NguchiroTheElde
Member
- Jun 13, 2010
- 22
- 1
Kuiba kura, kuchakachua matokeo ya uchaguzi ni kitendo cha uhaini kwani ni sawa na kupindua serikali. Serikali halali inachaguliwa na wananchi halafu vibosile vichache vinakaa na kula njama na kuamua kucheza na hizo namba ili aliyeshindwa aonekane kashinda na aliyeshinda aonekane kashindwa. Hilo ni jaribio la kupindua serikali na likifanikiwa mapinduzi yatakuwa yamefanyika.
Kwa hiyo wizi wa kura na kubadilisha matokeo ya chaguzi za wapiga kura ni kitendo cha uhaini na adhabu yake kwa Tanzania inaanzia kifungo cha muda mrefu hadi kifo. Hadi sasa wamekuwa wakilindwa na washirika wao na wanaofaidika na uhaini huo lakini siku tutakayowapata itabidi wajibu shutuma hizo za uhaini na wakihukumiwa kifo tutawanyonga - hata kama watakuwa wameshakufa.
Oliver Cromwel wa Uingereza alipindua serikali lakini baada yake kufa walipata mwanya wa kumshitaki kwa uhaini na alihukumiwa kunyogwa. Kwa hiyo walifukua mifupa yake na kuinyonga! Kwani kufa ndiyo kukukwepeshe kunyongwa?
Kwa hiyo wizi wa kura na kubadilisha matokeo ya chaguzi za wapiga kura ni kitendo cha uhaini na adhabu yake kwa Tanzania inaanzia kifungo cha muda mrefu hadi kifo. Hadi sasa wamekuwa wakilindwa na washirika wao na wanaofaidika na uhaini huo lakini siku tutakayowapata itabidi wajibu shutuma hizo za uhaini na wakihukumiwa kifo tutawanyonga - hata kama watakuwa wameshakufa.
Oliver Cromwel wa Uingereza alipindua serikali lakini baada yake kufa walipata mwanya wa kumshitaki kwa uhaini na alihukumiwa kunyogwa. Kwa hiyo walifukua mifupa yake na kuinyonga! Kwani kufa ndiyo kukukwepeshe kunyongwa?