Kujaza kiasi cha upepo tofauti mbele na nyuma

Kujaza kiasi cha upepo tofauti mbele na nyuma

Makobus

Senior Member
Joined
Jul 30, 2012
Posts
169
Reaction score
110
Habari wanajamvi. Kuna dhana imejengeka kwamba kujaza upepo kiasi sawa katika magurudumu ya mbele na nyuma siyo vizuri kwa utendaji kazi mzuri wa gari. Mara nyingi hupendekezwa mbele kuwe na ujazo mdogo kuliko nyuma.

Kuna ukweli wowote wa kisayansi juu ya dhana hii?
 
Ni juzi tu nilikuwa najiuliza haya maswali baada ya kukuta wamejaza 30 mbele na 40 nyuma. Gari ilipokuja kutoka huko kwao ilikuwa na 40 kote.

Nilipoenda kuweka tairi mpya ndio wakanijazia hivyo. Ikabidi nijaze sawa kama ilivyokua awali 40 Kwa zote nne.

Huwa nawaza, gari zinatofautiana, zipo zinazotumia matairi yote manne, zinazosukuma Kwa kutumia matairi ya nyuma na zinazovuta kutumia matairi ya mbele, Je hiyo Ina athari kwenye kiasi Cha upepo wa matairi?
Izingatiwe katika hizo Hali zote, tairi za mbele ndio zinazoongoza gari Kwa maana ya kubadili uelekeo unapokata Kona.

Tusubirie wataalam kutujuza
 
Mkipata majibu nisaidieni na hili......

Kwa usalama zaidi tairi za gari zinapoanza kuisha za nyuma,wakati unajitafuta kubadili kwa usalama zaidi ni vizuri tairi zilizoisha kufungwa nyuma au mbele....?
 
Mkipata majibu nisaidieni na hili......

Kwa usalama zaidi tairi za gari zinapoanza kuisha za nyuma,wakati unajitafuta kubadili kwa usalama zaidi ni vizuri tairi zilizoisha kufungwa nyuma au mbele....?
Jambo zuri ni kupaki gari mpaka upate pesa haya mengine ni kuhatarisha tu usalama wako na familia yako. Hakuna usalama kwenye tairi chakavu japo kuzifunga mbele ni hatari zaidi.
 
Habari wanajamvi. Kuna dhana imejengeka kwamba kujaza upepo kiasi sawa katika magurudumu ya mbele na nyuma siyo vizuri kwa utendaji kazi mzuri wa gari. Mara nyingi hupendekezwa mbele kuwe na ujazo mdogo kuliko nyuma.

Kuna ukweli wowote wa kisayansi juu ya dhana hii?
Ukifungua mlango wa dereva,kuna sehemu wameandika maelekezo ya tairi,ukubwa na kiasi cha upepo kinachotakiwa. Fuata walichoandika
 
Tatizo hao wanaojaza upepo nao hawana elimu ya gari na magurudumu ndiyo maana wanaojaza jaza tu Kwa uzoefu,ndiyo maana magari mengi yanakosa Wheel balance na kusababisha kuchakaa Kwa tairi !

Pia hata kama unajua kuendesha gari eidha ulifahamu kwasababu kwenu au ujombani au Kwa ndugu zako Kuna magari,ni vema ukaenda chuo ukapata kozi ya Udereva maana huwa inasaidia sana!
 
Kwema wazee, Kwa knowleldge ndogo ambayo ninayo mimi.
Kinachobeba mzigo kwenye tairi ni Upepo.
Logic ya kujaza nyuma upepo (PSI) kubwa ni kwa ajili ya kuhandle mzigo. Hii hua inafanyika zaidi kwenye magari ya mizigo. Standard PSI kwa passenger cars ni 35bars, Lakini wengine hueka 40 kwa sababu unakuta anabeba mizigo ili hata ikipungua inarange na tairi za mbele. Lakini Kitalaam kwa Passenger cars hizi ni vyema ukaweka PSI moja tairi zote Nne.

Pia kuhusu Kufanya rotation ya matairi kwenye gari, Magari mengi (2wheel) yanavutia mbele hivyo husababisha tairi za mbele kuisha haraka zaidi kwa sababu ya traction kati yake na barabara. Lakini pia kiusalama tairi za mbele ndio zinatakiwa kua imara zaidi kwa sababu zile ndio zinasaidia kwenye uelekeo wa gari(Rotation), Endapo ikapasuka tairi ya mbele ukiwa kwenye high speed unahatari zaidi ya kupata ajali mbaya kuliko ile ya nyuma ambayo haizunguki kulia na kushoto(Rotation). Hivyo Basi kitalaam ili tairi zote ziishe kwa uwiano sawa na ziwe salama atleast kila baada ya km5000 unafanya rotation, either za mbele kwenda nyuma na nyuma mbele, au unafanya full circle rotation ambayo kila tairi inahama kwenda kwa mwingine mpaka spare tire.
 
maelekezo ya ujazaji WA tire kwenye magari mara nyingi huwekwa kwenye mlango wa dereva hivyo si magari yote hujazwa upepo mwingi nyuma mfano BMW upepo mbele ndo unapaswa kuwa mwingi ila magari yetu haya mbele mara nyingi huandikwa upepo uwe mdogo na logic ni kwamba gari iwe na drag force nzuri tairi za nyuma zinavutwa na tairi za mbele hivyo upepo ukiwa mdogo maana yake utakua unazilamisha kwa nguvu kuzunguka. lakini pia tairi za mbele ndo zinazotoa mwelekeo wa ngapi upepo mdogo husaidi tairi kushikamana na Barbara vizuri na kusaidia gari kutokuhama hama. Zaidi kwa maisha marefu ya shockup na ma bush unashauriwa usijaze upepo mwingi tofauti na zilizoandikwa na mtengeneza gari
 
Hii theory ina apply kwenye Phoenix yangu au ni kwa wenye mandinga tu??

1722620009471.png
 
Kila gari ina recommendation zake kwenye ujazo wa upepo ili kuleta balance nzuri ni lazima upepo utofautiane maana uzito wa gari unapishana mbele na nyuma, sehemu yenye mzigo mkubwa inatakiwa kuwa na upepo zaidi ya ile yenye mzigo mdogo sasa mafundi wetu wa vichochoroni wanakwambia mbele weka kidogo wakati magari mengi mbele mazito.

Kila gari ina muongozo wake wa upepo mlango wa upande wa dereva una maelezo yote
 
Back
Top Bottom