Kuhusu deni la bodi ya mikopo (HESLB)

Kuhusu deni la bodi ya mikopo (HESLB)

Umkonto

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2018
Posts
2,652
Reaction score
4,593
Walibadilisha sheria ya makato kutoka 8% mpaka 15%. Mabadiliko haya yakawahusu hadi wale ambao walikuwa wanakatwa 8% katika mshahara. Wadau walipiga kelele lakini bodi hawakujali.

Sasa wameanza tena uhabaishaji wao kwa kuongeza makato (retention fee) kitu ambacho hakipo katika mikataba ambayo tulisaini miaka hiyo mfano mkataba wa bodi wa mwaka 2009.

Bodi wanatakiwa waheshimu mikataba tuliyosainishana, mfano mkataba wao wa mwaka 2009.

Bodi wakumbuke kuwa, mabadiliko yoyote hayapaswi kuwaathiri wale ambao tayari wamo katika makubaliano ya awali.

Kukaa kwetu kimya wasidhani tunaridhika na unyanyasaji wao. La hasha! tunasubiri muda tutapata haki yetu na kulipwa fidia kubwaaa.

Ni kwamba, nimeitunza nakala ya mkataba wa bodi niliousaini mwaka 2009.

Pia, kwa sasa, kila mwezi nadownload salary slip, nazi save kwenye mtandao, pia naziprint mpaka nitakapomaliza deni mwaka 2026.Salary slip ikiwa nyeupe, itakuwa ngumu kukubali makato mengine ya bodi, bodi wakilazimisha, itabidi kwenda mahakamani.

Kutokana na kuvunja mkataba, nimepanga kuwashitaki bodi ya mikopo hata kama ni mwaka 2040! Najua ipo siku mahakama itakuwa huru. Kwahiyo, chonde chonde bodi, jaribuni kufikiria future. Mtakuja kulipa fidia kubwa huko mbeleni.

Kwa sasa mmeshika mpini tumekaa kimya ila wengine tuna jambo letu, tunakusanya ushahidi. Cha ajabu, ikifika mwaka 2040 mahakama ikiamua tulipwe pesa ndefu kama fidia, wapo watakaotuona sisi siyo wazalendo, wakati leo tunavunjiwa mikataba, na wamekaa kimyaa.

Ushauri wa bure, bodi iombeni serikali hela ya kuwakopesha wanafunzi, mana ni jukumu la serikali kuwasomesha raia wake. Mnapotaka kujiendesha ndipo mnapoanza kutubambikia madeni, mwisho wa siku tunaishi maisha ya bila furaha.
 
Aisee man ni kweli mikataba ya bodi ya 2009 ukisoma vyema kuna loop holes kibao za bodi kusimamishwa kizimbani na kujibu hoja kwanini ni mandumilakwili.

Cha msingi ni raia kuamka na kukemea huu uonevu wa hawa wanyonyaji.
 
Aisee man ni kweli mikataba ya bodi ya 2009 ukisoma vyema kuna loop holes kibao za bodi kusimamishwa kizimbani na kujibu hoja kwanini ni mandumilakwili.

Cha msingi ni raia kuamka na kukemea huu uonevu wa hawa wanyonyaji.
Mkuu, kumbuka ammendments za wabunge wa bunge lako! Yawezekana mkasingizia bodi!
 
Mkuu, kumbuka ammendments za wabunge wa bunge lako! Yawezekana mkasingizia bodi!
Kiongozi yaani hata kama bunge lilifanya amendment bado lawana zitawaendea wote hasahas bodi kwa kukiuka mkataba ulio halali kabisaa.Kisheria kukiuka mkataba ni kosa.
 
Hapa inabidi kukaza,swala la bodi ya mikopo heslb ni hatari likifumbiwa macho.


"Mkija na mikuki tutakuja na risasi"
 
Watumishi wapunguziwe mzigo,kodi wanakatwa kubwa sana lakini mtumishi huyohuyo anajilipia pango,nauli,mawasiliano,umeme ,maji..... standing order kwa nchi yetu haina kazi kabisaaaa
 
Kiongozi yaani hata kama bunge lilifanya amendment bado lawana zitawaendea wote hasahas bodi kwa kukiuka mkataba ulio halali kabisaa.Kisheria kukiuka mkataba ni kosa.
Mkuu, narudia tena, sheria wanazozitumia zimepitishwa na bunge. Tukimwaga lawama zote kwao hatutawatendea haki.
 
Mkuu, narudia tena, sheria wanazozitumia zimepitishwa na bunge. Tukimwaga lawama zote kwao hatutawatendea haki.
Hata kama, lakini hiyo sheria haitakiwi kugusa substantive issues ambazo tayari zipo kwenye mkataba. Na ikitokea hivyo, hiyo sheria itakuwa haina mashiko kwenye mkataba. Hapa ndio sehemu pekee ya kwenda Mahakamani kutafuta tafsiri ya mkataba
 
Mkuu, narudia tena, sheria wanazozitumia zimepitishwa na bunge. Tukimwaga lawama zote kwao hatutawatendea haki.
Chief,je wao kama concerned body hawakuwa na weledi wa kushauri wakati wa kipindi cha utungaji wa hiyo sheri na kabla haijapitishwa au ndo walipiga kimya...at least basi wangejitutumua kuainisha mambo kidogo kwa bunge maana wao bodi ndo wenye dhamana ya kusimamia shughuli zao.
 
Watu wote wanaoumizwa na haya wanapaswa kupiga kelele na kujitetea kwa nguvu
Pole sana. Tatizo Afrika siasa ndio kila kitu na Rais ndio kila kitu kuliko hata siasa zenyewe.

Kila mtu yupo busy na mambo yake binafsi japo hili jambo linaumiza wengi.
 
Back
Top Bottom