Mvaa Tai
JF-Expert Member
- Aug 11, 2009
- 6,158
- 4,449
Wadau mwenzenu nimejaaliwa kuwa na marafiki wengi sana ukiachilia mbali wale niliofahamiana nao katika maisha ya shule na nika-maintain urafiki nao, lakini bado katika mazingira ya kazi na maisha ya mtaani napendelea sana ku keep in touch na watu wengi sana ambao nakutana nao. Kama mjuavyo watu wengi maisha huanza kwa kuwa wapangaji, hapa Dar maisha nilianzia Manzese nilikaa mwaka mmoja na nikajikuta nina marafiki kibao, nikahamia Sinza nikapata marafiki kibao, Nikahamia Tabata nikajipatia marafiki kibao, nikahamia Mbezi Tank Bovu nikajipatia marafiki pia, na mwisho nipo Tegeta nako nimepata marafiki wapya wengi tuu na kama kawaida huwa na keep in touch Miaka yoote nimekuwa nafanya hivyo kwa makusudi kabisa kwasababu nimekuwa nikisikia kwamba kujuana na watu wengi(Networks) ni kitu muhimu sana.
Mpaka sasa sijajua umuhimu wa kujuana na watu wengi zaidi ya Usumbufu, kwa mfano hapa nilipo nina kadi kumi na nane 18 za michango ya Harusi, Send offs, Vipaimara, Anniversaries nk. Haishii hapo nina SMS Tatu zinaniomba nihudhulie hizi weekend mbili bila kukosa vikao vya kwanza vya Harusi na Sendoffs.
Kujuana na watu wengi kumenifanya ghalama zangu za kuishi ziwe kubwa sana. Nifanye nini ili uwingi wa marafiki zangu na mimi uninufaishe???
Mpaka sasa sijajua umuhimu wa kujuana na watu wengi zaidi ya Usumbufu, kwa mfano hapa nilipo nina kadi kumi na nane 18 za michango ya Harusi, Send offs, Vipaimara, Anniversaries nk. Haishii hapo nina SMS Tatu zinaniomba nihudhulie hizi weekend mbili bila kukosa vikao vya kwanza vya Harusi na Sendoffs.
Kujuana na watu wengi kumenifanya ghalama zangu za kuishi ziwe kubwa sana. Nifanye nini ili uwingi wa marafiki zangu na mimi uninufaishe???