Kujiunga bando kwa vocha na Halopesa kunatofautiana kasi ya kuisha

Dabil

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2021
Posts
6,823
Reaction score
15,293
Sijui kama kuna mtu ameona hili kwa halotel na Tigo, ukijiunga MB kwa kuingiza vocha ni tofauti na kujiunga moja kwa moja kutoka halopesa au Tigo Pesa.

Kujiunga kwa vocha mb zinakaa ila kujiunga kwa halopesa au tigo pesa mb zinaenda kwa kasi.

Nikijiunga kwa vocha GB 1 naweza kukaa siku 3 hadi 4 lakini kwa halopesa inaisha siku hiyo hiyo.

Sijui kama kuna aliyeexperience hili.
 
Ngoja nijaribu nitaleta mrejesho..
 
Daah inawezekana mkuu, nimekuwa nashangaa siku hizi 1 gb inaisha ndani ya siku mbili na mimi huwa najiunga kwa tigo pesa. Hii imepelekea hadi baadh ya apps nimepunguza kutumia kama bile ig, twitter lkn wapi shida bado iko pale pale.
 
Tunakuwa tunawaibia sema hamjui,Itasoma 1gb ila tunwaoa mb 600 tu
 
It seems kuna ukweli..
Last week gb 1.3 ilikaa wiki nzima.
Ila jana nimeingia 1.3 leo zimebaki mb600
 
Halotel dikuhizi ni
Sikuhizi hao Halotel ni wezi zaidi ya vibaka wa keko, unajiunga bando la internet la 1 GB ndani ya nusu saa unaambiwa umetumia 75% ya matumizi yako yote, labda kwa kucheck vitu bila ku download chochote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…