Kuishitaki Star Times katika Tume ya Ushindani wa Kibiashara (FCC)

Kuishitaki Star Times katika Tume ya Ushindani wa Kibiashara (FCC)

Lupweko

JF-Expert Member
Joined
Mar 26, 2009
Posts
23,566
Reaction score
24,891
Wakuu nimejaribu kutafuta contact za Fair Competition Commission (FCC) ili niweze kuishitaki kampuni ya Star Media Ltd maarufu kama Star Times kwa kutangaza bei ya bidhaa ambayo ni tofauti na ile wanayotoza. Ikumbukwe kuwa Star Media ni moja kati ya kampuni tatu zilizopewa zabuni ya kuuza ving'amuzi kwa ajili ya migration from analogue to digital broadcasting. Kampuni nyingine ni Agape Associates Limited and Basic Transmissions Limited.

Hawa jamaa wamekuwa wakitangaza bei ya king'amuzi kimoja kuwa ni "sh. 39,000/= tu"!. Lakini ukienda katika shop/branch zao popote pale Dar es Salaam wanakuambia yafuatayo:
  • Kwamba huwezi kununua king'amuzi bila ya kifurushi (ambacho kidogo sana kinauzwa sh. 9,000/=, kwa hiyo pamoja na king'amuzi minimum jumla unatakiwa kutoa sh. 48,000/= na sio 39,000/= wanayotangaza
  • Kama vile haitoshi, kila shop yao utapewa jibu la kwamba kifurushi cha sh. 9,000/= kimeisha, so walau ununue kinachofuata kwa unafuu wa bei kinachouzwa sh. 18,000/= kwa hiyo pamoja na king'amuzi jumla unatakiwa utoe sh. 57,000/= na sio 39,000/= wanayotangaza.
  • Hawatangazi kuwa unatakiwa ununue antenna yao ili ukamate vizuri signal, lakini ukifika katika shop yao ndio unakutana na vitisho hivyo kuwa signal inaweza kuwa weak kwa kuwa hukutumia antenna yao, so unalazimika kununua.

Sasa mimi ninatamani niyafikishe mambo yote haya katika Tume ya Ushindani wa Kibiashara (FCC), lakini nimesearch website yao nipate contacts bila mafanikio. Anayewajua hawa jamaa wa FCC aniwekee hapa phyisical contacts niwashitaki Star Times. Nadhani nitakuwa nimewajibika kwa upande wangu kuliko kulalamika tu.
 
ngoja wadau waje mkuu watakusaidia contact, hawa jamaa hawana maana TCRA wanatangaza kuwa hivyo ving"amuzi vinalocal chanel zote kama itv na star tv lakini kiukweli hazipo hizo chanel... yaani full kuibiwa tu na haya makampuni wizi kila sehemu, ni ubabaishaji mtupu...pole mkuu
 
Mkuu Jabulani, startimes ni wahuni kabisa. Mambo yao ni kama uliyoandika, nina imani utakuwa umesaidia waTz wengi sana katika hili.
 
Mimi ninawasiwasi na hiyo tume unaweza kuta wana kula 10 yao hapo, si unajua bongo yetu ilivyo?
 
Mimi ninawasiwasi na hiyo tume unaweza kuta wana kula 10 yao hapo, si unajua bongo yetu ilivyo?
Hakuna taabu, cha msingi ni kupata contact zao tutimize wajibu wetu wa kufikisha malalamiko panapohusika. Kama na wao FCC watakuwa sehemu ya uhuni, hilo litakuwa ni suala lingine. Naombeni contacts wakuu
 
Wapo mtaa wa Azikiwe juu ya jengo la Benki ya CRDB - Posta mpya
 
Startimes another scandal in the making of DECI pyramid scheme proportion.
 
Ndugu yangu nimekusikiliza kwa maelezo yako ni kwamba wewe hujaelewa, maelezo yako ni sahihi ila unacholalamikia ni kutoelewa kwako. Ni kama simu inayouzwa sh. 39,000 sasa ili utumie lazima uneunue chip na baada ya chip unatakiwa ukanunue vocha ili utumie kuwasililiana. Sasa kingamuzi kinauzwa 39,000+9000 ya kifurushi=48 ili uone chanels unazotaka na baada ya hapo unatakiwa kulipia sh.9,000 tu kila mwezi tatizo liko wapi? Ukifika mahali ukiwa mtu wa kulalama kama mtoto yatima unatia aibu, siku zote jiweke upande wa positive nachambua mambo kwa mtizamo mpana. Samahani kama nimekujibu vibaya ila nakuelewesha.
 
Ndugu yangu nimekusikiliza kwa maelezo yako ni kwamba wewe hujaelewa, maelezo yako ni sahihi ila unacholalamikia ni kutoelewa kwako. Ni kama simu inayouzwa sh. 39,000 sasa ili utumie lazima uneunue chip na baada ya chip unatakiwa ukanunue vocha ili utumie kuwasililiana. Sasa kingamuzi kinauzwa 39,000+9000 ya kifurushi=48 ili uone chanels unazotaka na baada ya hapo unatakiwa kulipia sh.9,000 tu kila mwezi tatizo liko wapi? Ukifika mahali ukiwa mtu wa kulalama kama mtoto yatima unatia aibu, siku zote jiweke upande wa positive nachambua mambo kwa mtizamo mpana. Samahani kama nimekujibu vibaya ila nakuelewesha.
 
ni kweli mtoa mada,kama walitangaza tena kwa sura kavu za mbuzi kwamba kinauzwa 39,000 na hauhitaji kulipia channels kama hutaki za kununua as local channels 5 zipo hewani,ata kama say umenunua kifurushi cha 9000 na kikaisha 30 days,zile local channels zinaendelea kuwepo hazikatwi kama ilivokua TBC1...
ila kama Jabulani unasema eti ni lazima ununue kifurushi ndipo uone sasa huo ni uhuni na uongo wa yule mkuu/ofisa wa TCRA aliyekua akihojiwa
nilishakipaki siku nyiiingi kile kidude
 
Last edited by a moderator:
ngoja wadau waje mkuu watakusaidia contact, hawa jamaa hawana maana TCRA wanatangaza kuwa hivyo ving"amuzi vinalocal chanel zote kama itv na star tv lakini kiukweli hazipo hizo chanel... yaani full kuibiwa tu na haya makampuni wizi kila sehemu, ni ubabaishaji mtupu...pole mkuu

Local channel pekee isiyolipiwa ni TBC 1 peke yake.
 
Ndugu yangu nimekusikiliza kwa maelezo yako ni kwamba wewe hujaelewa, maelezo yako ni sahihi ila unacholalamikia ni kutoelewa kwako. Ni kama simu inayouzwa sh. 39,000 sasa ili utumie lazima uneunue chip na baada ya chip unatakiwa ukanunue vocha ili utumie kuwasililiana. Sasa kingamuzi kinauzwa 39,000+9000 ya kifurushi=48 ili uone chanels unazotaka na baada ya hapo unatakiwa kulipia sh.9,000 tu kila mwezi tatizo liko wapi? Ukifika mahali ukiwa mtu wa kulalama kama mtoto yatima unatia aibu, siku zote jiweke upande wa positive nachambua mambo kwa mtizamo mpana. Samahani kama nimekujibu vibaya ila nakuelewesha.
Kama huelewi usikurupuke kujidai kutoa majibu, watu watakucheka. Mimi ninataka kununua king'amuzi, wala sihitaji package ya Uhuru, Mambo wala Kilimanjaro. Wao wametangaza kuwa kinauzwa 39,000/- lakini ukienda pale ndio unaambiwa ni lazima ununue na package. Kwa nini wasingeiweka na hiyo bei ya package kwenye matangazo yao? Halafu huo mfano wako wa simu ni very weak. Nikitaka kununua simu ni lazima niitumie kwa mawasiliano? Kama mimi nataka niinunue kwa ajili ya redio au camera, kwa nini unilazimishe ninunue na line ambayo kimsingi haifacilitate chochote katika mahitaji ya radio na camera? Inaelekea wewe ni miongoni mwa wale wasioelewa concept ya digital migration ya TCRA ndio maana umeng'ang'ania malipo ya kifurushi
 
Kama huelewi usikurupuke kujidai kutoa majibu, watu watakucheka. Mimi ninataka kununua king'amuzi, wala sihitaji package ya Uhuru, Mambo wala Kilimanjaro. Wao wametangaza kuwa kinauzwa 39,000/- lakini ukienda pale ndio unaambiwa ni lazima ununue na package. Kwa nini wasingeiweka na hiyo bei ya package kwenye matangazo yao? Halafu huo mfano wako wa simu ni very weak. Nikitaka kununua simu ni lazima niitumie kwa mawasiliano? Kama mimi nataka niinunue kwa ajili ya redio au camera, kwa nini unilazimishe ninunue na line ambayo kimsingi haifacilitate chochote katika mahitaji ya radio na camera? Inaelekea wewe ni miongoni mwa wale wasioelewa concept ya digital migration ya TCRA ndio maana umeng'ang'ania malipo ya kifurushi



Hapa naona hukubali tu kushindwa
 
Wakuu nimejaribu kutafuta contact za Fair Competition Commission (FCC) ili niweze kuishitaki kampuni ya Star Media Ltd maarufu kama Star Times kwa kutangaza bei ya bidhaa ambayo ni tofauti na ile wanayotoza. Ikumbukwe kuwa Star Media ni moja kati ya kampuni tatu zilizopewa zabuni ya kuuza ving'amuzi kwa ajili ya migration from analogue to digital broadcasting. Kampuni nyingine ni Agape Associates Limited and Basic Transmissions Limited.

Hawa jamaa wamekuwa wakitangaza bei ya king'amuzi kimoja kuwa ni "sh. 39,000/= tu"!. Lakini ukienda katika shop/branch zao popote pale Dar es Salaam wanakuambia yafuatayo:
  • Kwamba huwezi kununua king'amuzi bila ya kifurushi (ambacho kidogo sana kinauzwa sh. 9,000/=, kwa hiyo pamoja na king'amuzi minimum jumla unatakiwa kutoa sh. 48,000/= na sio 39,000/= wanayotangaza
  • Kama vile haitoshi, kila shop yao utapewa jibu la kwamba kifurushi cha sh. 9,000/= kimeisha, so walau ununue kinachofuata kwa unafuu wa bei kinachouzwa sh. 18,000/= kwa hiyo pamoja na king'amuzi jumla unatakiwa utoe sh. 57,000/= na sio 39,000/= wanayotangaza.
  • Hawatangazi kuwa unatakiwa ununue antenna yao ili ukamate vizuri signal, lakini ukifika katika shop yao ndio unakutana na vitisho hivyo kuwa signal inaweza kuwa weak kwa kuwa hukutumia antenna yao, so unalazimika kununua.

Sasa mimi ninatamani niyafikishe mambo yote haya katika Tume ya Ushindani wa Kibiashara (FCC), lakini nimesearch website yao nipate contacts bila mafanikio. Anayewajua hawa jamaa wa FCC aniwekee hapa phyisical contacts niwashitaki Star Times. Nadhani nitakuwa nimewajibika kwa upande wangu kuliko kulalamika tu.

Mkuu.. mimi ni mmoja wa wateja wa star times.. japo inakera ila ndio lugha ya biashara... wanajua fika wabongo ukiwapa king'amuzi tupu hawatanunua package yeyote(tunapenda dezo) na hivyo wanakomaa wapate faida haraka wkati wa kipindi hiki kifupi kilichobakiambapo mahitaji ya ving'amuzi ni makubwa... Kuhusu antenna.. kila mtoa huduma atataka teknlolojia na vifaa vyake navyo vitumike..we kama mtumiaji walazimika kunua ili ufaidike na huduma(m.f.. huwezi kutumia voda intanet wakti una modemu ya tigo... labda uchakachue)..."

promosheni yao Hii haina tofauti na promosheni za M-pesa, Tigo Pesa na wengine kuwa unatuma pesa bure (kwa wateja wa mtandao mmoja. Ukituma kwa mteja wa mtandao mwingine walamba salio kama kawa..)

Oni langu: Hoja yako itakuwa na uzito ukisistiza kuwa katika promosheni zao lazima WAWE WAWZAI kuhusu ununuzi wa bishaa zao (kama walivyokomaliwa makampuni ya bia na sigara..) kuondoa usumbufu usio wa lazima kwa wateja!!

Nakupongeza kwa nia..
 
Ngoja ndugu yangu unajua StarTimes ni watu wazuri?kwasababu ukilinganisha bei yao na Dstv,Zuku,ATN au Ting.Startimes wao ni nafuu sana kwasababu huwezi kununua king'amuzi kingine tofauti na StarTimes chini ya 150,000 pia hakuna king'amuzi kingine unaweza kulipa sh 9000 lakini wao unalipa kwamfano dstv bei ya chini ni 16,500 kwahiyo StarTimes nawaheshimu sana hebu fanya utafiti wa tofauti yao kubwa na ving'amuzi vingine une ilivyo kubwa. Usilalamike chochote wewe nunua tu.NAKUTAKIA KAZI NJEMA.
 
ni kama Fast Jet mnatangaziwa naul 48,000 mkifika kukata ticket mnaambiwa laki 3.
kwa nini bei zote zisiwekwe pamoja na hiyo kodi? kuliko kusema kidogo kidogo
 
Wakuu nimejaribu kutafuta contact za Fair Competition Commission (FCC) ili niweze kuishitaki kampuni ya Star Media Ltd maarufu kama Star Times kwa kutangaza bei ya bidhaa ambayo ni tofauti na ile wanayotoza. Ikumbukwe kuwa Star Media ni moja kati ya kampuni tatu zilizopewa zabuni ya kuuza ving'amuzi kwa ajili ya migration from analogue to digital broadcasting. Kampuni nyingine ni Agape Associates Limited and Basic Transmissions Limited.

Hawa jamaa wamekuwa wakitangaza bei ya king'amuzi kimoja kuwa ni "sh. 39,000/= tu"!. Lakini ukienda katika shop/branch zao popote pale Dar es Salaam wanakuambia yafuatayo:
  • Kwamba huwezi kununua king'amuzi bila ya kifurushi (ambacho kidogo sana kinauzwa sh. 9,000/=, kwa hiyo pamoja na king'amuzi minimum jumla unatakiwa kutoa sh. 48,000/= na sio 39,000/= wanayotangaza
  • Kama vile haitoshi, kila shop yao utapewa jibu la kwamba kifurushi cha sh. 9,000/= kimeisha, so walau ununue kinachofuata kwa unafuu wa bei kinachouzwa sh. 18,000/= kwa hiyo pamoja na king'amuzi jumla unatakiwa utoe sh. 57,000/= na sio 39,000/= wanayotangaza.
  • Hawatangazi kuwa unatakiwa ununue antenna yao ili ukamate vizuri signal, lakini ukifika katika shop yao ndio unakutana na vitisho hivyo kuwa signal inaweza kuwa weak kwa kuwa hukutumia antenna yao, so unalazimika kununua.

Sasa mimi ninatamani niyafikishe mambo yote haya katika Tume ya Ushindani wa Kibiashara (FCC), lakini nimesearch website yao nipate contacts bila mafanikio. Anayewajua hawa jamaa wa FCC aniwekee hapa phyisical contacts niwashitaki Star Times. Nadhani nitakuwa nimewajibika kwa upande wangu kuliko kulalamika tu.

hakuna kesi hapo dont waste ur time...........
 
wasikukatishe tamaa ofisi za tume ya ushindani zipo ubungo plaza ila kabla ya kwenda huko inabidi upitie tcra andika barua ya malalmiko tcra hakikisha unaenda na barua mbili moja wagonge mhuri subiri baada ya wiki mbili andika barua tume ya ushindani maana tcra wana mtindo wa kuchelewesha kusikiliza madai watu wengi wananyanyaswa kwa sababu hawadai haki zao wanabaki kulalamika
 
Kisheria utakwama kidogo mkuu jabukani......na utakwamia hapa "vigezo na masharti kuzingatiwa"
 
Back
Top Bottom