Bw.Daffa
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 420
- 116
Wakuu wote!
Jana nilipata wasaa wa kutembelea maadhimisho ya sikukuu ya wakulima-Nane Nane pale Morogoro kwenye vya Mwl.JK Nyerere.
Kama kawaida watoto na vijana wa makamo(Form 1-4) ndo walikua wengi. Sasa utaratibu wa sherehe hizi kwa kweli unaboa sana.Kwanza hii tabia ya kufanya sherehe hizi kuwa kama soko la wamachinga(najua wote wanatafta rizki) sio mzuri.Nilishangaa kuona watu wengi wapo kwenye kununua viatu,miwani,nguo za mnada n.k wakati kenye bidhaa za kilimo zenyewe watu ni wachache.
Pili hili swala la kufanya Nane Nane ndio soko la kuuza mazao ya kilimo nalo sioni uzuri wake kwani nia ni kueleimisha na sio kuuza sana.Nimeshudia makundi ya kina baba na mama wanaenda tu kununua mboga na matunda,wengi hawana muda wa kuuliza hata jinsi mboga ile inavyolimwa..
Tatu,wazazi wengi wameona Nane Nane ni sehemu ya watoto kwenda kushangaa na hivyo wao hawaendi au wanawapeleka watoto wao.. kwa nyakati tofauti niliskia kina wakisalimiana na wenzao na wakisema "nimewaleta watoto bwana".. Hii ilifanya 80% ya watu wakawa watoto na School boys/girls..
Nne sisi vijana tunadharau kilimo sana.Nimeshuhudia maeneo mengi ya maonyesho yakitembelewa na wazee au vijana wakubwa(roughly with ages above 35yrs). Vijana wa kati ya 18-30yrs wengi nimewaona wakiwa wameshikana mikono na wapenzi wao na walifika kwenye maonyesha kupiga picha tu ila sio kupata elimu flani.
Tano hata wanaohusika wenyewe(Wakulima/Waelimishaji)wame jijengea imani kwamba watu wazima(wamama/wababa) ndio wanaofaa kuelimishwa.. kwa mara kadhaa niliomba kuelimishwa kuhusu Incubators,Greenhouse na nakumbuka hata kwenye kataasisi flani kakutoa mikopo walinipa maelezo kwa kifupi sana(ofcoz am 20's).. tena jamaa wa Incubators akanambia 'hizi vitu ni ghali sana'
Hii iliniskitisha sana mana inadhihirisha kwamba watu wapo pale kufanya biashara na sio kuelimisha!
Wakuu hayo ni mambo ambayo kwa upande wangu sikuyapenda mana yapo kinyume na Adhma ya maadhimisho ya Nane Nane. Pengine kuna mambo ambayo yapo sahihi ila tu sifahamu-tuelimishane. Au na nyie kama kuna mambo mliyaona basi tushirikishane..
Nadhani kuna haja ya serikali kuangalia upya utaritibu huu kwani vinginevyo Lengo litakua halifanikiwi.
Jana nilipata wasaa wa kutembelea maadhimisho ya sikukuu ya wakulima-Nane Nane pale Morogoro kwenye vya Mwl.JK Nyerere.
Kama kawaida watoto na vijana wa makamo(Form 1-4) ndo walikua wengi. Sasa utaratibu wa sherehe hizi kwa kweli unaboa sana.Kwanza hii tabia ya kufanya sherehe hizi kuwa kama soko la wamachinga(najua wote wanatafta rizki) sio mzuri.Nilishangaa kuona watu wengi wapo kwenye kununua viatu,miwani,nguo za mnada n.k wakati kenye bidhaa za kilimo zenyewe watu ni wachache.
Pili hili swala la kufanya Nane Nane ndio soko la kuuza mazao ya kilimo nalo sioni uzuri wake kwani nia ni kueleimisha na sio kuuza sana.Nimeshudia makundi ya kina baba na mama wanaenda tu kununua mboga na matunda,wengi hawana muda wa kuuliza hata jinsi mboga ile inavyolimwa..
Tatu,wazazi wengi wameona Nane Nane ni sehemu ya watoto kwenda kushangaa na hivyo wao hawaendi au wanawapeleka watoto wao.. kwa nyakati tofauti niliskia kina wakisalimiana na wenzao na wakisema "nimewaleta watoto bwana".. Hii ilifanya 80% ya watu wakawa watoto na School boys/girls..
Nne sisi vijana tunadharau kilimo sana.Nimeshuhudia maeneo mengi ya maonyesho yakitembelewa na wazee au vijana wakubwa(roughly with ages above 35yrs). Vijana wa kati ya 18-30yrs wengi nimewaona wakiwa wameshikana mikono na wapenzi wao na walifika kwenye maonyesha kupiga picha tu ila sio kupata elimu flani.
Tano hata wanaohusika wenyewe(Wakulima/Waelimishaji)wame jijengea imani kwamba watu wazima(wamama/wababa) ndio wanaofaa kuelimishwa.. kwa mara kadhaa niliomba kuelimishwa kuhusu Incubators,Greenhouse na nakumbuka hata kwenye kataasisi flani kakutoa mikopo walinipa maelezo kwa kifupi sana(ofcoz am 20's).. tena jamaa wa Incubators akanambia 'hizi vitu ni ghali sana'
Hii iliniskitisha sana mana inadhihirisha kwamba watu wapo pale kufanya biashara na sio kuelimisha!
Wakuu hayo ni mambo ambayo kwa upande wangu sikuyapenda mana yapo kinyume na Adhma ya maadhimisho ya Nane Nane. Pengine kuna mambo ambayo yapo sahihi ila tu sifahamu-tuelimishane. Au na nyie kama kuna mambo mliyaona basi tushirikishane..
Nadhani kuna haja ya serikali kuangalia upya utaritibu huu kwani vinginevyo Lengo litakua halifanikiwi.