Kitendo cha rais wa TFF Walles Karia kulinganisha Bonifasi Wambura na Tundu Lissu kuwa hataki watu wenye utundu Lissu katika soka kuwakela baadhi ya wanachama wa vyama vya upinzani nchini. Hii inaweza kusababisha wanachama wa vyama vya upinzani nchini kuona kuwa viongozi wa vyama vya mchezo nchini ni miongoni mwa wanaovichukia vyama vya upinzani nchini na kupelekea na kupelekea wafuasi wa vyama hivyo kutojitokeza viwanja,na hii inaweza kufanya timu zetu kutofanya vyema kutokana na kukosa hamasa.Namuomba rais huyo siasa awaachie wanasiasa wenyewe na yeye ajikite zaidi katika soka ili timu zetu zifanye vizuri katika soka.Pia nawaomba wote walioguswa na kauli ya TFF kumsamehe Walles na hii isije ikawafanya washabiki wa vyama vya siasa kuingia viwanjani na bendera za vyama vyao badala ya bendera ya taifa au za virabu.