Kuhusu Marekani kujiondoa WHO, Hili likoje kisheria?

Kuhusu Marekani kujiondoa WHO, Hili likoje kisheria?

FRANC THE GREAT

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2016
Posts
5,500
Reaction score
8,060
Habari zenu wakuu!

Kwanza kabisa, baada ya Marekani kupitia rais Donald Trump kutangaza kusitisha rasmi mahusiano na Shirika la Afya Duniani WHO, kunaweza kuwa pigo kubwa kwa shirika hilo maana hapo baadaye ndani ya kila miaka miwili shirika litakuwa likizikosa dola za Kimarekani takribani milioni 900, kiasi ambacho ni kikubwa kuliko mchango wa nchi nyingine yeyote ile.

Lakini kabla hatujafika huko, kuna swali la kujiuliza;

Kama Trump alikusudia kuiondoa rasmi Marekani kutoka WHO katika taarifa yake hiyo Ijumaa, suala hilo likoje kisheria?

Kuna mkanganyiko!

Kikanuni, WHO haijaweka wazi kuhusu utaratibu wa wanachama kujiondoa katika shirika hilo kikatiba, suala ambalo linakwenda moja kwa moja katika Mkataba wa Vienna wa mwaka 1969 juu ya Sheria za Mikataba ama kwa lugha nyingine Vienna Convention on the Law of Treaties.

Hapo sasa Marekani itahitajika kutoa notisi ya miezi kumi na miwili (12) kabla ya kujitoa rasmi WHO, chini ya huo Mkataba wa Vienna wa mwaka 1969, unaodhibiti mikataba ya kimataifa.

Maana yake ni kuwa, Marekani bado ni nchi mwanachama wa Shirika la Afya Duniani WHO kulingana na sheria ya kimataifa pamoja na Trump kutangaza kuvunja mahusiano na shirika hilo saa kadhaa zilizopita.

Pia,

Mnamo mwaka 1948 wakati Marekani inajiunga WHO, bunge la Congress nchini humo lilipitisha azimio kwamba nchi hiyo yaweza kujiondoa katika ushirika kwa notisi ya mwaka mmoja, ambalo lilikubaliwa na Shirika la Afya Duniani WHO.

Maana yake ni kwamba, rais Trump anao uhalali kisheria wa kuiondoa Marekani kutoka WHO bila idhini ya Congress lakini kutokana na azimio lililopitishwa na bunge hilo, Trump atalazimika kusubiri mwaka mmoja kabla ya kufanikisha azma yake kama kweli anahitaji kuiondoa Marekani kutoka WHO.

Hivyo basi si jambo la ghafla tu kutangaza kujiondoa bali ni suala lenye mlolongo mrefu kisheria ama kinyume na hapo tunaweza kusema kuwa Trump hakukusudia kujiondoa WHO kama watu wanavyodhani ama alinukuliwa vibaya jambo linaloibua maswali mengi.

Kinachoonekana kwa sasa ni Marekani chini ya Trump kusitisha ufadhili ama fedha kwa shirika hilo katika kipindi cha muda usiofahamika na si jambo la kujiondoa kabisa uanachama wa shirika hilo kwa sasa. Asante!



Karibu kwa maoni!
 
Ahsante kwa taarifa na hoja nzuri. Mie kwa kuwa sio mtaalam wa sheria, nawaachia wajuvi waje kudadavua.

Jambo moja nnalolifaham, Marekani mara nyingi amekua akifanya maamuzi bila kupata kibali cha hayo mashirika, ikiwepo UN. Rejea mashambulizi na vida dhidi ya Iraq na harakati zake za kupambana na ugaidi.

Vile vile kuna nchi nyingi tu zilizoendelea hakuna hata ofisi za UN wala mashirika yao kuwepo kwenye nchi zao lakini wanayafadhili, na kwa mambo yalivyo, hata ukiwa sio mwanachama wa UN, unatakiwa kutii maazimio yaliyopo hata kama wewe sio mwanachama.

Nnachotaka kusema ni kwamba, mkubwa hakosei.
 
USA wao wana jitosheleza katika masuala ya afya wanataasisi nyingi za afya zimesambaa duniani,hawana haja ya kuwa washirika wa WHO,

Sasa hapo china ndio ichukue nafasi iliyoachwa na USA,
Yule director wa WHO angejiuzuru mapema Haya yote yasingetokea

Sema ndio nature ya viongozi wa kiafrika hawawezi kujisacrifice au kuhisi wako responsible kwa makosa yaliyotokea.
 
WACHA ENDE , TUTASLALIMIKA NA SHARI ZAKE
Afrika hatuhitajii chanjo,bali wazungu ndio wanaotuletea magonjwa kisha huleta chanjo ili kutuamgamiza zaidi kwa kutumaliza Immunity zetu, hatimae kutufanya tuwe accessible kwa maradhi mbali mbali ili wao waendeleze viwanda vya vya madawa
 
USA wao wana jitosheleza katika masuala ya afya wanataasisi nyingi za afya zimesambaa duniani,hawana haja ya kuwa washirika wa WHO,

Sasa hapo china ndio ichukue nafasi iliyoachwa na USA,
Yule director wa WHO angejiuzuru mapema Haya yote yasingetokea

Sema ndio nature ya viongozi wa kiafrika hawawezi kujisacrifice au kuhisi wako responsible kwa makosa yaliyotokea.
Viongozi wakiafrika wengi hawapendi kujisacrifice wanapoona wamekosea ila kwahuyu hana kosa lolote nahata hao US waliambiwa walete ushahidi kama wanao mpaka leo wameshindwa kuuleta wamekimbilia kujitoa kwa WHO

Watu wengi wanaweza wakateseka kwakujitoa kwake ama tunaweza kuteseka ila tutaepukana namingi pia

US wanajitengenezea wenyewe mazingira yakupoteza ushawishi katika sekta muhimu DUNIANI naitakua vyema sana maana kwakiasi fulani DUNIA itasalimika nahila zao US wameinyanyasa DUNIA kwakweli nawanaendelea kuinyanyasa navilivyomo
 
Back
Top Bottom