Kuhusu swala la umeme serikari inatuchukuliaje ?

Kuhusu swala la umeme serikari inatuchukuliaje ?

Mr Mhando

Member
Joined
Nov 2, 2018
Posts
17
Reaction score
20
Hivi serikari yetu inatuchukukiaje wananchi, hivi ni kweli kabisa tumeshindwa kuzalisha umeme wetu wenyewe, Tusichukulie mazoea kwamba sio mala ya kwanza kununua mbona tunanunua zambia umeme wa Rukwa, kwamba kagera umeme wa Uganda, ivi tuna mabwa mangapi?
Tuje tulinganishe kati ya bwawa la Ethiopia na bwawa la mwl nyerere
Kulinganisha Bwawa la Grand Ethiopian Renaissance (GERD) na Bwawa la Mwalimu Nyerere (JNHPP)


GERD nchini Ethiopia na Bwawa la Mwalimu Nyerere nchini Tanzania ni miradi mikubwa ya umeme wa maji barani Afrika.


  • Mahali na Mito: GERD liko kwenye Mto Blue Nile, Ethiopia, wakati Bwawa la Mwalimu Nyerere liko kwenye Mto Rufiji, Tanzania.

  • Urefu na Upana: GERD lina urefu wa 145 m na upana wa 1,780 m, wakati Bwawa la Mwalimu Nyerere lina urefu wa 134 m na upana wa 1,025 m.

  • Uwezo wa Kuhifadhi Maji: GERD linaweza kuhifadhi 74 bilioni m³, mara mbili ya Bwawa la Mwalimu Nyerere, ambalo lina 34 bilioni m³.

  • Uwezo wa Kuzalisha Umeme: GERD lina uwezo wa 6,450 MW (mitambo 13), wakati Bwawa la Mwalimu Nyerere lina 2,115 MW (mitambo 9).

  • Gharama ya Mradi: GERD linagharimu $4.8 bilioni, na Bwawa la Mwalimu Nyerere $2.9 bilioni.

  • Mwaka wa Ujenzi: GERD lilianza kujengwa mwaka 2011, na Bwawa la Mwalimu Nyerere mwaka 2019.
  • Hali ya Sasa: GERD limeanza kuzalisha umeme kwa baadhi ya mitambo, wakati Bwawa la Mwalimu Nyerere linafanyiwa majaribio.

  • Lengo Kuu: GERD linazalisha umeme kwa Ethiopia na kuuza nje, wakati Bwawa la Mwalimu Nyerere linaongeza usambazaji wa umeme Tanzania na kudhibiti mafuriko.
  • Migogoro: GERD limezua mvutano kati ya Ethiopia, Misri, na Sudan, wakati Bwawa la Mwalimu Nyerere linakabiliwa na mijadala ya kimazingira.

Hitimisho


GERD ni kubwa zaidi kwa uwezo wa kuhifadhi maji na kuzalisha umeme lakini linauwezo wa kuzalisha umeme kwa zaidi ya nchi 6, je kwa uwezo wa bwawa la mwl nyerere + Mtera + umeme wa upepo singida tunashindwa kutatua hili swala, Ni aibu sana kwa sisi ngozi nyeusi ikiwa dunia imegama kwa kasi umumu unatengenezwa hadi kwa nucler/uranium ambazo hata kwetu zipo tunakwama wapi, NANI WA KUMFUNGA PAKA KENGERE 😀
 
Uzalendo mdogo sana mambo yanafanyika kwa maslahi yao au ya wengine na sio kwa kuzingatia maslahi ya Tanzania na vizazi vijavyo.
 
Hii nchi viongozi wanatuona mazuzu sana na wanachowaza wao ni kupiga madili tu badala ya kuwaza mambo makubwa ya kuitoa nchi mahali pamoja kwenda pengine!
Ni ajabu sehemu ilizungukwa na mito ya kutosha, maporomoko ya maji, mvua za Mara kwa mara badala ya kwenda sehem Kama pale mtowambu mkatega bwawa la nguvu mnawaza kununua umeme si ukichaa huu!
 
Hivi serikari yetu inatuchukukiaje wananchi, hivi ni kweli kabisa tumeshindwa kuzalisha umeme wetu wenyewe, Tusichukulie mazoea kwamba sio mala ya kwanza kununua mbona tunanunua zambia umeme wa Rukwa, kwamba kagera umeme wa Uganda, ivi tuna mabwa mangapi?
Tuje tulinganishe kati ya bwawa la Ethiopia na bwawa la mwl nyerere
Kulinganisha Bwawa la Grand Ethiopian Renaissance (GERD) na Bwawa la Mwalimu Nyerere (JNHPP)


GERD nchini Ethiopia na Bwawa la Mwalimu Nyerere nchini Tanzania ni miradi mikubwa ya umeme wa maji barani Afrika.


  • Mahali na Mito: GERD liko kwenye Mto Blue Nile, Ethiopia, wakati Bwawa la Mwalimu Nyerere liko kwenye Mto Rufiji, Tanzania.

  • Urefu na Upana: GERD lina urefu wa 145 m na upana wa 1,780 m, wakati Bwawa la Mwalimu Nyerere lina urefu wa 134 m na upana wa 1,025 m.

  • Uwezo wa Kuhifadhi Maji: GERD linaweza kuhifadhi 74 bilioni m³, mara mbili ya Bwawa la Mwalimu Nyerere, ambalo lina 34 bilioni m³.

  • Uwezo wa Kuzalisha Umeme: GERD lina uwezo wa 6,450 MW (mitambo 13), wakati Bwawa la Mwalimu Nyerere lina 2,115 MW (mitambo 9).

  • Gharama ya Mradi: GERD linagharimu $4.8 bilioni, na Bwawa la Mwalimu Nyerere $2.9 bilioni.

  • Mwaka wa Ujenzi: GERD lilianza kujengwa mwaka 2011, na Bwawa la Mwalimu Nyerere mwaka 2019.
  • Hali ya Sasa: GERD limeanza kuzalisha umeme kwa baadhi ya mitambo, wakati Bwawa la Mwalimu Nyerere linafanyiwa majaribio.

  • Lengo Kuu: GERD linazalisha umeme kwa Ethiopia na kuuza nje, wakati Bwawa la Mwalimu Nyerere linaongeza usambazaji wa umeme Tanzania na kudhibiti mafuriko.
  • Migogoro: GERD limezua mvutano kati ya Ethiopia, Misri, na Sudan, wakati Bwawa la Mwalimu Nyerere linakabiliwa na mijadala ya kimazingira.

Hitimisho


GERD ni kubwa zaidi kwa uwezo wa kuhifadhi maji na kuzalisha umeme lakini linauwezo wa kuzalisha umeme kwa zaidi ya nchi 6, je kwa uwezo wa bwawa la mwl nyerere + Mtera + umeme wa upepo singida tunashindwa kutatua hili swala, Ni aibu sana kwa sisi ngozi nyeusi ikiwa dunia imegama kwa kasi umumu unatengenezwa hadi kwa nucler/uranium ambazo hata kwetu zipo tunakwama wapi, NANI WA KUMFUNGA PAKA KENGERE 😀
This is good feasibility analysis. You can't say more.
 
Back
Top Bottom