Kuhusu suala la Kagere, Kaduguda umetuachia maswali yasiyo na majibu

Kuhusu suala la Kagere, Kaduguda umetuachia maswali yasiyo na majibu

Fohadi

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2020
Posts
772
Reaction score
2,421
Nilikuwa namsikiliza katika kipindi cha sports arena Mwina Kaduguda akizungumza kuhusu swala la Meddie Kagere kupata nafasi hafifu ya kucheza kwa siku za hivi karibuni. Mashabiki wamekuwa wakilalamika inakuwaje the best striker anakosa nafasi katika kikosi. Point kubwa aliyoizungumza ni Afya ya mchezaji (Kagere). Kaduguda anasema kuwa Simba kwa kushirikiana na FA ya Rwanda walifanikisha matibabu ya Meddie Kagere. Timu ya taifa ilifanikisha kagere kupata nafasi ya kutibiwa ufaransa na simba ikagharamia matibabu yote.

Na ushauri wa daktari ulionesha kuwa Kagere anatakiwa kupewa muda mfupi uwanjani hadi hapo atakapokuwa tayari kucheza dakika 90 (full recovered). Hii ndio sababu ya meddie kagere kupewa muda mfupi kwenye mechi ya plateau kwasababu bado hajapona sawia na simba haitaki kutake risk. Cha kushangaza, baada ya matibabu timu ya kwanza kumtumia kagere ni timu ya taifa ya Rwanda. Akiwa kule amecheza mechi za timu ya taifa na nyingine amemaliza dakika 90.

1. Inakuwaje Timu ya taifa wamchezeshe dakika nyingi huku wakijua ushauri wa daktari hauruhusu hivyo?
2. Inakuwaje Simba hawajalalamika kuhusu mchezaji wao kuchezeshwa dakika nyingi tofauti na ushauri wa daktari?
3. Kama swala lilikuwa ni kutibiwa nje ya nchi, na kama simba ilikuwa na uwezo wa kugharamia gharama zote za matibabu, ilishindikanaje wao wenyewe kumpeleka nje ya nchi bila kushirikiana na FA ya rwanda.
4. Inawezekanaje simba watumie gharama kumtibu mchezaji na wala wasichukue hatua zozote dhidi ya timu ya taifa kwa kurisk kumchezesha mchezaji muda mrefu kinyume na ushauri wa daktari?

Kuhusu swala la kagere kuanza kwa kucheza dakika 90 kule Rwanda baada ya kutoka kwenye matibabu halafu hapo hapo Simba wanampa dakika 15 kufata ushauri wa madaktari, Kaduguda anasema pengine falsafa za walimu (Simba na Rwanda) zimetofautiana. Je, ni faslsafa gani zisizoheshimu ushauri wa madaktari? Hii ni sawa na kunawa baada ya kula.

Kaduguda umeongea, tumeskusikia ila tumeshindwa kukuelewa. Maswali ni mengi sana.​
 
Hapo hapo tujiulize, kama mchezaji hayuko fiti anawekwaje kwenye orodha ya wachezaji wa akiba katika mechi muhimu kama ile?
 
Kuna hawa vijana watatu pale simba Bocco,mzamiru na dilunga hapana aisee kuna shida mahali watu mtasema nina chuki binafisi lakni hapana haiwezekani dilunga ampige bench kahata mzamiru anapataje pale nafasi na kumuacha ndemla nje kama huyu boco kweli ni boco kama jina lake
 
Kuna hawa vijana watatu pale simba Bocco,mzamiru na dilunga hapana aisee kuna shida mahali watu mtasema nina chuki binafisi lakni hapana haiwezekani dilunga ampige bench kahata mzamiru anapataje pale nafasi na kumuacha ndemla nje kama huyu boco kweli ni boco kama jina lake
@GENTAMYCINE aliliongelea hili swala la kupiga misumari wenzao
 
Hapo hapo tujiulize, kama mchezaji hayuko fiti anawekwaje kwenye orodha ya wachezaji wa akiba katika mechi muhimu kama ile?
Nikiongelea generally (sio specific kwa Kagere), ni kitu cha kawaida kwa kocha kumpa dakika chache mchezaji anayetoka kwenye majeraha au ambaye hajawa fit kwa kiwango kikubwa akiwa anatokea katika mapumziko fulani, iwe ya kuumwa au ya kutocheza kwa sababu nyingine, lengo ni kumuandaa kucheza kwa muda mrefu katika mechi zijazo
 
Kwanza habari ya kagere kupelekwa ufaransa kwa matibabu ni uongo, simba wana akaunti zao Instagram, Tweeter na mitandao mingine ya kijamii hii ingeshapostiwa zamani.

Wakati Simba inajiandaa kucheza na yanga kagere alikuwa anafanya mazoezi na timu ya taifa ya Rwanda mpaka unajiuliza inakuwaje Simba wanamwachia kagere wakati kuna mechi muhimu.

Fraga alikuwa mchezaji muhimu sana Simba lakini ameenda kwao ndio kafanyiwa operation hivi Simba walishindwa kumpeleka ufaransa atibiwe.

Kaduguda ni mropokaji tu kuna siasa ndani ya Simba ambayo sio nzuri kwa afya ya timu, mfungaji bora miaka.miwili anawekwa benchi na mtu ambaye wote tunaona kiwango chake ni kidogo.

Kagere alianza kuwekwa benchi muda mrefu pia kuna Rashid Juma, Shibob na Deo Kanda walikuwa wanawekwa benchi na kina Dilunga sasa hivi Kahata naye anasugua benchi wakati wanaopangwa uwezo wao ni mdogo inaonekana kqma wanamtafutia sababu aondoke mwenyewe ili wasilaumiwe na mashabiki.
 
Nikiongelea generally (sio specific kwa Kagere), ni kitu cha kawaida kwa kocha kumpa dakika chache mchezaji anayetoka kwenye majeraha au ambaye hajawa fit kwa kiwango kikubwa akiwa anatokea katika mapumziko fulani, iwe ya kuumwa au ya kutocheza kwa sababu nyingine, lengo ni kumuandaa kucheza kwa muda mrefu katika mechi zijazo
Kimichezo ukishampanga mchezaji substitutions umatake risk maana kuna muda mbadala wake anapata majeruhi within 5 minutes baada ya mechi kuanza utalazimika kumuweka pili kagere kwao anacheza 90 minutes na ukumbuke mara nyingi wachezaji huumia kwenye timu za taifa hii inakaaje akija kwetu anapewa 5 minute kwa kuhofia afya yake.

Ila mpira wetu una uswahili mwingi
 
Kwa kipindi cha miaka 8 iliyopita katika ligi ya bongo..Amis tambwe na Meddie Kagere ndio namba 9 natural niliowaona...Wote wamebeba kiatu cha ufungaji back to back..Takwimu zao zinaongea..gaps wanazoziweka dhidi ya strikers wa timu zingine ni hatari sana...angalia mechi alizocheza kagere msimu huu, halafu pia angalia goals alizo score..Probability ya kagere kufunga ni kubwa kuliko ya Bocco..

Bocco anafunga, sawa ila kwa upande wangu, namuona ni mmoja wa wachezaji wenye bahati tu na sio kipaji...Sometimes maisha ni bahati..Ni kama vile Rashford kuvaa jezi namba 10 ya Manchester united...Hana hadhi hiyo
 
Kwanza habari ya kagere kupelekwa ufaransa kwa matibabu ni uongo, simba wana akaunti zao Instagram, Tweeter na mitandao mingine ya kijamii hii ingeshapostiwa zamani.

Wakati Simba inajiandaa kucheza na yanga kagere alikuwa anafanya mazoezi na timu ya taifa ya Rwanda mpaka unajiuliza inakuwaje Simba wanamwachia kagere wakati kuna mechi muhimu.

Fraga alikuwa mchezaji muhimu sana Simba lakini ameenda kwao ndio kafanyiwa operation hivi Simba walishindwa kumpeleka ufaransa atibiwe.

Kaduguda ni mropokaji tu kuna siasa ndani ya Simba ambayo sio nzuri kwa afya ya timu, mfungaji bora miaka.miwili anawekwa benchi na mtu ambaye wote tunaona kiwango chake ni kidogo.

Kagere alianza kuwekwa benchi muda mrefu pia kuna Rashid Juma, Shibob na Deo Kanda walikuwa wanawekwa benchi na kina Dilunga sasa hivi Kahata naye anasugua benchi wakati wanaopangwa uwezo wao ni mdogo inaonekana kqma wanamtafutia sababu aondoke mwenyewe ili wasilaumiwe na mashabiki.

Viongozi wa soka la bongo wanajua mashabiki zao hawafanyi reasoning. Wanakuja na cheap excuses kwakuwa wanajua asilimia kubwa ya mashabiki ni watu wa kupokea kilivyo na kukiamini bila kufanyia uchambuzi yakinifu...Nilimsikiliza kwa makini mwalimu wangu huyu wa sekondari enzi hizo lakini nimeshindwa kumuelewa...Mpaka sasa bado sijaelewa ni falsafa zipi za kiufundi ambazo zinatofautiana kuhusu afya ya mchezaji..Muda ni mwalimu mzuri sana...Time will tell.
 
Kwanza habari ya kagere kupelekwa ufaransa kwa matibabu ni uongo, simba wana akaunti zao Instagram, Tweeter na mitandao mingine ya kijamii hii ingeshapostiwa zamani.

Wakati Simba inajiandaa kucheza na yanga kagere alikuwa anafanya mazoezi na timu ya taifa ya Rwanda mpaka unajiuliza inakuwaje Simba wanamwachia kagere wakati kuna mechi muhimu.

Fraga alikuwa mchezaji muhimu sana Simba lakini ameenda kwao ndio kafanyiwa operation hivi Simba walishindwa kumpeleka ufaransa atibiwe.

Kaduguda ni mropokaji tu kuna siasa ndani ya Simba ambayo sio nzuri kwa afya ya timu, mfungaji bora miaka.miwili anawekwa benchi na mtu ambaye wote tunaona kiwango chake ni kidogo.

Kagere alianza kuwekwa benchi muda mrefu pia kuna Rashid Juma, Shibob na Deo Kanda walikuwa wanawekwa benchi na kina Dilunga sasa hivi Kahata naye anasugua benchi wakati wanaopangwa uwezo wao ni mdogo inaonekana kqma wanamtafutia sababu aondoke mwenyewe ili wasilaumiwe na mashabiki.
Nitarudi Simba siku nikisikia Sven ameondoka. Simtaki huyu kocha balaa kosa lake kwangu ni mosi kanda na shboub kawaondoa bure tu pili kutumia striker mmoja
Naomba siku zote ifungwe aumbuke Ila kwa bahati anachoka tu km last wiki najua na platinum hachomoki kwa formation zake za kuvuzia Bora mara elf uchebe
 
Nitarudi Simba siku nikisikia Sven ameondoka. Simtaki huyu kocha balaa kosa lake kwangu ni mosi kanda na shboub kawaondoa bure tu pili kutumia striker mmoja
Naomba siku zote ifungwe aumbuke Ila kwa bahati anachoka tu km last wiki najua na platinum hachomoki kwa formation zake za kuvuzia Bora mara elf uchebe
Huyu kocha kazi yake ni kushisha viwango vya wachezaji mechi na plateau nilijilaumu sana kwenda uwanjani nilikuwa naona madudu tu kwani timu ilikuwa inacheza bila mwelekeo wachezaji waliokuwa wanavurunda wanaachwa bila kufanyiwa sub
 
Back
Top Bottom