Kujishusha!!.....

nimekusamehe lakini sitokusahau aliimba nani tena???

Unaomba msamaha hata kama kosa si lako ndo solution mambo yaishe na maisha yaendelee mbele

kama husahau,basi hujasamehe....
 
Looo mie sehemu hizo huwa sirembi, napiga mzigo kwanza nikimaliza kama kununa niendelee kununa

Dah, sipati picha hii huwa inakuwaje,
yaani mnuno unakuwa umeuweka pending, kisha mzigo kama kawa!!lol.....
I wish i would be there watching you..................................
 
kama husahau,basi hujasamehe....

lol...samahani wapendwa kama ntakuwa nimechakachua huu uzi,
lakini sio kusudio langu wajameni,
kuna siku nilisikia hoja kutoka kwa jamaa mmoja anadai kwenye ndoa,
cha msingi ni upendo na wala sio uvumilivu,
Upendo ndo kila kitu, lakini uvumilivu unatoa picha kuwa,
unakuwa na mwenzako hata kama amekukosea basi unavumilia tu,
mabaya yake, uovu wake; vyote unaendelea kuvivumilia kwakuwa,
kwenye ndoa unapaswa kuvumilia ili maisha yaendelee.
Lakini laiti kama ukiwa na upendo kwa mwenzio basi hayo mengine yanakuja automatically.


Hitimisho:''Uvumilivu sio component ya msingi kwenye ndoa"

sijui ukweli ni upi hapo!!!!!!!!
Kwaherini na samahani kama nimewachakachulia uzi,
najua hata Mungu hapaendi!!!!!!
 
Its funny unajua

watu watakuambia be urself.....halafu utaambiwa vumilia.....

Wakati wengine tukiwa ourselves hatuna uvumilivu lol

funny...........
 
Kama mnamapenzi ya kweli sidhani kama hivo visasi vitakuwepo.

Hata mimi naona jambo la kujishusha linatakiwa luchukuliwe kwa busara kwasababu nia ni kurudisha hali ya amani na mawasiliano mazuri..kwahiyo visasi si vizuri kabisa.


Ni vizuri linapotokea tatizo wote mkajishusha,mkazungumza kisha mkajua nani mwenye tatizo halafu yakaisha kwa amani na furaha!

Kweli inatia moyo kuona wenza wanajishusha na kujadili matatizo halafu hali ya furaha irejee..

Kibaya zaidi wanawake wengi mnagombana asubuhi

mnayamaliza....

Wewe unafikiri yameisha......

Sasa pale jioni unapotaka game......ndo yanaaaanza upyaaaaaaaaaa....

Talaka mnatafutaga wenyewe kwa kweli

Kwakweli sisi wanawake tupo so emotional, hivyo basi mpaka akili ikubali matatizo yameisha na kila kitu kingine kinafanya kazi..

Uwe unabembeleza The Boss, halafu kumbuka kumwambia kama sisi tumegombana vile vitu viwili vinahitaji haki yake na havina mgogoro..atacheka na kuishia kuenjoy game na wewe!!
 

Bacha mi nafikiri cha myuhimu hapo ni Upendo na uvumilivu uwe kiasi .ule tu wa kuyavumilia mapungufu ya mwenzi wako yale aliyoumbwa nayo na si yale atakayoyafanya kwa makusudi.
Ukiwa na upendo huwezimtenda mwenzio hivyo hakakuwa na sehemu ya kuexercise uvumilivu unaosemwa
Ukiwa na upendo huwezikwazwa na mwenzio kwa yale ambayo ni mapungufu yake ya kibinaadamu, hivyo hutapata pa kuexercise uvumilivu wako BUT
Ukiwa na upendo HUTOSITA kumvumilia mwenzio pale ambapo amepungukiwa............

Ila

Ukiwa na Uvumilivu bila upendo iko siku utashindwa kuvumilia zaidi
Ukiwa na uvumilivu bila upendo, utayabaini mapungufu ya mwenzio mengi (na mengine si mapungufu bali umeyafanya wewe yawe mapungufu)
Ukiwa na Uvumilivu bila upendo, hutojali mahitaji ya kimapenzi ya mwenzako.................

Kifupi
Upendo huambatana na uvumilivu- ni pacha but
Uvumilivu hukinzana na upendo
 

Mwanajamii1, umefafanua vizuri tena kuhusiana na situations. nadhani suala la kujishusha liwe linafikiriwa na pande zote mbili, mtu akiwa amekosea aweze kuomba msamaha..
 
Nimekusamehe lakini sitokusahau aliimba nani tena???

Unaomba msamaha hata kama kosa si lako ndo solution mambo yaishe na maisha yaendelee mbele

Ila ukweli ni kwamba kusahau mambo mengi ni ngumu, hiyo ni kazi ya ubongo🙂he he

Halafu inaelekea kuna watu wengine wanapenda sana kuombwa msamaha..napenda life iendelee lakini mtu anakuwa amemaanisha kwa msamaha?au inakuwa tu mazoea laa mkosaji nae haelewi kuwa yeye ndie alichemsha..du!

Dah, sipati picha hii huwa inakuwaje,
yaani mnuno unakuwa umeuweka pending, kisha mzigo kama kawa!!lol.....
I wish i would be there watching you..................................

He he..honestly, ni wachache sana wanaweza kufanya hivi..
wanawake wakinuna mpaka akili irejee kwenye majamboz siyo kuweka pending. ila ingekuwa vyema sana kuweka kinyongo pembeni na kufurahia tendo wote..
 
Mwanajamii1, umefafanua vizuri tena kuhusiana na situations. nadhani suala la kujishusha liwe linafikiriwa na pande zote mbili, mtu akiwa amekosea aweze kuomba msamaha..

Mpenzi kama nilivyosema inategemea mtu na mtu pia.......mie nilishawahiona mtu anakosea yeye (tena makusudi) halafu anakuwa mkali anapandisha sijui yalikuwa maruhani yale na akimaliza hapo anaongezea na dozi ya mnuno...wiki hadi umbembeleze. Ukisema unakomaa eti kosa ni lako sijui nini .....ukitoka kazini jioni utakuta amefungasha virago kavipanga mlangoni, anatishia kuondoka. Unaamua tu yaishe na unayazika maana siku ukisema leo mukide ngoja nitoe dukuduku ndo unaliamsha upyaaaa.

Acheni tu
 

Bacha naona umekokotoa kweli leo suala la upendo vs uvumilivu..Naamini pia upendo unabeba kila kitu kwenye mahusiano/ndoa kwasababu ukiwa unampenda mtu unaweza kumvumilia na kuwa nae bega kwa bega regardless ya weakness aliyonayo..pia kwa upendo huo huo, mkikwaruzana unaelewa ni part ya maisha hivyo unamsamehe na kuendelea nae.
Je kuna watu wana upendo wa dhati na hawana uvumilivu?
 
Kibaya zaidi wanawake wengi mnagombana asubuhi

mnayamaliza....

Wewe unafikiri yameisha......

Sasa pale jioni unapotaka game......ndo yanaaaanza upyaaaaaaaaaa....

Talaka mnatafutaga wenyewe kwa kweli

kweli mkuu hii inapata watu wengi sana..mda ukitaka maneno anaanza ohh unajua mimi hiki sikupenda sasa hiyo ni nini!!! ndio maana mtu unaamua kuiba sasa
 

Ni sawa ila nadhani ni vema ukacheza ngoma kama inavyopigwa na sio ivumavyo maana ikivuma sana mwisho huwa mnaujua.
Hivyo mwenzio akipanda panda akishuka shuka namaana moja lazima uwe na ile hali ya woga kuwa ukipanda au ukijishusha sana kunathari yake haijalishi mwanamke au mwanaume.{ukijishusha sana kunakudharaulika au kujipandikiza utumwa b'se omba omba huzidisha unyonge na ukipanda sana kumbuka ujasiri ukizidi huwa ukatili lazima uogope ndo maana hata jasiri huingia vita kabeba sila cause hujua kuna kufa} Chamsingi ni busara ya usuluhishi kufuata mkondo wake, baba mama na mtoto huwa na majukumu sawa katika familia directly and indirect be contigence. It doesn't cost.
 

Huko kwa kutia unyonge sifiki babaaangu!I do ot reasonably....
 


Asante MJ1,
Nimeipenda hiyo conclusion!!!!!!!
 

BJ,

Kwenye hizi ndoa zetu, tena sie wa 1947, lazima kuna mmoja atalazimika kuwa kiazi (mjinga mjinga) ili mambo yaende. Na bahari mbaya (kwa uzoefu wangu), wanaume ndiyo huchukua hiyo nafasi. Na kwa wale wanaomudu kufanya hivyo ila wakabaki na akili, busara na hekima ya kuongoza familia zao basi ndoa zao hudumu ukilinganisha na wale ambao wanakuwa wajinga zaidi na kulala fofo au wanakuwa ngangari!

Mhhh...Ngoja kwanza nikatafute ugali.....Sukari inaniishia mu kichwa!
 
mimi ninachopinga ni kuwa the price ya kuifanya ndoa idumu isiwe kubwaa saana
mpaka raha isiwepo.....
 
mimi ninachopinga ni kuwa the price ya kuifanya ndoa idumu isiwe kubwaa saana
mpaka raha isiwepo.....
Una akili kama babu yangu....ndoa sio mapambano...watu wanapambana mpaka kukosa usingizi eti ili tu ndo iwepo!!!
 
mimi ninachopinga ni kuwa the price ya kuifanya ndoa idumu isiwe kubwaa saana
mpaka raha isiwepo.....

Kweli mkuu,

Ila nadhani wanaume wengi wanamudu kulipa hiyo price kwa sababu wana cushioning mechanism. Hata hivyo hizo mbinu mwisho wa siku huwaumiza wanawake!

Ni mambo magumu haya....tuwape pole na kuwaonea huruma ambao ndoa zao zimegeuka kuwa kaa la moto!
 
Huko kwa kutia unyonge sifiki babaaangu!I do ot reasonably....

Hivyo ukweli ni kwamba kuwa tayari kuchukua uamuzi mgumu ni sehemu ya maisha ya mapenzi au ndoa ile kuepusha shari ambazo ni -ve.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…