Kuimarisha mitandao yetu ya kijamii na kuondokana na Utegemezi wa Facebook, WhatsApp na Instagram

Kuimarisha mitandao yetu ya kijamii na kuondokana na Utegemezi wa Facebook, WhatsApp na Instagram

Abdalah Abdulrahman

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2019
Posts
222
Reaction score
202
Idadi ya watumiaji wa mitandao ya kijamii Tanzania imeongezeka kwa kasi na kufikia 4.5 Milioni. Idadi hii imegawanyika katika makundi makubwa mawili,Kundi la kwanza ni wale wanaotumia mitandao ya kijamii kwa manufaa bila kuvunja Sheria,na Kundi la pili ni wale wanaotumia mitandao ya kijamii kwa uhalifu. Idadi ya wanaotumia mitandao ya kijamii kufanya uhalifu ni ndogo ukilinganisha na idadi kubwa ya watumiaji wa mitandao ya kijamii kwa manufaa.

Mitandao ya kijamii kama Jamii Forums, Facebook, Twitter, Instagram, imekua ikiwanufaisha wafanyabiashara,wanasiasa,wakulima na wafanyakazi.Mitandao hiyo hiyo imekua ikitumika na wahalifu kufanya wizi wa fedha,kutukana viongozi,kudhalilisha watu pamoja na kutekeleza jinai zingine.

Tatizo katika mitandao ya kijamii linatokana na uhuru usio na kikwazo ambao unaweza kusababisha madhara makubwa ndani ya jamii.Udhibiti wa mitandao ambayo inatoka nchi zingine ni mgumu kutokana na sheria za zinazolinda ule mtandao wa kijamii.Mfano si kushabikia mapenzi ya jinsia moja kwa mitandao kama Facebook,Twitter,Instagram na WhatsApp,kinyume chake ni kuwa mitandao hii inajali Kundi la watu hawa na inawapa kipaumbele maalumu.

Mifano hii na mingine inaweza kuleta madhara ndani ya nchi kama vile kupenyeza chuki za dini,rangi na ukabila ndani ya jamii.

Zipo nchi kama China,Urusi na zingine ambazo hazitumii mitandao hii ya kijamii kutokana na madhara yanayoweza kupatikana kutokana na matumizi ya mitandao hii.Badala yake imeanzisha mitandao yake ya kijamii na imekua inafaida kubwa kwa nchi na usalama wa nchi.

Nitatoa mifano ya nchi za Afrika ambazo zimewahi kupata hasara kubwa kwa matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii.

1. Misri
Ndani ya nchi ya Misri waandamanaji wachache waliweza kutumia mitandao ya kijamii kupotosha umma na kufanikiwa kuandaa maandamano January 25, 2011 ambayo yalisababisha mapinduzi

2. Tunisia,
Tunisia kama nchi zingine za Afrika ina changamoto ya ajira,changamoto hii ilitumika na wapinzani wa serikali.Kijana mmoja aliamua kujichoma moto kwa kupinga ukosefu wa ajira na kusambaza video hii kwenye mitandao ya kijamii.Watu waliandamana katika miji ya Sfax and Tunis kwa kujiweka pamoja kwa njia ya mitandao ya kijamii. Rais Ben Ali alikimbia na kuacha nchi ikiwa na maandamano yaliyosababisha vifo na hasara kubwa.

3. Kenya
Hali ya Kenya mwaka 2013 inaonesha kuwa wanasiasa walitumia mitandao ya kijamii kwenye kampeni zao.Kampeni hizi ziliibua hisia za ubaguzi na mambo mengine ambayo yalisababisha fujo zilizoua Wakenya wengi.

Hivyo basi uhuru wa mitandao ya kijamii unapaswa kupimwa madhara na faida zake hasa kipindi ambacho ni muhimu kama kipindi cha Uchaguzi. Pia serikali iweke utaratibu wa kuhamishia Wananchi katika mitandao ya kijamii ambayo imesajiliwa nchini kama Jamii Forums ili kudhibiti maudhui.
 
Peleka ombi basi kwa serikali mitandao ya kijamii ifungwe na kusiwepo na mbadala wowote hiyo itapendeza zaidi
 
Unapendekeza tuishi bila mitandao ya kijamii??
Au unapongeza TCRA kutufungia??
Au mimi uelewa wangu mzito sijakuelewa??

Nilifikiri umekuja na mitandao mbadala wa hiyo, badala yake naona unapiga politiki!

Everyday is Saturday............................... 😎
Nashangaa umehoji Swali wakati huyo 'Juha / Popoma' ameonyesha wazi kabisa kutokuwa na Mtandao baada ya TCRA kuamua 'Kipuuzi' kabisa Kutuzimia Watanzania. Na labda asichokijua tu ni kwamba kwa Kitendo hili cha TCRA kufanya huu 'Upuuzi' wao kwa 100% Mapato ya Serikali yamepungua, wamepata Hasara na Kusababisha 'Usumbufu' mkubwa Kwetu. Makampuni ya Simu yakimpata 'Laywer' mzuri kuna uwezekano TCRA wakadaiwa 'Pesa' kama 'Faini' ya kuwalipa ambayo wanaweza Kuliuza Jengo lao hadi na lile la 'aliyewatuma' hapa Dar es Salaam na kule Dodoma.
 
Nashangaa umehoji Swali wakati huyo 'Juha / Popoma' ameonyesha wazi kabisa kutokuwa na Mtandao baada ya TCRA kuamua 'Kipuuzi' kabisa Kutuzimia Watanzania. Na labda asichokijua tu ni kwamba kwa Kitendo hili cha TCRA kufanya huu 'Upuuzi' wao kwa 100% Mapato ya Serikali yamepungua, wamepata Hasara na Kusababisha 'Usumbufu' mkubwa Kwetu. Makampuni ya Simu yakimpata 'Laywer' mzuri kuna uwezekano TCRA wakadaiwa 'Pesa' kama 'Faini' ya kuwalipa ambayo wanaweza Kuliuza Jengo lao hadi na lile la 'aliyewatuma' hapa Dar es Salaam na kule Dodoma.
Tumefeli in the name of "amani". Na huyu mleta mada kawa brainwashed politically. Yaani ni dhahiri huyu ni mnufaika wa hili.

Hali ya mzunguko wa fedha ni mbovu, mtaani hali ngumu, mawasiliano nayo yawe magumu, hawajui ugumu wa maisha waweza kuwa chanzo kikubwa zaidi cha uvunjifu wa amani kuliko hata 'uchafuzi wa kura.'
Njaa na madeni vinaumiza.

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Mtandao wenyewe mmeshindwa kuimalisha je iyo bznes mtaweza?
 
Itachukua muda sana kukuza mtandao hiyo iwe kama Facebook n.k
 
Kuimarisha JF iwe kama FB Au Instagram na WS hiyo hiyo impossible.
Hiyo mitandao ni worldwide dunia nzima inatumia na ni njia pekee ya watu dunia nzima kujumuika kibiashara kuona mambo mbalimbali yanayoendelea duniani in real time pia kuwa na uhusiano na watu tofauti duniani even kuajiriwa nje nk.

Tatizo wewe umeangalia negative pekee ili ujustfy hoja yako ya kuifungia hiyo mitandao.
Wakati positive ni zaidi ya hizo negative considering umeegemea siasa tu.
Au wewe unadhani mitandao ya ndani haiwezi kuhamasisha maandamano?

Ukichangia JF ni forum na tena inatambulika africa mashariki.
Ukifungia hiyo mitandao ni kama kujifungia mwenyewe nyumbani kwako hapo utaweza kuwasiliana na familia yako pekee majirani hutowajua kamwe.

Kiufupi ni sawasawa na kujitenga na dunia na kurudi zama za chuma.
Africans tunatakiwa tukimbizane na kasi ya technology lakini nyie ndo mnaanza kufikiria kuquit race yenyewe.

Think again.
 
Back
Top Bottom