Kujiajiri VS Kuajiriwa

Kujiajiri VS Kuajiriwa

Masokotz

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2018
Posts
3,713
Reaction score
6,121
Habari za asubuhi;
Kama kawaida huwa kuna maamuzi mengi magumu ya kufanya katika maisha,baadhi yake ikiwa ni uamuzi wa ama kujiajiri au kuajiriwa.

Uamuzi au uchaguzi huu mara nyingi haufanywi na mtu kwa hiari yake bale husukumwa na circumstance pamoja na fursa.Wengi wa waliojariwa ni kwa sababu waliomba ajira wakapata na wengi ambao hawajaajiriwa ni kwa sababu ama hawakupata ajira au walipa fursa.

Vyovyote vile uamuzi wowote huwa na msukumo bila kujali uwezo binafsi wa mtu.

Ni ukweli usiopingika kwamba kama utaajiriwa au kujiajiri bado ugumu utakua pale pale na usifikiri kwamba ugumu ulioko kwenye kujiajiri basi utaondoka pale ukiajiriwa au ugumu ulioko kwenye kuajiriwa utaondokana nao ukijiajiri hapana.Changamoto na zile zile.

Tofauti kati ya kuajiriwa ama kujiajiri ni ndogo sana na kwamba vyovyote utakavyochagua kuna kanuni za msingi zitakufunga.Baadhi ya kanuni hizi ni bidii,ubunifu,uvumilivu.Zinahitajika katika ajira na kujiajri na ni msingi wa mafanikio.

Unapojiajiri,utafanya kazi overtime lakini hutadai malipo ya overtime,ili ukipiga faida kubwa ni yako yote.Ukiajiriwa utalipwa overtime ila ukizalisha faida kubwa utakula ujira wako tu.

Ukijiajir jiandae pia kuajiri watu kama kweli unataka kukua kibiashara.Unapoajiri watu tambua kwamba baadhi yao watakuwa na fikra kama zako,na ndoto za kujiajiri hivyo waheshimu sana.

Ukiajiri muheshimu sana boss wako na ufanye kazi kwa bidii kwani itakujengea nidhamu na kukuwezesha kumudu kazi zako pindi uamuapo kujiajiri.

Usikimbilia kujiajri kama wewe ni mvivu asiyekuwa na nidhamu ya kazi.Usikimbilie kujiajiri kama hujaona fursa ya uhakika,Usikimbilie kujiajiri kama hujajianda kubadili kabisa mfumo wako wa maisha.Kujiajiri sio kichaka cha watu wavivu na wazembe.

Yote kwa yote,Iwapo kwa sababu yoyote ile umeamua au kulazimik kujiajiri au kuajiriwa basi fahamu kuwa msingi wa mafanikio yako ni Nidhamu,bidii na uvumilivu bila kusahau ubunifu.

Uwe na wakati mwema
 
Sawa kabisa nakubaliana na wewe ila fahamu mwisho wa siku lazima ujiajiri.Huwezi kuajiriwa milele. Pili kujiajiri ni sahihi zaidi kuliko kuajiriwa.Huwezi kumrithisha mtu yeyoye yule ajira yako.

Tatu mtizamo wangu kati ya kuajiriwa na kujiajiri ni mkubwa sana.Ukichunguza watu wenye mafanikio ya kimaisha na kiuchumi ni watu waloojiajiri.Sifa tu muhimu ni bidii na maarifa.
 
Yaani kuajiriwa sio kabisa lakini ni uvivu wa kufikiri tu ndio tunakomaa na makampuni ya watu... Ukistaafu bado utazungushwa kulipwa, yaani shida tu.
 
Kiukweli kujiari ni kuzuri na kunanufaisha kuliko kuajiriwa mimi nilikuwa nafanya kazi inanichosha Sana wiki nzimq nipo kazini kuondoka asubuh kuliko usku afu msharaha ndo hvyo hauelewiki sasa ivi nimejiajiri napata pesa nzuri kuliko msharahara niliyokuwa nalipwa kujiajiri ni kuzuri sana.

Sent from my TECNO B1f using JamiiForums mobile app
Unafanya biashara gani
 
Pesa ya ajira tamu wewe.Ikifika mwisho wa mwezi unaelekea benki huku ukitabasamu.
 
Habari za asubuhi;
Kama kawaida huwa kuna maamuzi mengi magumu ya kufanya katika maisha,baadhi yake ikiwa ni uamuzi wa ama kujiajiri au kuajiriwa.

Uamuzi au uchaguzi huu mara nyingi haufanywi na mtu kwa hiari yake bale husukumwa na circumstance pamoja na fursa.Wengi wa waliojariwa ni kwa sababu waliomba ajira wakapata na wengi ambao hawajaajiriwa ni kwa sababu ama hawakupata ajira au walipa fursa.

Vyovyote vile uamuzi wowote huwa na msukumo bila kujali uwezo binafsi wa mtu.

Ni ukweli usiopingika kwamba kama utaajiriwa au kujiajiri bado ugumu utakua pale pale na usifikiri kwamba ugumu ulioko kwenye kujiajiri basi utaondoka pale ukiajiriwa au ugumu ulioko kwenye kuajiriwa utaondokana nao ukijiajiri hapana.Changamoto na zile zile.

Tofauti kati ya kuajiriwa ama kujiajiri ni ndogo sana na kwamba vyovyote utakavyochagua kuna kanuni za msingi zitakufunga.Baadhi ya kanuni hizi ni bidii,ubunifu,uvumilivu.Zinahitajika katika ajira na kujiajri na ni msingi wa mafanikio.

Unapojiajiri,utafanya kazi overtime lakini hutadai malipo ya overtime,ili ukipiga faida kubwa ni yako yote.Ukiajiriwa utalipwa overtime ila ukizalisha faida kubwa utakula ujira wako tu.

Ukijiajir jiandae pia kuajiri watu kama kweli unataka kukua kibiashara.Unapoajiri watu tambua kwamba baadhi yao watakuwa na fikra kama zako,na ndoto za kujiajiri hivyo waheshimu sana.

Ukiajiri muheshimu sana boss wako na ufanye kazi kwa bidii kwani itakujengea nidhamu na kukuwezesha kumudu kazi zako pindi uamuapo kujiajiri.

Usikimbilia kujiajri kama wewe ni mvivu asiyekuwa na nidhamu ya kazi.Usikimbilie kujiajiri kama hujaona fursa ya uhakika,Usikimbilie kujiajiri kama hujajianda kubadili kabisa mfumo wako wa maisha.Kujiajiri sio kichaka cha watu wavivu na wazembe.

Yote kwa yote,Iwapo kwa sababu yoyote ile umeamua au kulazimik kujiajiri au kuajiriwa basi fahamu kuwa msingi wa mafanikio yako ni Nidhamu,bidii na uvumilivu bila kusahau ubunifu.

Uwe na wakati mwema
Well said Boss...ingawa naona mtu aliyejiajiri anakua hana frastuation kubwa sana kama yule aliye ajiriwa....
 
Ujue watu wanashindwa kuelewa vizuri faida na hasara za kuajiliwa na kujiajili na lazima uangalie vitu furani kwenye maisha ndio utapata jibu sahihi mfano;

Kama unataka kuijia kwenye biashara au kuajiliwa lazima ujue yafuatayo;

1: Je mimi nina miaka mingapi
2: Je nina familia inayo nitegemea, Kama ndio?
3: Kipato changu cha kiasi gani unaweza kuaendeshea familia kwa mwezi?
4: Kama hauna familia je nina watu wanaonitegemea na wanaweza kuishi kwa kipato cha kiasi gani kwa mwezi?
5 Nimeshawai kufanya biashara yeyote iwe ya kununua na kuuza au ya kutoa huduma?
6: Natumia Muda gani kwa siku kwenye hiyo biashara?

Hayo ni maswali ya kujiuliza kabla ya kufanya maamuzi ya kuchangua upande upi ni sahihi kwako. Kuna muda Kufanya biashara ni zuri zaidi na kuna wakati kufanya kazi ni zuri zaidi lakini kuna muda kufanya vyote kwa pamoja ni zuri zaidi ... kwa ajili ya kuwa na maisha bora.

Sijui kuandika... Samahanini sana
 
Ukiwatambua hawa watu vizuri hutaona tofauti kati ya kuajiriwa na kujiajiri kamwe, vyote vinategemea sana Tabia binafsi PERSONALITIES au Entrepreneurial traits

Hapo kuna Entrepreneur (Mjasriamali)(Kujiajiri) na Intrapreneur(Mjasriakazi)(Kuajiriwa)

Huyo huyo mtu mmoja popote akienda atafanikiwa na kama ni wa kufail popote anaweza fail japo pia tegemea na factors zingine au mazingira kutofautiana.
Changamoto ziko pale pale.

Tatizo tulilonalo Watanzania jamii yetu imetokea kwenye siasa ya ujamaa, kwa maana hiyo hatuna Role Model wa kutosha kwenye Ujasriakazi(Intrapreneur) Kuajiriwa.

Wapo watu wameajiriwa(DEO) na mafanikio makubwa sana kuliko hata matajiri na makampuni yao kwa Siasa zetu za kitanzania mtawaita majina ya ajabu ajabu.

Mfano aliyekuwa 1.CEO wa shrika moja la makazi kumbuka mapato yake(mshahara)
2. Aliyekuwa CEO wa safari com marehemu Bob Collymore mapato yake
3. Aliwahi kuwa waziri mkuu hapa kwetu, angalia makampuni yake na mapato yake

Hao wote hapo juu na wengine wengi ni INTRAPRENEURS - WAAJIRIWA MATAJIRI
 
Nimefundisha kwa miaka mitano sikua na hata akiba ya mil. kwenye account nimejiajiri ninajenga na nina akiba kwa account.
Kujiajiri uko vizuri mngekua mnatoa na mifano halisi labda upo kwenye harakati zipi za kujiajiri ili tuweze kutathmini
 
Kujiajiri uko vizuri mngekua mnatoa na mifano halisi labda upo kwenye harakat zipi za kujiajiri ili tuweze kutathmini
Nafanya biashara ya samaki spare za pikipiki na kulima mazao ya muda mfupi japo nalima kwa timing sana.
 
Kujiajiri msoto mkubwa tena mkubwa sana sio wa kitoto
 
Back
Top Bottom