tunaweza kulichukua jambo hili kwa taratibu wakati namna bora na rahisi zaidi zikiendelea kuvumbuliwa. Nchi nyingi (kama sio zote) zimefungulia watu wake kuendelea na shughuli zao kama kawaida, zimeanza kuipuuza corona. Nimeangalia fainali za Kombe la Ulaya (UEFA) mashabiki wameruhusiwa kuingia uwanjani, hata sasa mechi za kirafiki za FIFA mashabiki wanaingia uwanjani wengine wamevaa barakoa wengine hawakuvaa, hii ina maana moja tu kubwa; tunaweza kuishi na corona. Hatua hii sisi tuliipita muda mrefu na JPM hatupaswi kurudi nyuma na Samia Suluhu.

5. Kabla ya kutangaza kuleta chanjo, Serikali itambue endapo ni lazima iruhusu chanjo kufuata Itifaki ya Dunia inaweza kutumia njia mbili; MOSI. Iombe kupata chanjo za corona bila gharama (free of charge). PILI. Iruhusu wenye kutaka kuchanja (kwa ajili ya safari nk.) watafute chanjo kokote wachanje nje ya gharama za Serikali ikiwa ni lazima kufanya hivyo. Kusudi la njia hizi ni kuiondoa Serikali katika gharama zisizo na lazima.

HITIMISHO. Dunia inacheza kamari katika tatizo hili la corona. Kwa kawaida kwenye kamari wajinga ndio wenye kuliwa nyingi.Tanzania tumepiga hatua kubwa katika mapambano dhidi ya corona, tumelipa gharama yake kuliko nchi yoyote katika Dunia hii kwa vyovyote hatupaswi kulipa gharama kwa mara nyingine tena kwa ajili ya chanjo. Watanzania badala ya ku-sign petition ili Diamond asishinde BET tunaweza ku-sign petition kupinga matumizi ya fedha zetu kwa ajili ya chanjo, inaweza kutuheshimisha!

#TutakukumbukaDaimaJPM.

MenukaJr,
Da'slama-Tanzania.
 
We endelea kumkumbuka dikteta kichaa, chanjo itakuja, na atakae taka atachomwa.

Nyi wasukuma endeleeni kupiga nyungu Kama mlivyoelekezwa na mungu wenu kichaa dikteta.
 
Mwenye kuchanjwa anaweza kupata tena Corona, jibu ni ndiyo kadri ya Tafiti, ila akipata tena haina tena madhara kwake ila anaweza kumuambukiza mtu mwingine na ikamletea shida.

Mtu akiugua mafua atapona na anaweza kumuambukiza mwenzake na mafua atapata lakini kwa sababu tumeshajijengea kinga, hayatudhuru chochote. Nimejaribu kutoa maoni kadri ya hoja namba 1 ulivyoiwasilisha.
 
We endelea kumkumbuka dikteta kichaa, chanjo itakuja, na atakae taka atachomwa,

Nyi wasukuma endeleeni kupiga nyungu Kama mlivyoelekezwa na mungu wenu kichaa dikteta.
Hizi elements za ethnic accusations and labelling kama hatutazikemea kwa pamoja ipo siku kama taifa tutazilipia with premium tears
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Madakatari wanaotibu wagonjwa wenye korona wanataka wachanjwe ili wawe salama halafu wewe unaleta habari za kizushi!
Matope kabisa kwa akili yako ukichanjwa huambukizwi corona? Huko walikoanzia kuchanjwa lockdown za nini? mbona maambukizi yanaibuka upya?

kama hujui kitu nyamaza kuliko kuleta ujuaji wa simba na yanga.
 
Matope kabisa kwa akili yako ukichanjwa huambukizwi corona? Huko walikoanzia kuchanjwa lockdown za nini? mbona maambukizi yanaibuka upya?
kama hujui kitu nyamaza kuliko kuleta ujuaji wa simba na yanga.
Ukichanjwa unaweza kupata virusi vya Korona tena lakini vinakuwa havina madhara tena maana mwili unakuwa unaweza kuvimudu bila wasiwasi
 
Matope kabisa kwa akili yako ukichanjwa huambukizwi corona? Huko walikoanzia kuchanjwa lockdown za nini? mbona maambukizi yanaibuka upya?
kama hujui kitu nyamaza kuliko kuleta ujuaji wa simba na yanga.
Dikteta mwehu aliiletea kiburi Covid19,
Kilichompata imebakia historia, hakuna Tena mwehu Kama yeye wakuivimbia sayansi, nyie vichaa wenzie endeleeni kumuenzi
 
Ivi Hawa wapuuzi wanashindwa kufahamu kwanini mama na team nzima serikalini wapo makini juu ya covid-19, wanafahamu kuwa yule majinuni covid19 imelalanae mbele, kwaiyo lazima na wao wachukue tahadhali,na pia wananchi must wawe makini pia,
 
Kama unaona unarudishwa nyuma tangulia mbele ya haki kwa mwendazake umwache mama apige kazi...kila zama na kitabu chake 🤣
 
  • Kicheko
Reactions: BAK
Viongozi wa Afrika wanaua na kuangamiza nchi zao kwa sababu ya kutojiamini na kuogopa wazungu.

Ugonjwa wa Corona haukuwa ugonjwa wa kupewa kipaumbele Afrika. Fikiria hapo Afrika vifo havizidi laki mbili,wakati Mabara mengine vifo 3.76 milioni. Huko wazungu ndo walitakiwa kuchunguza kwanini Waafrika hawajafa wengi pamoja na maisha ya kulala chumba kimoja watu kumi,na wao na uchache wao ndo wanateketea.

kwa kujua Afrika hawana akili tunalazimishwa tuamini janga la wazungu ndo janga la dunia,na janga la Afrika kama UKIMWI na Malaria siyo janga la dunia.

Tanzania ni nchi pekee ambayo watu wake hawakuchanjwa na maisha yao yanaendelea kama kawaida,daladala zimesheheni,watoto shuleni wanakanyagana,na corona tunaiona ni mafua ya kawaida.

Sasa viongozi wanafanya vyitu vya kushangaza sana. Wanataka mkopo wa emergency kupambana na corona, yaani mko tayari kuanza kutangaza visa ili tu mpate pesa.Je huo mkopo utawasaidia kwa miaka mingapi? Maana ni zaidi ya mwaka sasa tangu corona iingie.

ushauri. Acheni tuishi maisha haya maana hatukupungukiwa na kitu,maana hata majirani zetu waliochanjwa visa vinaongezeka,vifo kama kawaida mara lockdown.
Kinawauma nini viongozi mkiona tunaishi bila hofu?
je nchi haitaendelea kwa kukosa mkopo huo?
Ama mna maslahi gani.
Sasa hivyi mnaweza kutufanyia vyovyote mtakavyo huko mbele mtajutia sana maamuzi yenu.
 
Ulichosema ni sawa kabisa Mkuu. Aliye pats chanjo anaweza kabisa kupata COVID-19 lakini katakuwa ni kagonjwa kadogo tu hakahitaji hata kulazwa, isipokuwa wale wenye matatizo makubwa ya kiafya inaweza kuwa ni ugonjwa mkubwa wa kulazwa na hata kufa. Mara ya mwisho niliisikia watu 74 waliopata chanjo zote mbili za Pfizer walikufa baada ya kupata ugonjwa huo. Na hii habari Pfizer waliithibitisha.
Mwenye kuchanjwa anaweza kupata tena Corona, jibu ni ndiyo kadri ya Tafiti, ila akipata tena haina tena madhara kwake ila anaweza kumuambukiza mtu mwingine na ikamletea shida.

Mtu akiugua mafua atapona na anaweza kumuambukiza mwenzake na mafua atapata lakini kwa sababu tumeshajijengea kinga, hayatudhuru chochote. Nimejaribu kutoa maoni kadri ya hoja namba 1 ulivyoiwasilisha.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Dikteta mwehu aliiletea kiburi Covid19,
Kilichompata imebakia historia, hakuna Tena mwehu Kama yeye wakuivimbia sayansi, nyie vichaa wenzie endeleeni kumuenzi
Ok Mwendazake kafa huko Ulaya kwa babu zako wamekufa wangapi?
je wewe utaishi milele kwa kuwa ni mwema sana kuliko JPM?
siye wewe utakaye kufa kwa ugonjwa mbaya sana na kuijutia tabia hii ya kufurahia mauti ya wengine?
 
Ak
Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Serikali iliyotolewa tarehe 05 June, 2021 imebainisha kwamba Rais wa JMT amepokea tayari taarifa mbili kutoka katika Kamati aliyoiunda kwa ajili ya kufuatilia na kuishauri Serikali namna ya kupambana na gonjwa la corona. Taarifa ya kwanza ilikua ni yenye maoni ya namna Serikali inavyoweza kupambana na corona na taarifa ya pili inahusu namna ambavyo Serikali inaweza kupata rasilimali (nadhani fedha) kwa ajili ya kupambana na corona.

Kwa mantiki ya kawaida, taarifa ya pili ya Kamati imeamua tayari msimamo wa Serikali juu ya corona. Kwa kawaida huwezi kufikiria kutafuta fedha kwa jambo ambalo bado kulifanyia uamuzi. Kwa hiyo, taarifa ya kwamba Baraza la Mawaziri litaketi hivi karibuni kuamua iwapo Serikali ikubaliane na chanjo au la ni ya uongo (danganya toto). Ukweli Serikali itakua tayari imeamua kuruhusu chanjo ndio maana imeagiza Kamati kupendekeza namna ya kupata fedha kwa ajili ya kununulia na kusambaza chanjo. Ndiyo maana pia imeruhusu Watanzania wenye kufanya kazi katika mashirika na taasisi za nje hapa nchini kuchanjwa.

Kwa sababu hiyo, kama Mwananchi mwenye HAKI ya kutoa maoni kwa mujibu wa Katiba, kama raia mwenye kuhusika na chanjo hiyo moja kwa moja, kwa ajili ya kumbukumbu natoa maoni yangu binafsi kwa Serikali kuelekea kikao cha Baraza la Mawaziri la uamuzi.

1. Kabla ya kuamua kutangaza kuleta chanjo Serikali itambue kuwa chanjo ya corona haizuii maambukizi ya corona wala haiondoi masharti ya kujikinga na corona kwa uzoefu wa taarifa zilizopo. Taarifa zinasema mwenye kuchanjwa anaweza kuambukizwa sawa na asiyechanjwa. Tutafakari umhimu wake kulinganisha na madhara ya corona katika nchi yetu tusije kurudi nyuma.

2. Kabla ya kuamua kutangaza kuleta chanjo, Serikali itambue kuwa chanjo ya corona ni biashara ya Mataifa yenye nguvu. Kwa vyovyote ili tuhimili gharama za chanjo itatupasa kukopa pesa zaidi kwao pamoja na mashirika ya fedha Duniani. Hadi sasa nchi yetu inadaiwa zaidi ya Tshs. 60 trioni. Hiki ni kiasi cha juu ukilinganisha na mahitaji ya pesa yaliyopo ili kugharamia miradi ya maendeleo. Kama hatukuwa makini, tunaweza kukopa pesa nyingi kwa ajili ya corona na kulifanya deni letu kuwa kubwa zaidi lisilohimilika au kushindwa kukamilisha miradi yetu ya maendeleo, tutarudi nyuma.

3. Kabla ya kuamua kutangaza kuleta chanjo, Serikali itambue kuwa nchi yetu haina uwezo wa kuchanja hata theluthi moja ya watu wake kwa miaka mingi zaidi. Mathalani, tangu February mwaka huu nchi ya Afrika Kusini imechanja watu 481k tu sawa na wastani wa watu 160k kwa mwezi. Kwa takwimu hii, itawahitaji miaka 30 kuwachanja watu wake wote. Idadi ya Wa-South Africa haitofautiani sana na sisi. Swali la kujiuliza, tunawezaje kuchukua jitihada za kukinga watu wetu ili tuikamilishe miaka 30 ijayo. Kati ya sasa na wakati huo tutakua tumepoteza watu wangapi (kama kweli tatizo lipo), tutakua tumepoteza pesa kiasi gani. Kwa vyovyote vile njia hii haiwezi kuwa na maana yoyote zaidi ya upotevu wa pesa.

4. Kabla ya kutangaza kuleta chanjo, Serikali yetu itambue kuwa kwa sasa corona sio tishio tena Duniani na kwa sababu hiyo isifanye uamuzi under a such serious tension. Tunaweza kulichukua jambo hili kwa taratibu wakati namna bora na rahisi zaidi zikiendelea kuvumbuliwa. Nchi nyingi (kama sio zote) zimefungulia watu wake kuendelea na shughuli zao kama kawaida, zimeanza kuipuuza corona. Nimeangalia fainali za Kombe la Ulaya (UEFA) mashabiki wameruhusiwa kuingia uwanjani, hata sasa mechi za kirafiki za FIFA mashabiki wanaingia uwanjani wengine wamevaa barakoa wengine hawakuvaa, hii ina maana moja tu kubwa; tunaweza kuishi na corona. Hatua hii sisi tuliipita muda mrefu na JPM hatupaswi kurudi nyuma na Samia Suluhu.

5. Kabla ya kutangaza kuleta chanjo, Serikali itambue endapo ni lazima iruhusu chanjo kufuata Itifaki ya Dunia inaweza kutumia njia mbili; MOSI. Iombe kupata chanjo za corona bila gharama (free of charge). PILI. Iruhusu wenye kutaka kuchanja (kwa ajili ya safari nk.) watafute chanjo kokote wachanje nje ya gharama za Serikali ikiwa ni lazima kufanya hivyo. Kusudi la njia hizi ni kuiondoa Serikali katika gharama zisizo na lazima.

HITIMISHO. Dunia inacheza kamari katika tatizo hili la corona. Kwa kawaida kwenye kamari wajinga ndio wenye kuliwa nyingi.Tanzania tumepiga hatua kubwa katika mapambano dhidi ya corona, tumelipa gharama yake kuliko nchi yoyote katika Dunia hii kwa vyovyote hatupaswi kulipa gharama kwa mara nyingine tena kwa ajili ya chanjo. Watanzania badala ya ku-sign petition ili Diamond asishinde BET tunaweza ku-sign petition kupinga matumizi ya fedha zetu kwa ajili ya chanjo, inaweza kutuheshimisha!

#TutakukumbukaDaimaJPM.

MenukaJr,
Da'slama-Tanzania
Nakuunga mkono mara milioni!!
Wazungu walishaingia gharama ya kutengeneza chanjo na wanalazimisha kurudisha gharama zao!! Watatuona wajinga sana kama wakifanikiwa kutuingiza mkenge huo!! Tuna wasomi wazuri lakini waoga mno!! Wanasiasa waoga mno ! Viongozi wa dini waoga mno!! Mbona mko kimya japo dhamiri zenu zikishuhudia kuwa ukweli mnaujua!! Shame upon your faces!! Mungu bado atatuokoa na nyie atawabebesha mzigo mnaoustahili!
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Back
Top Bottom