Mkuu sijawahi kwenda kwa Bus ila nimekua Kigali several times..ni mji mzuri msafi sana..nimekua naenda na Rwanda Air..sehemu nzuri za kutembelea na nyama choma na bia ni Carwash..hilo ni eneo limetulia sana na jina linaitwa hivo hivo sijui kwanini..
Kingne hotel pale ni aghali sana nenda fikia Impala ni safi na salama ina internet na mambo yote ya kisasa dola 40 per nite.
Asante Mkuu, ningependa kwenda kwa barabara (basi) napata ku-explore mambo mengi. Sifahamu Impala itakuwa ni star ngapi, naweza kupata accommodation ya USD10 - 20, sihitaji sana mambo ya kisasa, nataka usalama tu. Kuhusu internet naweza kutumia modem?, mtandao gani huko?
Karibu mkuu..
Rwanda ni pazuri,salama na wala usipate hofu...
Mkuu sijawahi kwenda kwa Bus ila nimekua Kigali several times..ni mji mzuri msafi sana..nimekua naenda na Rwanda Air..sehemu nzuri za kutembelea na nyama choma na bia ni Carwash..hilo ni eneo limetulia sana na jina linaitwa hivo hivo sijui kwanini..
Kingne hotel pale ni aghali sana nenda fikia Impala ni safi na salama ina internet na mambo yote ya kisasa dola 40 per nite.
Mie pia cjawahai kwenda Kigali kwa Bus...zaidi ya KQ au Rwanda Air
ila ni mjini mzuri wenye baridi kdg...kuhusu malazi inategemea na hotel unayofikia mm huwa nafikia Alpha palace au Sports View
sehemu za kutembelea ni Gisenyi na Kivu kwa utalii...maeneo hayo kuna Ndege wanapatikana rwanda wanaitwa Inyange na Pia unaweza kuona sokwe mtu...Rwanda ni Nchi ya Milima na Mabonde...pia unaweza kutembelea ziwa kivu..njian utaona vitu vingi sana..mlima Kivu ambao ni volcano hai..inafuka moshi hadi leo
Sehemu za kuruka disco usiku kuna sehemu inaitwa KBC.....(Kigali Bussiness Centre)...Au Cardrac ambayo iko karibu na Carwash
pia si mbaya ukitembelea Kigali Memorial Centre ukajionea kumbukumbu ya Mauji ya Kimbari...Jengo la Bunge la Rwanda ambapo ndiko kikosi cha kwanza cha jeshi la RPF lilikaa kusubiri muaafaka wa Arusha ..kabla ya ndege ya Rais kulipuliwa...
we fika mkuu utajufunza vitu vingi sana
na Kigali kuna warembo wazuri balaa
Ni hayo tu mkuu
Mimi nimetumia njia zote. Ndege na basi kwa nyakati tofauti. Kwa ndege lazima kupitia Uganda/Entebbe au Nairobi. Mbali ya Rwanda Air pia KQ na ndege moja ya Uganda inakwenda huko.
Kwa njia ya basi, nenda Ubungo. Kama unapanda basi la moja kwa moja utachoka..unless wewe hupendi ku-view sites. Ila uzuri panda gari pale Ubungo la kwenda Kahama. Unalala pale Kahama. Asubuhi unapanda vipanya hadi eneo linaitwa Benaco (just 15kms from Tanzania Rwanda Border -Rusumo). Kutoka Kahama hadi Benaco ni masaa matatu hadi matatu na nusu. Pale Benaco unaweza kupanda taxi (za jumla ya watu4),gharama haizidi elfu3. Ukifika Border unapanda basi za Kigali. Kawaida ni mwendo wa masaa 3-5 kwa gari la abiria kutoka mpakani (Rusumo) hadi Mjini Kigali. Majina ya mabasi ni vigumu, lakini recently basi la TAWAQAL lilikuwa linaenda huko tokea Dar (Ubungo), sijui inawezekana yapo mengine pia. Kwa vyovyote vile lazima unalala Kahama
[/QUOTE][Mgombezi
Tafadhali angalia majibu yangu kuhusu Nauli. QUOTE=Mgombezi;3164479]Asante Sana BUBE kwa maelezo haya, nitashukuru kama utaweza kuniwekea bayana gharama za usafiri zifuatazo:
DAR - KAHAMA = ...Tzs 35,000............... (Japokuwa naweza kuuliza Ubungo)
KAHAMA - BENACO = Tzs 12,000.....................
BENACO - RUSUMO = Tsh 3000 ok
RUSUMO - KIGALI = ..Hapa sijui na kumbuka franks za Rwanda ni strong kuliko madafu ya kitz. Btn Airtel inafanyakazi kule! Unless kumbebadilika siku za karibuni.
Natanguliza shukrani, ukipata wasaa unaweza kunipa dondoo nyinginezo ukioanisha na gharama zake.