Kuishiwa Damu Mwilini

Vamahala

New Member
Joined
Jul 26, 2014
Posts
3
Reaction score
0
Leo nimeambiwa na daktari Kuwa sina damu ya kutosha wakati Mimi ninajiona niko sawa Kabisa; je tatizo linaweza Kuwa ni nini? Ninaomba ufafanuzi wa kitaalamu


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mkuu ulipimwa damu? mimi pia nilipimwa nikaambiwa nna damu kidogo, katika maelezo niliyomueleza daktari ni kuwa si mtumiaji mkubwa wa maji, nikaandikiwa dawa moja ya maji na vidonge nikatumia huku nikishauriwa kula mboga za majani kwa wingi na kunywa maji mengi, tena bora wewe utakuwa umewahi mimi niliumwa hadi nikisima nadondoka, kunywa maji mengi pia fuata ushauri wa daktari.
 
mi hapo ndo huwa sielewagi... hivi damu ikiisha mwilini na kabla ulikuwa.nayo nyingi, huwa inakwend wapi..??? au inageuka kuwa nyama?
 
mi hapo ndo huwa sielewagi... hivi damu ikiisha mwilini na kabla ulikuwa.nayo nyingi, huwa inakwend wapi..??? au inageuka kuwa nyama?

Mkuu inaonekana hujui damu ni kitu gani..ungejua ingekusaidia sana majibu ya maswali yako
 
kwel tumezidiana. mimi nilikuwa nahisi kizunguzungu kila wakat, kwenda kwa daktar na kupima naambiwa nina damu nyingi sana ndo maana napata kizunguzungu. Hivi wakuu hakuna njia ya kufanya nisisikie kizunguzungu, au niwe natoa dam kwa watu, ushauri wenu wakuu
 
Mkuu inaonekana hujui damu ni kitu gani..ungejua ingekusaidia sana majibu ya maswali yako
ungefanya la maana sana kueleza hayo unayodhani siyajui, kuliko kuendelea kunieleza nisiyoyajuwa. hainisaidio mimi wala mwingine aliye kama mimi kwenye ufahamu wa hilo
 

pole sana mkuu...huo ugonjwa ulitaka kuniua wakati niko form one 1998 mtwara tech... hali ilikuwa mbaya sana. nashukuru mungu leo niko pouwa nakunywa lita 3 kwa siku za maji, juice nusu lita na mboga 100 gm
 
pole sana mkuu...huo ugonjwa ulitaka kuniua wakati niko form one 1998 mtwara tech... hali ilikuwa mbaya sana. nashukuru mungu leo niko pouwa nakunywa lita 3 kwa siku za maji, juice nusu lita na mboga 100 gm

Nimeshapoa mkuu, kwa sasa hata mimi nakunywa maji mengi na mboga za majani na matunda kwa wingi, kwani nilikuwa nadondoka mara kwa mara.
 
mi hapo ndo huwa sielewagi... hivi damu ikiisha mwilini na kabla ulikuwa.nayo nyingi, huwa inakwend wapi..??? au inageuka kuwa nyama?

Msinirushie mawe bure..nakupa higlights..

Damu haigeuki nyama mkuu.
Damu ni tissue iliyo katika hali ya kimiminika.

Damu inatengenezwa mwilini sehemu tofauti kama kwenye Ini, bone marrow, spleen (nafikiri kongosho), thymus, stem cells n.k.

Damu pia ina components zake Kama seli za damu, plasma(majimaji) na protini.

Kuisha kwa damu ina maana kadhaaa ikiwemo kukosekana kwa raw material za kuitengeneza, matatizo kwenye sehemu inapotengenezwa na pia kupungua kwa components zake.

Mfano..majimaji(plasma)yatapungua usipoingiza maji mwilini..hivyo volume ya damu itapungua..cells zinakufa daily hivyo seli za damu zisipotengenezwa kureplace zile worn out..pia zitapungua kadhalika Damu tutasema imepungua..

Anzia hapa kujua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…